mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,227
- 6,670
Kinachoendelea nchini kwa sasa, kisiasa, kuna viashiria vya kijamii na kiuchumi kwamba huenda ndio mwisho wa utawala wa CCM.
KIJAMII
Kuna matukio kadhaa makubwa ambayo yanamomonyoa misingi imara ya usalama wa kijamii. Matukio hayo, yanayotokana na uongozi wa CCM, ni kama vile wanasiasa wa upinzani:
[emoji830]︎ kunyanyaswa;
[emoji830]︎ kutekwa;
[emoji830]︎ kujeruiwa;
[emoji830]︎ kufunguliwa mashtaka, nk.
Matukio hayo yanathiri siyo tu viongozi hao wa siasa bali pia, na hasahasa, familia zao, ndugu na marafiki. Ikizingatiwa kuwa ni karne ya TEHAMA, matukio hayo siyo siri tena.
Kwa sababu hiyo kizazi kipya, kitakachopiga kura 2025, kinajenga chuki dhidi ya utawala uliopo.
KIUCHUMI
Miaka mitano ya utawala wa Awamu ya Tano, miradi mingi ya kimkakati, ujenzi na uboreshaji wa miundo mbinu ya usafiri na huduma za jamii (afya, elimu, maji) zilifanyika kwa pesa za ndani kutokana na kodi za wafanya biashara wakubwa ambao awali walikwepa kulipa.
Awamu iliyoko madarakani, pamoja na kuwabana wanyonge kwa tozo, misaada na mikopo ya nje, pia imewapunguzia kodi wawekezaji ili kuwavutia.
Mikakati hiyo ya kiuchumi, hakuna shaka inawaweka wanyonge, wengi wao vijana, katika hali ngumu. Isitoshe, jeshi hilo la vijana, liko kwenye sekta isiyo rasmi, ambayo kwa bahati mbaya au kwa makusudi, utawala ulioko madarakani, haujawatendea haki inayostahili. Mazingira yao ya kufanya biashara, na shughuli zingine za kiuchumi, siyo rafiki kama awamu iliyopita.
Je, ni viashiria vya mwisho wa utawala wa CCM?
KIJAMII
Kuna matukio kadhaa makubwa ambayo yanamomonyoa misingi imara ya usalama wa kijamii. Matukio hayo, yanayotokana na uongozi wa CCM, ni kama vile wanasiasa wa upinzani:
[emoji830]︎ kunyanyaswa;
[emoji830]︎ kutekwa;
[emoji830]︎ kujeruiwa;
[emoji830]︎ kufunguliwa mashtaka, nk.
Matukio hayo yanathiri siyo tu viongozi hao wa siasa bali pia, na hasahasa, familia zao, ndugu na marafiki. Ikizingatiwa kuwa ni karne ya TEHAMA, matukio hayo siyo siri tena.
Kwa sababu hiyo kizazi kipya, kitakachopiga kura 2025, kinajenga chuki dhidi ya utawala uliopo.
KIUCHUMI
Miaka mitano ya utawala wa Awamu ya Tano, miradi mingi ya kimkakati, ujenzi na uboreshaji wa miundo mbinu ya usafiri na huduma za jamii (afya, elimu, maji) zilifanyika kwa pesa za ndani kutokana na kodi za wafanya biashara wakubwa ambao awali walikwepa kulipa.
Awamu iliyoko madarakani, pamoja na kuwabana wanyonge kwa tozo, misaada na mikopo ya nje, pia imewapunguzia kodi wawekezaji ili kuwavutia.
Mikakati hiyo ya kiuchumi, hakuna shaka inawaweka wanyonge, wengi wao vijana, katika hali ngumu. Isitoshe, jeshi hilo la vijana, liko kwenye sekta isiyo rasmi, ambayo kwa bahati mbaya au kwa makusudi, utawala ulioko madarakani, haujawatendea haki inayostahili. Mazingira yao ya kufanya biashara, na shughuli zingine za kiuchumi, siyo rafiki kama awamu iliyopita.
Je, ni viashiria vya mwisho wa utawala wa CCM?