OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 426
- 685
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali kila mwaka wa fedha baada ya kutoa ripoti ya ukaguzi hutoa mapendekezo ili kuongeza ufanisi wa taasisi na kudhibiti upotevu wa fedha na mapato ya serikali. Hata hivyo mapendekezo machache hutekelezwa hali inayotia mashaka kwa nini CAG anaendelea kuwepo ikiwa mapendekezo yake hayatekelezwi ipasavyo
Ripto ya mwaka wa fedha 2020/21 imeonesha kuwa mapendekezo 10,824 ya 2019/20 kwa serikali za mtaa mengi hayakufanyiwa kazi i.e. 36% hayakutekelezwa kikamilifu, 13% yamejirudia, 34% yapo katika hatua mbalimbali za utekelezwaji, yaani kama wameanza tu kuonesha lakini ndio hadi mwaka unapita?. Hata hivyo 17% yamepuuzwa. Yaliyofanyiwa kazi kikamilifu ni 0%.
Je suala la uwajibikaji linakuwa wapi ikiwa mapendekezo ya CAG hayatekelezwi.?
Ripto ya mwaka wa fedha 2020/21 imeonesha kuwa mapendekezo 10,824 ya 2019/20 kwa serikali za mtaa mengi hayakufanyiwa kazi i.e. 36% hayakutekelezwa kikamilifu, 13% yamejirudia, 34% yapo katika hatua mbalimbali za utekelezwaji, yaani kama wameanza tu kuonesha lakini ndio hadi mwaka unapita?. Hata hivyo 17% yamepuuzwa. Yaliyofanyiwa kazi kikamilifu ni 0%.
Je suala la uwajibikaji linakuwa wapi ikiwa mapendekezo ya CAG hayatekelezwi.?