Kuna umuhimu wa mimi kupiga kura tena?



Umenena kuongeza ni kuharibu tutafakari hizi bold zikifanyiwa kazi anachotaka chrispin kitakuwa
 
I suggest uache kupiga kura uangalie njia nyingine nyingi za kujiongezea kipato!

Nakushukuru mdau kwa point yako nzuri, haiwezekani kila siku nikawa looser halafu niendelee kuhangaika na kupiga kura.
 
Piga kura my pal.
Every vote counts, hata kama jamaa hatashinda..


Inauma sana, unampigia kura mtu anayeamini anakufaa. Na mazingira yanaonyesha atapata ushindi wa kishindo. Badala yake linashinda lijitu jingine, halina jipya.
 

Umevaa viatu vyangu mkuu.
 
kwakuwa kila unayempigia anashindwa nakushauri yule usiyemtaka ndio umpigie ili ashindwe
 

Kwa mantiki hiyo ndugu yangu, bila mabadiliko katika tume ya uchaguzi na kuyafanyia marekebisho mapungufu yote, kuna sababu gani ya kupiga kura? Sio wizi huu? Kwanini nipige kura wakati najua fika hata nifanyeje mgombea nayeona anafaa hatashinda?
 
mimi nazani wewe ndio unajua lipi bora
1. kati ya ambaye hujampigia kura na ameshinda je umeona kuna mambo ya maana aliyo fanya.
2 kama kuna mambo ya maana aliyo fanya je huyo uliye mtaka je angeweza kufanya zaidi yake. kama ameweza kufanya zaidi yake itabidi ujutie ila kama hajafanya na ameharibu zaidi nazani inabidi ujivunie sana kwa machaguo yako.

kwa mfano mimi nipo kama wewe hakuna ambaye nilisha wahi kumpigia akashinda ila mpaka sasa hivyi nafarijika kuwa katika haya madudu yanayo fanya na viongozi walio kuwa madarakani mimi sikuwapendekeza wala kushiriki kuwaweka. ingawa naumia ila ningeumia zaidi kama kura yangu ndiyo ingekuwa imechangia kumuweka.


kitendo cha kuacha kupiga kura ni kibaya zaidi kwa mfano uliye mtaka angeshidwa kwa kura moja nazani ungejisika vibaya sana na ungeihukumu hiyo siku kwa kufanya kosa kushiriki kufanya kosa la kihistoria
piga kura kwa unayezani atakuletea maendeleo yako na ya tanzania sio kwa unaye zani atashinda. na kama unayezani atakaye kuletea maendeleo ana possibility ndogo ya kushinda ni jukumu lako kusaidia ili aweze kushinda kwa mfano unaweza kuwashawishi watu kwa nini huyo ni bora zaidi ya huyo mwingine. mpaka hapo utakuwa umefanya majukumu yako yote na hakuna atakaye kulaumu katika kizazi hiki na vyingine vyijavyo ndugu yangu.
 
Mkuu,tupo sawa kabitha..
Mi pia nimeanza kupiga kura 2000,kunzia diwani,mbunge,mpaka rais wote niliwapigia wapinzani,wakakosa....2005 zoezi likawa vilevile,wakakosa......
Sikati tamaa kamwe mkuu,nitaendelea kupiga kura kwa wapinzani km wagombea wao watakuwa wakiniridhisha kwa sera.km sera mbovu, nalala home,lakini ccm nooooooo1


mkuu endelelea kupiga kura,hivi ni vita usirudi nyuma,daima nenda mbele..ukirudi tu umewapa mwanya maadui.
 


Kinachokera ni kupoteza muda wangu bure. Nasimama kwenye foleni kutwa nzima nampigia kura mpiganaji lakini anapigwa mweleka wa kifisadi. Heri angeshindwa kihalali ningeelewa, lakini anashindwa kwa wizi wa kura!
 

1.Walioshinda hakuna hata moja la maana walilofanya zaidi ya kuongeza kero
2. Hakuna jema alilofanya kwa hiyo naamini hakustahili kuchaguliwa. Niliyempigia kura angefanya mazuri zaidi ya aliyeshinda kiwiziwizi.
 
Mie mwakani kura yangu ninampa Kingunge Ngombale Mwiru maana hataki kustaafu ila anataka kufia pale mjengoni.
 
kama walio shinda wameharibu kwanza hongera sana na inabidi ujipongeze sana kwani wewe hujahusika kwenye kuwaweka viongozi wabaya madarakani kwa hiyo hutahukumiwa kwa hilo (ninaposema kuhukumiwa ni naama nafsi yako haita kuhukumu wala laana ya vyizazi vijavyo haita pata uzao wako.

sasa kwenye la kupiga kura usinge piga kura nazani ungekuwa unawajibika katika matatizo kwani kukaa kimya kwako tungejua unamsaport.

huyo mbunge uliye naye siku zote anajua kuwa kuna watu hawamkubali na mmja wao ni wewe kwa hio anafanya hayo kwa wale wanao mkubali ila we sio mmoja wao.

piga kura siku zote usiache haki yako ya msingi mi nakumbuka mwaka 2005 ili nibidi nisafiri usiku mzima ili niende kupigA KURA NAMPAKA SASA NAFARIJIKA KUWA NILIYE MPIGIA HAKUPATA ILA ALIYE SHINDA NA KUFANYA UTUMBO SIO CHAGUA LANGU,.
 
Mkuu una moyo mgumu kama wa kobe! Hongera kwa ujasiri huo.
 

Niko jimbo la KAWE.
 
Mimi nakushauri uwapigie CCM ama yoyote unayotaka ashindwe kwa kuwa takwimu zako zinonesha wazi kwamba umpigiae kura siku zote hushindwa.
 


Mwakani mpigie JK atashinda!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…