Kuna umuhimu wa leseni ya biashara ya TRA mapema kabla sijaanza ,ninataka kuanza biashara ya duka la

MENISON

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2013
Posts
726
Reaction score
621
Msaada mimi ni mgeni kabisa kwenye biashara ,frame ninayo ninataka nianze biashara lakini haya mambo sijui ya TRA na TIN number ,naweza kutafuta sasahivi au badae? na wanafuatilia hata vibiashara vidogo vya uswahilini?
 
Msaada mimi ni mgeni kabisa kwenye biashara ,frame ninayo ninataka nianze biashara lakini haya mambo sijui ya TRA na TIN number ,naweza kutafuta sasahivi au badae? na wanafuatilia hata vibiashara vidogo vya uswahilini?

TIN namba hutolewa bure we fika ktk ofisi yoyote ya TRA utaipata ikiwa ni pamoja na kupata taratibu zingine za kodi.
 
biashara ndogo ni ipi mkuu?
Mtaji wako ni bei gani?
Kama ni Genge la mboga na matunda , hawatafika!!
 
biashara ndogo ni ipi mkuu?
Mtaji wako ni bei gani?
Kama ni Genge la mboga na matunda , hawatafika!!

mil 1 .5 nguo za kike na watoto ndio ntaanza nazo
 
Wale TRA wala hawatoi TIN bure kama wanavyojitangaza. Mimi nimekwenda pale marakadhaa eti wanalazimisha kwanza nilipe pesa, jamani hivi hii ndiyo haki? Kwanini mna lazimisha watunwalipe kwanza? Kama mtu asingekuwa na nia ya kulipa kodi wala asingethubutu kuja ofisini kwenu. Unakuta mtu hata bado hajaanza biashara , jamaa wanalazimisha ulipe kwanza...aghaa
 
hata mi ni mefatilia tin. nikawa na imani bure wala si bure eti wananipigia pesa na yolipa pango 50,000 kwa mwezi mara mwezi 6 unapata laki 3 ×10% +5000 haya kesho uje nayo tukupe tin na upige pix na finger print
sasa pango nalipa kwa mwenye nyumba na kodi ya mapato ya chumba zigo langu mimi mh hatari lakini ndo bongo.badala wamfuate baba nyumba alipe hiyo kodi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…