Kuna wimbo nilitamani Ney auimbe. Huu hapa

Kuna wimbo nilitamani Ney auimbe. Huu hapa

Raia Fulani

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2009
Posts
11,478
Reaction score
3,659
Ukweli nilikaa mwaka jana mwishoni na katika kutafakari juu ya jambo husika nikasema niandike wimbo. Sina ujuzi wa uandishi wa nyimbo (rap au kuimba) ila mimi ni mwandishi mzuri tut wa mashairi na simulizi pia.

Baada ya kuuandika nikasema huu wimbo kwa jinsi ulivyo na ujumbe wake, msanii ambaye anaweza kufikisha ujumbe huu ni Ney (wa mitego).

Nikaanza harakati za kumtafuta. Ukweli ni kwamba sikujua wakati mwingine kumtafuta msanii kuna ukiritimba pengine hata zaidi ya kumtafuta mkuu wa mkoa. Of course kuna changamoto fulani za kimantiki zilikuwepo kwani awali nilionana na mtu wake wa karibu na akanipa maelekezo fulani.

Toka hapo ndio nikaanza mzunguko wa mawasiliano na kalenda za kutosha.

Sina hakika kama naye Ney aliona ujumbe wangu kwenye akaunti moja ya mtandao wa kijamii na kuupuuzia. Pengine ana haki hiyo kwa kuwa ana approach za kutosha za watu kama mimi.

Mwisho hata simu zangu zikawa hazipokelewi na wadau wake. Pengine ningesema nataka kwenda kurekodi wangenielewa.

Kwa kuwa nilisema nina wimbo ambao unamfit jamaa, na kwa kuwa sijulikani kwao siwezi wahukumu sana, ila jambo ambalo wangefanya ni kukutana nami.

Kwamba kwa nini sikwenda studio zao, ni kuwa walihama pale walipokuwa. Kadhalika sikutaka kukamia sana jambo hilo.

Muhimu nilitaka jamaa auone wimbo na kama ungemfaa auimbe. Maswala ya hela sikuzingatia. Pengine baade ndio tungeongea kama wimbo ungefanya vyema.

Hivyo basi kwa kuwa wimbo huo sijaona tena nani unamfit, nauweka hapa jukwaani tufurahie mashairi kwa pamoja. Wimbo unaitwa "Rainbow"

rainbow.jpg


WIMBO

RAINBOW​

Rainbow (Upinde)

Rainbow (Upinde)

Rainbow (Upinde)

Rainbow (Upinde)

Agano la Mungu (Upinde)



Ya walimwengu tuwaachie hao hao walimwengu
Ila ya Mungu tuyafanyie vikao wanangu
Watanijia tena na hawatafanikiwa, I know
Tena sijaanza leo kuwafokea, you know
Wakali hao! kwa nje kama quinine!
Weledi wa kupindisha ukweli hatari
Nina support ya umma wajue (Na ya Mungu unayo!!!)
Wanapenyeza ajenda tunapindua meza
Mwendo wa ambush, mwendo wa kuchakaza
Mwaka huu niko nao, tunaidai rainbow
Wamebadili asili, tunawacheki tu
Wamepora upinde, tunawacheki tu
Wanasambaza ajenda, tunawacheki tu
Wanatuona wajinga, tunawacheki tu
Ishara ya agano, mbingu na nchi
Leo rainbow inaogopwa, why?
Kwa sababu ya nyie? Haiwezekani

CHORUS
Wameupinda ukweli
Ukweli wa Mungu
Ukweli wa maandiko
Wameshapata fungu lao
Wanahamisha magoli

BRIDGE
Tusichukulie poa, dunia ilichafuka
Sio nyie wanadamu, ni kosa la malaika
Ngono, vita, mauaji, tamaa, ushirikina, ibada mbovu...
Wana wa Mungu wakaichakaza dunia kwa maovu
Dunia ikaharibika mbele za Mungu, tena ikajaa dhuluma
Someni maandiko, kilichofuata majanga
Mungu akasema sitatumia tena gharika
Na ishara ya agano angani mimi n'taweka
Ni bendera ya amani toka kwa Mungu mtukuka
Alisafisha waovu kunusuru kizazi chema
Enyi kizazi cha Azazel mlimkwepaje Mungu?
Mliipanda Safina ndani ya viuno vya Nuhu?
Au kwa kuwa ninyi mapepo? Anga, maji, ardhi mnapeta, sio?
Mkapeta mkafurahi mkaiteka Sodoma (na Gomora)
Mungu akapiga moto bado mkawepo masalia
Mnamjaribu Mungu aitwange tena dunia?

CHORUS
Muwanusuru wanadamu kwa ghadhabu za Mungu
Acheni kazi ya Mungu idhihirike, sio ya mzungu
Tunaukwepa upinde kuwahofia nyie wachache?
Mna agano na nini? wekeni hoja mezani
Agano kuhusu nini? Mmeivuruga imani
Neno litasimama na ahadi haitofutika
Upinde ni ishara iliyotukuka
Tukikaa kimya mtapora hadi maandiko

CHORUS
BRIDGE



Writer – Raia Fulani

©2023​
 
Wimbo mzuri usishangae wiki ijayo ukausikia kwenye redio zetu unadunda tena huyo huyo ndio atadai wimbo wake.
 
Halafu MODS niliweka huu ujumbe kule Hoja mchanganyiko iwe kama habari na si wimbo. Niliweka kama ujumbe mwingine tu
 
Mashairi yapo vizuri sana naamini Ney atafiti vizuri zaidi, najua kuna mambo anaweza kuyaongezea ngoma ikanoga zaidi
Ni kweli, kwa atakayeimba kwa namna yoyote kuna vitu/vionjo anaweza kuongeza
 
Huu wimbo unamfiti Afande, mpelekee kamavipi
 
Fanyeni namna wadau apatikane wa kuupaisha huu wimbo na ujumbe ufike parefu
 
Aiseeeeee,nilikuwa naisoma ajabu nikawa naimba naaksi Kama Nay!.

Sema watu wake ndo wanazingua jamaa hanaga maringo kabisa
 
Back
Top Bottom