wastani kwa idadi
JF-Expert Member
- Jun 28, 2024
- 503
- 1,432
Mfano kwa hapa Tanzania kila mkoa uwe na serikali yake,
Kuna ukweli huu mfumo unaweza kuleta ukabila au udini ?
Kuna ukweli huu mfumo unaweza kuleta ukabila au udini ?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Si kweliMfano kwa hapa Tz kila mkoa uwe na serikali yake, kuna ukweli kiasi gani itachochea ukabila ?
Shinyanga tumezalisha Almasi miaka yote hiyo tangu utawala wa Mwalimu lakini hakuna Stand ya mabasi ya maana, Bora hii nchi igawanywe kimajimbo Kila sehemu ineemeke kivyake.Wataalam wa politics, kuna ukweli kiasi gani kwamba kila jimbo likiwa na serikali yake kutachochea ukabila ?
Mfano kwa hapa Tz kila mkoa uwe na serikali yake
Makabila yanatofautiana kwa idadi, mkoa unaweza kuwa na makabila 10 lakini kabila moja ni asilimia kubwaUkabila upi, wakati mikoa inayounda Jimbo inamakabila tofauti?. Mfano chukulia Jimbo la magharibu litakua na makabila mangapi na ukabila utatoka wapi?.
Mfano kwa hapa Tanzania kila mkoa uwe na serikali yake, kuna ukweli gani itachochea ukabila au udini ?
Kwa Tanzania tukifuata huu mfumo itabidi majimbo yawe mikoa badala ya wilaya / halmashauri..sio kila mkoa.
..ni kila JIMBO.
..Na hakuna jimbo ambako wanaishi kabila moja.
..kabla ya mikoa kuundwa, Tanganyika ilikuwa imegawanywa ktk majimbo nane kama sikosei.
..Na kipindi hicho hakukuwa na ukabila kwani tuliweza kupigania uhuru wa Tanganyika kwa umoja bila kubaguana kikabila.
Sio lazima kila mkoa uwe jimbo.Kwa Tanzania tukifuata huu mfumo itabidi majimbo yawe mikoa,
Kenya kuna majimbo 47, Nairobi ni jimbo na huku kwetu DSM itabidi iwe jimbo moja
Kila mkoa kuna administrative regional office hivyo ni rahisi ku assume kila mkoa utakuwa jimbo, kuna baadhi ya mikoa inaweza kuanzishwa na mingine kuunganishwaSio lazima kila mkoa uwe jimbo.
KIla mkoa unatakiwa kuwa jimbo. Kinyume na hapo kunakuwa hakuna chochote cha maana kilichofanyika.Kila mkoa kuna administrative regional office hivyo ni rahisi ku assume kila mkoa utakuwa jimbo, kuna baadhi ya mikoa inaweza kuanzishwa na mingine kuunganishwa
Kuna mikoa haiendelei kwasababu ya upigaji na wapigaji watu wake, Pesa zinatolewa kuendeleza miradi, zinaishia mifukoni mwa madiwani, halmashauri, chama ngazi ya mkoa, n.k.Huu mfumo unafaa sana asee.Kuna mikoa inatoa rasilimali nyingi lakini wana hali mbaya kuanzia uchumi,miundombinu mpaka elimu.
Upigaji ni tatizo mtambuka kwa nchi nzima.Kuna mikoa haiendelei kwasababu ya upigaji, Pesa zinatolewa kuendeleza miradi, zinaishia mifukoni mwa madiwani, halmashauri, chama ngazi ya mkoa, n.k.
Mfano mdogo ni Bukoba, wametoa mawaziri kibao wenye power ya kupanga bajeti lakini mkoa hauna maendeleo ila ni hao mawaziri wanaita milioni 50 pesa ya mboga
Upigaji ni tatizo ila viwango vimetofautiana, Kama mbunge kapata nyadhifa nzito ya uwaziri na bado kashindwa kusimamia miradi jimbo lake au kapiga pesa za miradi, hilo tatizo haliwezi kutatuliwa na serikali ya majimbo.Upigaji ni tatizo mtambuka kwa nchi nzima.
Wahaya mkoa wao umepauka bwana asikwambie mtu,wana ardhi nzuri yenye rutuba,hali ya hewa mwanana kabisa lakini mkoa umefubaa sana.
Acha kuwaamini vilaza waliojazana si si emu. Hata kwenye uraia pacha ukiwauliza sababu za kuupinga, utaisha tu kucheka kwa dharau na kutikisa kichwa.