Kuna wakati dawa pekee ya maumivu ni kukubali ukweli kuwa unaumia

Kuna wakati dawa pekee ya maumivu ni kukubali ukweli kuwa unaumia

Daudi Kempu

Member
Joined
Dec 6, 2024
Posts
26
Reaction score
56
Utofauti ni kuwa, wewe unaumia sasa hivi, mwenzako aliumia jana, mwingine aliumia juzi, na mwingine aliumia miaka mingi iliyopita.

Umewahi kujiuliza, kama hayo maumivu utaishi nayo miaka kumi zaidi, yatakuumba kuwa kiumbe cha aina gani?

Kila mtu ana zamani yake ambayo, kama ingewezekana angeifuta kwa kifutio cha moto; isahaulike kama haikuwako mwanzo.

Zamani ni kama tu makovu; mengi ni ngumu kufutika. Na kadri tunavyojitahidi kuyafuta, pasi na utulivu tunaambulia kutengeneza majeraha mapya.

Hakuna namna utaumia zaidi ya vile umeruhusu.

Nakubali, maumivu huja mahali yasipotarajiwa kabla ndo maana huutafuna sana moyo.

Kuvunjwa moyo, hutokea kwa watu tuliowaamini kuliko namna tunaweza elezea, ndo maana kuna muda tunahisi kukata tamaa.

Lakini, ni sawa vile tunavyojitendea'ga' baada ya kupitia uzoefu huo mchungu?

Ni sawa kukosa usingizi kwa miaka kadhaa na kujipalia sonona?

Ni sawa kushindwa kula na kujichumia madonda ya tumbo? Ni sawa kujipuuza na kujiachaniza kisa tu umeruhusu kupokea maumivu kuliko unavyomudu?.

Uonavyo wewe, unajitendea haki?

Kuna pahala ili usogee ni lazima ukubali ukweli na uchambue ya kubeba na ya kuacha. Kuna mizigo ni hatarishi kwa safari ya ndoto zako.

Kuna watu kuwabeba kunahakikisha anguko lako. Kuna maumivu kuishi nayo na kuyakumbatia ni kama kuishi na adui anayekuua taratibu.

Kama unaweza japo kidogo, jifunze kuipenda nafsi yako kiasi cha kufika wakati wa kusema, "enough is enough"

Hakuna mwanzo wa furaha wenye tija bila kuruhusu mwisho wa huzuni ufike. Futa machozi. Vuta pumzi ndefuu, kisha achia...tuliza akili, fanya maamuzi sahihi.

Wewe ni wa thamani kama utaendelea kuwa mtu salama kwako na kwa wanaokuzunguka. Uchungu na maumivu vinakufanya uwe adui kwako mwenyewe, na kwa wale unaowathamini.

Tuwajibike, tukubali kuna mahali tuliacha mlango wazi na mwizi akaingia na kuiiba furaha yetu.

Hatua ya mapema na ya makusudi ya kurejesha upendo binafsi inahitajika kufanyika ili kuokoa jahazi.

Kuna makovu yatatakiwa kuishi kama ushahidi ili mwisho tukubali; HATUWEZI KUBADILISHA KILA KITU.
 
Utofauti ni kuwa, wewe unaumia sasa hivi, mwenzako aliumia jana, mwingine aliumia juzi, na mwingine aliumia miaka mingi iliyopita.

Umewahi kujiuliza, kama hayo maumivu utaishi nayo miaka kumi zaidi, yatakuumba kuwa kiumbe cha aina gani?

Kila mtu ana zamani yake ambayo, kama ingewezekana angeifuta kwa kifutio cha moto; isahaulike kama haikuwako mwanzo.

Zamani ni kama tu makovu; mengi ni ngumu kufutika. Na kadri tunavyojitahidi kuyafuta, pasi na utulivu tunaambulia kutengeneza majeraha mapya.

Hakuna namna utaumia zaidi ya vile umeruhusu.

Nakubali, maumivu huja mahali yasipotarajiwa kabla ndo maana huutafuna sana moyo.

Kuvunjwa moyo, hutokea kwa watu tuliowaamini kuliko namna tunaweza elezea, ndo maana kuna muda tunahisi kukata tamaa.

Lakini, ni sawa vile tunavyojitendea'ga' baada ya kupitia uzoefu huo mchungu?

Ni sawa kukosa usingizi kwa miaka kadhaa na kujipalia sonona?

Ni sawa kushindwa kula na kujichumia madonda ya tumbo? Ni sawa kujipuuza na kujiachaniza kisa tu umeruhusu kupokea maumivu kuliko unavyomudu?.

Uonavyo wewe, unajitendea haki?

Kuna pahala ili usogee ni lazima ukubali ukweli na uchambue ya kubeba na ya kuacha. Kuna mizigo ni hatarishi kwa safari ya ndoto zako.

Kuna watu kuwabeba kunahakikisha anguko lako. Kuna maumivu kuishi nayo na kuyakumbatia ni kama kuishi na adui anayekuua taratibu.

Kama unaweza japo kidogo, jifunze kuipenda nafsi yako kiasi cha kufika wakati wa kusema, "enough is enough"

Hakuna mwanzo wa furaha wenye tija bila kuruhusu mwisho wa huzuni ufike. Futa machozi. Vuta pumzi ndefuu, kisha achia...tuliza akili, fanya maamuzi sahihi.

Wewe ni wa thamani kama utaendelea kuwa mtu salama kwako na kwa wanaokuzunguka. Uchungu na maumivu vinakufanya uwe adui kwako mwenyewe, na kwa wale unaowathamini.

Tuwajibike, tukubali kuna mahali tuliacha mlango wazi na mwizi akaingia na kuiiba furaha yetu.

Hatua ya mapema na ya makusudi ya kurejesha upendo binafsi inahitajika kufanyika ili kuokoa jahazi.

Kuna makovu yatatakiwa kuishi kama ushahidi ili mwisho tukubali; HATUWEZI KUBADILISHA KILA KITU.
... appreciate it.
Kinachosababisha watu waumie Kwa lugha ya ujumla NI nini?
 
Ndy,inaweza kuwa kikwazo hasa pale unapokuwa na mqenza ambaye yeye hulka yake ni muongeaji mzuri,mchangamfu mzuri alafu wewe ukawa n mtu wa tofauti na yeye hapo lazma mtakuwa mnaingia kwenye lugha ya kukwarudhana
 
Utofauti ni kuwa, wewe unaumia sasa hivi, mwenzako aliumia jana, mwingine aliumia juzi, na mwingine aliumia miaka mingi iliyopita.

Umewahi kujiuliza, kama hayo maumivu utaishi nayo miaka kumi zaidi, yatakuumba kuwa kiumbe cha aina gani?

Kila mtu ana zamani yake ambayo, kama ingewezekana angeifuta kwa kifutio cha moto; isahaulike kama haikuwako mwanzo.

Zamani ni kama tu makovu; mengi ni ngumu kufutika. Na kadri tunavyojitahidi kuyafuta, pasi na utulivu tunaambulia kutengeneza majeraha mapya.

Hakuna namna utaumia zaidi ya vile umeruhusu.

Nakubali, maumivu huja mahali yasipotarajiwa kabla ndo maana huutafuna sana moyo.

Kuvunjwa moyo, hutokea kwa watu tuliowaamini kuliko namna tunaweza elezea, ndo maana kuna muda tunahisi kukata tamaa.

Lakini, ni sawa vile tunavyojitendea'ga' baada ya kupitia uzoefu huo mchungu?

Ni sawa kukosa usingizi kwa miaka kadhaa na kujipalia sonona?

Ni sawa kushindwa kula na kujichumia madonda ya tumbo? Ni sawa kujipuuza na kujiachaniza kisa tu umeruhusu kupokea maumivu kuliko unavyomudu?.

Uonavyo wewe, unajitendea haki?

Kuna pahala ili usogee ni lazima ukubali ukweli na uchambue ya kubeba na ya kuacha. Kuna mizigo ni hatarishi kwa safari ya ndoto zako.

Kuna watu kuwabeba kunahakikisha anguko lako. Kuna maumivu kuishi nayo na kuyakumbatia ni kama kuishi na adui anayekuua taratibu.

Kama unaweza japo kidogo, jifunze kuipenda nafsi yako kiasi cha kufika wakati wa kusema, "enough is enough"

Hakuna mwanzo wa furaha wenye tija bila kuruhusu mwisho wa huzuni ufike. Futa machozi. Vuta pumzi ndefuu, kisha achia...tuliza akili, fanya maamuzi sahihi.

Wewe ni wa thamani kama utaendelea kuwa mtu salama kwako na kwa wanaokuzunguka. Uchungu na maumivu vinakufanya uwe adui kwako mwenyewe, na kwa wale unaowathamini.

Tuwajibike, tukubali kuna mahali tuliacha mlango wazi na mwizi akaingia na kuiiba furaha yetu.

Hatua ya mapema na ya makusudi ya kurejesha upendo binafsi inahitajika kufanyika ili kuokoa jahazi.

Kuna makovu yatatakiwa kuishi kama ushahidi ili mwisho tukubali; HATUWEZI KUBADILISHA KILA KITU.
Barikiwa.
Mimi nilijifunza kitu kimoja na kimenisaidia kutokuumia Sana.
Nilijifunza kutokutarajia mengi Sana kutoka kwa watu.
Not expecting too much from human being,they can let you down any time.
 
And you have heard it.
Sobga mbele sasa
Ahsante mkuu...

some shitty things happened in my life, sasa nimejikuta najiingza kwenye destructive behavior lakini baada ya kusoma hili bandiko lako nimeona ninazidi kujiumiza mwenyewe, bora kuyapokea na kusonga mbele....

Napanga nisafiri kidogo kureboot...
 
Ahsante mkuu...

some shitty things happened in my life, sasa nimejikuta najiingza kwenye destructive behavior lakini baada ya kusoma hili bandiko lako nimeona ninazidi kujiumiza mwenyewe, bora kuyapokea na kusonga mbele....

Napanga nisafiri kidogo kureboot...
Asante sana wewe kwa sababu umepata kitu ambacho kimekusaidia na kitakusaidia,kwa sababu kupata kwako matumaini ya machaguo mazuri maishani mwako,ndivyo unavyonitia moyo katika uandishi wa vibandiko kama hivi asante sana na pia MUNGU akusaidie sana uwe bora zaid ya sku za nyuma ASANTE SANA MUNGU ALIYEKUUMBA ATAKUSAIDIA
 
Ahsante mkuu...

some shitty things happened in my life, sasa nimejikuta najiingza kwenye destructive behavior lakini baada ya kusoma hili bandiko lako nimeona ninazidi kujiumiza mwenyewe, bora kuyapokea na kusonga mbele....

Napanga nisafiri kidogo kureboot...
Asante sana wewe kwa sababu umepata kitu ambacho kimekusaidia na kitakusaidia,kwa sababu kupata kwako matumaini ya machaguo mazuri maishani mwako,ndivyo unavyonitia moyo katika uandishi wa vibandiko kama hivi asante sana na pia MUNGU akusaidie sana uwe bora zaid ya sku za nyuma ASANTE SANA MUNGU ALIYEKUUMBA ATAKUSAI
Nakuja kusoma vizuri, hongera Kwa Post yenye uponyaji ndani yake
Asante sana kaka mkubwa MUNGU akubariki kwa kunitia moyo
 
Barikiwa.
Mimi nilijifunza kitu kimoja na kimenisaidia kutokuumia Sana.
Nilijifunza kutokutarajia mengi Sana kutoka kwa watu.
Not expecting too much from human being,they can let you down any time.
For sure,
Matarajio huumiza sana yasipotimia
 
For sure,
Matarajio huumiza sana yasipotimia
Hataree na yote yatapita na maisha yataendelea.

"Kama huwezi kubadilisha fikra na mitazamo ya watu juu Yako, basi badili mtizamo wako juu Yao".

Huu msemo ninaishi nao Kila siku
 
Back
Top Bottom