Mapenzi ni matashi (wills); na upendo (love) ni wema wa ndani wa mtu kwa mtu mwingine. Kwa hiyo mtu kuwa na mapenzi ya kweli maana yake ni kuwa na matashi ya dhati kwa mtu/watu wengine. Kwa jumla mapenzi ni aspect ya upendo kwani upendo ndiyo unaofumbata kila jema. Na hapa unakuta maneno kama "mapenzi ya Mungu" na "Upendo wa Mungu". Mapenzi ya Mungu ni utashi wake, nia yake, yale awatakiayo wanadamu, amri zake na maelekezo yake. Upendo wa Mungu ni wema wake.