Kuna watu wanaleta utamaduni wa ovyo wa kutukana viongozi wa nchi. Ndugu zangu hiyo sio demokrasia

Orodhesha hayo matukano tuyachambue kama yanafaa au tumfokee mtukanaji.🤔
 
Mkuu nisaidie kwani Mtu akisema vibaya kuhusu utendaji wa kazi wake ni matusi au
Sijakuelewa ni Nini una Manisha.
Ila Ile kusema kiongozi anatukanwa Ili Hali viongozi Hawa wanatutukana wananchi Kwa kuuza maliasili zetu bila huruma rushwa za mabilioni ya shilingi. Huku mama zetu na dada zetu wakijifungulia chini hakuna huduma Wala vitanda.

Kila kona ni matusi mtupu tunatukanwa na viongozi Hawa wanao tetewa Leo.

Mwanza pale Kuna tusi la nguoni wananchi wameshatukanwa miaka mingi. Huwezi amini mwanza hapo pamoja na kuwa na maji karibu vile ila mwanza hawana maji safi na salama ya uhakika!!


Unataka viongozi aambiwe Kwa lugha Gani kama wananchi wanawaona ni umbwa?


Mgodi wa Bulyanhulu. Ile barabara ya kwenda kahama Hadi Leo Haina lami pamoja na kuwa hupisha maroli ya mchanga na ushuri kibao hulipwa.

Japo nasikia Kwa Sasa wameanza harakti za kuweka lami.
 
Na hii inakula kotekote...kiongozi aheshimu wananchi na wananchi waheshimu viongozi. Kifupi watu wote WAHESHIMIANE bila kujali ni kiongozi au ni mwananchi asie na cheo.
Tena kwa viongozi wasiwe na kauli za kukwaza kwaza watumie hekima.
 
Upo sahihi Ila Kama MTU unataka usitukanwe mitandaoni na sehemu mbalimbali unabidi ukae mbali na siasa.

..tatizo CCM wanaamiñi viongozi wa upinzani hawastahili heshima.

..Na wao ndio wako mstari wa mbele kudhalilisha na kutukana viongozi wa vyama vya upinzani.
 
Hii Nchi inahitaji uamsho. Kuna haja gani ya Mbunge au waziri kutembelea gari ya 500ml, wakati wananchi hawapati huduma muhimu kama maji safi?.
 
Sio kutukana viongozi tu hata kumtukana binadamu mwenzako ni tabia ya hovyo sana na inaonesha jinsi gani mtu hujastaarabika. Inapokuja kwa wanasaisa tena wengine ni wasomi wakubwa kutumia lugha ya matusi kwa kiongozi kisa tu mmepishana itikadi ni tabia ya hovyo na inawapotezea uungwaji mkono wa jamii ya wastaarabu wanabaki na jamii ya wachache ambao wao matusi ndio ustaarabu wao.
 
Unapozungungumzia viongozi wa nchi wapo pia mbowe .maaskofu .machifu.tatizo lako umejikita kutetea mama samia kwa kumdharau kuwa nimdhaifu wa kupenda sifa hivo umeandika maunafiki .ila ungetulia ulikuwa na point nzuri tu
 


Tatizo kila neno ni tusi Mnashidwa hoja na kutafuta visingizio. Mama habebeki
 
Mwambie Samia .haiwezi na haijawahi kutokea Giza na Nuru kukaa pamoja, yaani hawezi akawa anataka vyote Democrasia na udikteta kwa wakati mmoja. Aamue moja. Hata maji na mafuta haichangamani. Huwezi ukahubiri amani mchana, utekaji usiku
 
Kutukana ni nini na kukosoa ni nini?

Staha ni nini?

Marekani wanamtukana rais kwa matusi ya nguoni, kama sehemu ya uhuru wa kujieleza (first amendment) na rais hana haki ya kuwanyamazisha. Unaelewa nini kuhusu Marekani? Unaelewa nini kuhusu First Amendment ya katibabya Marekani?

Angalia Marekani watu wanauza fulana za "Fvck Joe Biden" "Fvck Trump" na "Fvck them Both" kama sehemu ya uhuru wa kujieleza.

Kuna T-Shirt inauzwa imeandikwa "Fvck Joe Biden. And Fvck You for Voting for Him". Kama sehemu ya uhuru wa kujieleza tu. Tanzania tunaweza hilo?

Tanzania unaweza kuuza T-Shirt ya "Fvck Samia Hassan" ?

 
Matusi wanayataka wenyewe.
Kuna wakati unaona kabisa hapa ni boga linaogea.
 
Daah mkuu huko marekani wanatukana sana viongozi yaani hata usifanye kuwa mfano.

Huko watu wamedata kabisa.

Ila ukitisha kumdhuru kuongozi hiyo inakua jambo jingine na hutachukua hata nusu saa watakukamata.
 
Huo ni uchawa mnaoleta, hebu tuonyeshe tusi moja alilotukanwa. Si lazima apongezwe hata anapokosea, jinsi alivyohandle issue ya watekaji na wauaji akiwa mfariji mkuu mnaona ni sawa?

Akiwa ni amiri jeshi mkuu lazima awajibike kwa usalama wa raia, kusema kifo cha kawaida na maneno yake ni sawa?
 
Ukitaka kujua watu Wana mateso kiasi gani nafsini mwao soma lugha wanayotumia kuzungumza au kuwasilisha mambo yao,ukiwa ni kiongozi mwenye Akili TIMAMU unajifunza kwa haraka sana lkn ukiwa kilaza ni ngumu kuelewa na unaweza kuja kuelewa mambo yakiwa yamesha haribika kwa sababu ya ugumu wa Akili ya kiongozi inayochelewa kuelewa mapema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…