BICHWA KOMWE -
JF-Expert Member
- Jul 21, 2022
- 6,373
- 16,073
- Thread starter
-
- #41
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Wale wanaokula senene mbona ni kwa asilimia kubwa maana nimeisha nao sana advance nawajua wawili wote walikuwa na tatizo hilo.
Ninapofanya kazi wapo wawili nao wote wana tatizo hilo jamani sijui kwa nn? Sina nia mbaya ndo maana sijataja mkoa moja kwa moja.
Halafu ni wabishi sana na kupenda kuongea .!
Asante sana.Kama umeoa au kuolewa piga mara 3 angalau.
Mi mzee babuKumbe unampata Kabwe Makanika Jitu kumbuka safi sana
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Sisi akina kabwe makanika. Tukijisahau tu kupiga mswaki asubuhi watu wanatukimbia
Hapana mkuuKaka nikuulize swali,
Umewahi kuzibwa meno hospitali au kuwekewa machuma au meno bandia?
Ndio wananuka mdomo humu jukwaani hawa?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Ndio wananuka mdomo humu jukwaani hawa?
Mwanzo nilikuwa sijijui ila kadri siku zilivyokuwa zinakwenda nikawa nashangaa kila nikiongea na mtu anageukia pembeni, wengine wananitenga, nikachunguza na kujiuliza ni kwanini mwishoe alitokea rafiki yangu akanieleza ukweli kwamba ninanuka sana mdomo ila aliogopa tu kuniambia.Utapona usijalii. Hilo ni tatizo dogo sana.
Wakati mwingine tatizo linaweza kuwa kwenye akili yako zaidi kuliko katika uhalisia.
Na mimi ninavyojua mtu hawezi kujijua kama ananuka mdomo isipokuwa mpaka AAMBIWE.
Lakini ndugu yangu, nini kimekufanya uamini unanuka mdomo??
Tafadhali, kindly share! Tunaweza kupata pa kuanzia.
Asante kwa ushauri wako na Mwenyezi Mungu akubariki sana nduguUkiwa unajishughulikia tatizo lako kwa daktari, usiache pia kusali.
Hii dunia ina mengi sana, kuna watu wanalogezewa kunuka midomo ndugu. Serious.
Lakini kwanza hebu fanya utaratibu wa hospitali wayaangalia hayo meno, pamoja na mfumo wa pua na tumboni huko pamoja na mafizi yote.
Fanya hayo yote huku unasali kwa juhudi, Mungu atakusaidia pia.
Ndio ila vijiwe zivioni kwa kweliKuna kutoa TONSIL STONES, na KUTOA TONSILS zenyewe.
Baadhi ya TONSILS zinapaswa kukatwaa kabisa na kuondolewa kwa sababu zinabeba mauchafu bila kukoma.
Unaweza ukatoa TONSIL STONE leo halafu kesho tena unakuta kengine kameota kananuka.
Una tabia ya kujikaguaa angalau kwa kioo kuchungulia kule ndani mdomoni uone kama kuna vijiwe jiwe vya njano????
Dawa ni kuvikata vile VIFUKO kwa operasheni maalumu. Sijui kama umewahi kufanya hilo!Pole sana sana,
Tonsils ni tatizo kubwa, kuna watu huwa wana VIFUKO VYA TONSILS ambavyo kila siku vinatengeneza uchafu hata utolewe.
Dawa ni kuvikata vile VIFUKO kwa operasheni maalumu. Sijui kama umewahi kufanya hilo!
Lakini piaa kuna upande wa pili wa shilingi, kuna KULOGWA na KUVAMIWA NA MAPEPO hii inahitaji maombi binafsi ya nguvu haswa!
Lakini utapona, kwa hakika!
Pole sana ndugu, lakini hilo ni tatizo dogo sana, na unalikuza zaidi katika akili yako linazidi kukuvuruga kumbe ni katatizo kadogo sana.Mwanzo nilikuwa sijijui ila kadri siku zilivyokuwa zinakwenda nikawa nashangaa kila nikiongea na mtu anageukia pembeni, wengine wananitenga, nikachunguza na kujiuliza ni kwanini mwishoe alitokea rafiki yangu akanieleza ukweli kwamba ninanuka sana mdomo ila aliogopa tu kuniambia.
Kuanzia hapo mambo yakaanza kuharibika... nikaanza kupoteza kujiamini, kukosa furaha na amani hatimae nikaenda hospitali kuonana na wataalam wa kinywa na meno( dentist) lakini haikusaidia chochote zaidi ya kupoteza pesa tu.
Kuna watu sijui midomo yao ina nini, hata asiposukutua mwezi mzima lakini mdomo wake haunuki hata chembe.
Akiamka asubuhi kinywa safi hadi raha, hakuna maharufu ya panya kuoza.
Yaani hata asipopiga mswaki ni ananukia mdomoni marashi matupu.
Kuna wale wenzangu na mimi wananuka midomo kama wamekula samadi au mbolea.
Hata wasukutue mara mia lakini midomo inatema cheche za moto.
Hii imekaaje?
MY TAKE: Tupige miswaki mara mbili kwa siku.
Huwa vinajificha kwa ndani, fanya kuingiza mswaki kwa upande wa mshikio, ubinye zile tonsils taratibu kwa mtindo wa kushuka uone kama hakuna kitu kinatoka.Ndio ila vijiwe zivioni kwa kweli
Sawa mkuuHuwa vinajificha kwa ndani, fanya kuingiza mswaki kwa upande wa mshikio, ubinye zile tonsils taratibu kwa mtindo wa kushuka uone kama hakuna kitu kinatoka.
Sio lazima kuvikata, maana huwa vinakatwa pale ambapo tu mawe yanaota kila mara.Dawa ni kuvikata vile VIFUKO kwa operasheni maalumu. Sijui kama umewahi kufanya hilo!
Kuhusu hilo niwe mkweli sijawahi mkuu zaidi ya kuondoa zile stones
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]Pole sana ndugu, lakini hilo ni tatizo dogo sana, na unalikuza zaidi katika akili yako linazidi kukuvuruga kumbe ni katatizo kadogo sana.
Nikushauri uanze tiba ya asili ya kubadilisha kabisa mfumo wako wa chakula pamoja na usafi wa meno.
1. Upe mwili wako nafasi ya kujitibu kwa kuachana na vyakula vinavyozalisha sulphur au vinavyosababisha harufu kuzidi maradufu kama vile nyama nyekundu, mayai, vitunguu nk. Na badala yake ule matunda na mbogamboga tupu angalau kwa miezi mitatu. (Na pia kama ulikuwa unameza madawa yoyote achana nayo).
2. Usinywe kabisa soda na vinywaji vyovyote vya kiwandani au vilevi na badala yake kunywa maji mengi sana angalau lita nne kwa siku na hata zaidi ya hapo.
3. Usitumie dawa za meno zenye flouride, na ikiwezekana tumia baking soda kwa kusukutulia angalau mara tatu kwa siku au zaidi ya hapo kwa kila baada ya mlo.
4. Sugua ulimi mpaka kwenye koromea kule ndani kabisa na kwenye kuta zote za tonsils, na pia sugua juu kwenye PAA la mdomo, pembezoni na mdomo na kuzunguka fizi zote.
5. Chukua uzi wa kushonea nguo ingiza katikati ya meno safisha meno yote mpaka kwenye magego, ingiza katikati kila mahali.
6. Koroga maji ya chumvi fanya kama unayabwia mdomoni na kuyasukutua kisha yateme na meza kidogo kila siku baada ya kusukutua.
7. MAJI, MATUNDA, MBOGA ZA MAJANII ongeza kwa wingi sana.
8. Sali na fanya maombi. Nguvu za giza zipo.
9. Kila siku asubuhi unapoamka chukua malimau mawili makubwa yabinye kwenye kikombe cha maji kunywa. Kila siku angalau kwa miezi miwili uone hali ikoje.
10. Mwisho, fanya zoezi la kisaikolojia kwa kupuuza maneno na fikra za watu. Jiamini na endelea kujitibu. Hakuna aliye mkamilifu.
Sawa nimekuelewa vizuri mkuuSio lazima kuvikata, maana huwa vinakatwa pale ambapo tu mawe yanaota kila mara.
Kama hauna tatizo la kutoka vile vimawe, basi haina haja.
Na wakati mwingine unaweza ukakuta hakuna vimawe lakini kuna MAAMBUKIZI kwenye VIFUKO VYA TONSILS.
Yale maambukizi yanasababishwa na fangas au bakteria, na yanafanya kuleta HARUFU MBAYA.
Fanya jaribio la kuingiza mswaki kwa upande wa mshikio, ingiza kwenye vifuko vya tonsils chokonoa taratibu halafu unuse uone kama kuna harufu ama la.