Kuna uhusiano wowote wa uganga na hivi vitu?

Kuna uhusiano wowote wa uganga na hivi vitu?

Mgaigai

Member
Joined
Nov 20, 2021
Posts
44
Reaction score
70
Habarini wakubwa,

Kuna mzee mmoja huwa anapendelea sana kununua daftari lile lisilo na mistari (la kuchora),Marker pen nyekundu na udi.

Mwanzo sikuelewa nikaamua nimuulize jamaa Fulani hivi wa hapa mtaani ,akaniambia ni Mambo ya uganga.

Je,ni kweli hivyo vitu tajwa hapo juu vina uhusiano na uganga.

Naomba kuwasilisha.

JPEG_20230227_132112_9072964219222720494.jpg
JPEG_20230227_132140_6842885059319955419.jpg
JPEG_20230227_132210_7594368966250491956.jpg
 
Mchawi usually ana kitabu( usually kitabu cheusi),anaandika mule ndani magic spells zake anazotumia. ANAANDIKA KWA MKONO WAKE.
 
We sema umeagizwa ndo unajiuliza hizi mavitu mganga aenda kufanyia nn
 
Habarini wakubwa,

Kuna mzee mmoja huwa anapendelea sana kununua daftari lile lisilo na mistari (la kuchora),Marker pen nyekundu na udi.

Mwanzo sikuelewa nikaamua nimuulize jamaa Fulani hivi wa hapa mtaani ,akaniambia ni Mambo ya uganga.

Je,ni kweli hivyo vitu tajwa hapo juu vina uhusiano na uganga.

Naomba kuwasilisha.

View attachment 2531545View attachment 2531546View attachment 2531549

Umenikumbusha mbali sana hilo lilikuwa linaitwa Daftari la Sanaa. Sijui kama watoto wanatumia siku hizi.
 
Habarini wakubwa,

Kuna mzee mmoja huwa anapendelea sana kununua daftari lile lisilo na mistari (la kuchora),Marker pen nyekundu na udi.

Mwanzo sikuelewa nikaamua nimuulize jamaa Fulani hivi wa hapa mtaani ,akaniambia ni Mambo ya uganga.

Je,ni kweli hivyo vitu tajwa hapo juu vina uhusiano na uganga.

Naomba kuwasilisha.

View attachment 2531545View attachment 2531546View attachment 2531549
Ndio vina uhusiano hasa katika kuandika tarasimu...kwa mfano hii ni tarasimu ya kuvuta pesa mwilini mwako imeandikwa na wino wa peni hiyo na kufukizwa na udi huo..Ni shirki kama shirki zingine na shirki siku zote huwa ni dhambi do at your own risk
FB_IMG_1676313829979.jpg
 
Habarini wakubwa,

Kuna mzee mmoja huwa anapendelea sana kununua daftari lile lisilo na mistari (la kuchora),Marker pen nyekundu na udi.

Mwanzo sikuelewa nikaamua nimuulize jamaa Fulani hivi wa hapa mtaani ,akaniambia ni Mambo ya uganga.

Je,ni kweli hivyo vitu tajwa hapo juu vina uhusiano na uganga.

Naomba kuwasilisha.

View attachment 2531545View attachment 2531546View attachment 2531549
Ni lowest ingredients za uganga na hakuna mtu anatumia hivi isipokuwa waganga mafukara sana ambao wateja wao huwalipa elfu 5 hadi 20 ili kuweza kufanyiwa mambo yao na vile tu ni watu ambao wanafanya uganga ili kuweza kupata chochote kinywa hivyo haoni shida kupokea elfu 10 au 5 yako kwa ajili ya kukutengenezea dawa zilizojaa uongo na utapeli;

Marker pen:
Katika uganga kalamu hii hutumika kuandikia nazi na mayai ambayo kuandika kwake nia na talasimu husika ili iweze kufanya kazi vema na maandishi yabakie pale bila kufutika;
Sio lazima kutumia marker pen nyekundu basi wengi hupenda kutumia hiyo ajili ni nzuri rangi yake katika kutishia amani watu kuwa imeandikwa labda kwa damu au nini.

Karatasi nyeupe;

Hii hutumika kuandikia makombe na spells tofauti tofauti ili kuweza kufanikisha spells ambazo zinahitaji kuandikwa mfano kwenye ngozi za wanyama fulani ama madini fulani ambayo kama muhusika hana uwezo wa kupata basi atatumia karatasi nyeupe ambayo haina kitu nayo effect zake katika kazi za utabibu ni ndogo sana unless kinachoandikwa hapo ni Maneno ya mwenyezi Mungu kwa imani yoyote katika kutegemea mwenyezi Mungu kufanikisha hilo.


Udi;
Kuna aina nyingi za udi nazo kila moja ina harufu yake na kazi yake lakini kazi kubwa ya udi ni kunukia harufu ambazo roho ya muhusika hupenda na kuondoa harufu mbaya au uvundo sehemu husika. Yes inaweza pia kutumika kwa kuondosha harufu ya bangi eneo husika lakini madhara yake ni makubwa.


Conclusion:
  1. Moshi wa udi sio chakula cha majini wala hautoi nguvu yoyote katika kufanya spell ama amali yoyote ya kimaarifa kijini,kiganga,kitiba wala kichawi ni vitimbi kama vitimbi vingine:
  2. Chakula cha majini ni Moshi wa bukhuri tofauti tofauti na selective sana, ikiwa ni pamoja na juu ya mifupa na vyakula vya kawaida anavyokula binadamu visivyo vyenye kutoka kwa wanyama na pia damu za wanyama ni binadamu ni kama kilevi tu kwa baadhi ya majini
  3. Huyo anaenunua hivyo vitu usimuhukumu kwa dhana zako kwa maana hujui anaenda kufanyia nini labda anakwenda kuandikia mirathi au kuchora lebo kwenye baadhi ya vitu. Na pia vile vile anaweza kuwa ni tapeli wa uganga kama matapeli wengine tu wasiojua madhara ya miaka mitano baadae.
  4. Usichangie mada kwa jambo usilolijua kwa maana wenye kujua watakuona ni mjinga ama huna maarifa.
Mwenye kuuliza ni mwenye kujifunza.

Rakims
 
Ndio vina uhusiano hasa katika kuandika tarasimu...kwa mfano hii ni tarasimu ya kuvuta pesa mwilini mwako imeandikwa na wino wa peni hiyo na kufukizwa na udi huo..Ni shirki kama shirki zingine na shirki siku zote huwa ni dhambi do at your own riskView attachment 2531600
Well hiki unachofanya sio sahihi na sio sawa kwa maana unahamasisha watu wenye uelewa mdogo kuhusu mambo haya kuthubutu kufanya kitu wasichokijua kwanza umeanza na mkwala kwamba hii ni shirki lakini ajabu mwisho wa siku unafundisha watu kuwa wakifanya watapata nini?

Kwenye hali ya sasa hivi ambayo mtu hawazi haramu wala halali unaweka sanaa yoyote ile lazima atathubutu tu. Wapo watakao kufuata PM na kukuomba uwape maelezo kamili kisha baada ya hapo utaigiza kama vile sio muhusika na baadae utataka uwadirect kwa muhusika na kutoa ladha nzima ya kile ulichopost na kunadi kwamba ni SHIRKI na unajikuta wewe ni agent wa hiyo shirki.

Nimekukosoa wewe kama umekasirika tukana sijali.

Kisha namkosoa aliyekuonyesha ama kukupa hii kitu na kudai kwamba inavuta pesa. Ikivuta pesa niite mbwa nimekaa hapa kwenye quote yako.

JIBU LA KIMAARIFA:
Kwanza kabisa hii sio talasimu ya kuvuta pesa haina ukweli wowote na ina madhara kwa asilimia 99.99%.

tuitizame,
Tukianza Ina shamsi katikati yaani alama ya kuwakilisha jua ambayo ni nishati ya kila kiiumbe hai na ambacho kisicho hai na inawakilishwa na nyota ya pembe tano ambayo ni utawala wa jumapili yenye thamani ya herufi F kwa maana ya Jina la Mwenyezi Mungu Farid (MMOJA) nyota yenyewe imekaa upande ikielekea zaidi upande wa kushoto imechorwa kwa wino wa blue ambayo ni rangi kinzani ya jua na pia na wino uliotumika ni wa kalamu za chemical ambazo hazina uhusiano wowote na buhuri zilizopo katika sayari (nyota) ya jua.

Pili: Jina linalozunguka hapo HASHAMSHAHAYNI ambalo ni jina la jini anayetawaliwa na watumishi wa malaika Izrael (Azrael) malaika mtoa roho za watu hivyo utawala wa mkuu wao wa chini ni Abu muhriz Al Hamar katika majini na Phaleg katika mashetani uandishi uliotumika hapo ni wa MIRIKHI ambayo ni utawala wa DAMU,MAAFA,VITA na MAANGAMIZI.

Tatu; Shikeli iliyotumika hapo ni Amisio ambayo ni kinyume cha Aquisto hivyo;
Amisio ni shikeli ya kukosa na Aquisto ni shikeli ya Kupata

Nne; Mpangilio wa talasimu za sayari hapo juu ni FA JA ZA kisha zikamalizikia na SHA KHA ZA moja kwa moja ni baina ya sayari 6 katika mpangilio wa vurugu jua mwezi na zuhura kwa pamoja na Jua Mushtara na Zuhura.

TARGET YA TALASIMU HII:
Hii talasimu malengo yake ni kumfilisi yeyote yule atakaye kuwa nayo na hatapata mafanikio na mafanikio kwake ayaone kama ukoma kila fursa awe anaiona ni tatizo,
Hii mlenga alitaka kumpa mlengwa ili afilisike ama aweze kufa maskini.

HITIMISHO 1:
yaani mtizamo wa talasimu hili ni vijakazi wamekuwa wafalme na wafalme wamekuwa vijakazi. Hana tofauti na mtu mwenye kusema baba alale na mtoto na mtoto alale na mama kingono hapo utakuwa umetukana familia ya watu. watakachokufanya mbona utaenda kuchekea chooni.

HITIMISHO 2:
Msipeane vitu msivyovijua maana zake kwa maana mtaleteana matatizo wenyewe kwa wenyewe Imagine mwenye kubeba talasimu hii hana tofauti na muandamanaji aliyebeba bango la kutukana uongozi wenye hasira kali na watu kama yeye.
Ukitumia talasimu malengo yake na results huanza hapo hapo unapokuwa umeipokea sasa embu kaa nayo muda fulani kisha utaona mbivu na mbichi mwenye kuishi miaka alfu moja hana tatizo kukusubiri ujisahau ukifika miaka arobaini na tano ili akuchekeshee chooni. watu wengi wanajiangamiza wao na familia zao kwa kushiriki wasio yajua.

Binafsi sishauri mtu apokee kitu pasipokuwa na msaada wa wenye kujua.

Rakims
 
Back
Top Bottom