Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Nchi yetu sasa imeingia rasmi katika ulimwengu wa uvuvuzela wa mpira. Kama vile ulivyo uraibu wa pombe, ngono, sigara n.k Idadi kubwa ya raia wa nchi kwa sasa wanalala wanazungumza mpira, wanaamka wanazungumza mpira na wanashinda wanazungumza mpira.
Bahati mbaya sana mpira wenyewe ambao haukauki midomoni ni mpira wa Liverpool, Arsenal, Man United n.k na sio mpira wa Namungo, Dodoma jiji, Ruvu Shooting na timu nyinginezo wenyeji kutoka miji wanayoishi raia wenyewe.
Wenye ajira nzuri, wamachinga, wasio na ajira, walalahoi, waliopigika, wanaoujua mpira, ambao hawaujui na wanaojifanya kuujua mpira wote content kubwa kila siku ni Liverpool, Chelsea, Simba na Yanga.
Hatuna mambo mengine tunayoweza kuyazungumza na kuyafanya makubwa na muhimu kama mpira?
Bahati mbaya sana mpira wenyewe ambao haukauki midomoni ni mpira wa Liverpool, Arsenal, Man United n.k na sio mpira wa Namungo, Dodoma jiji, Ruvu Shooting na timu nyinginezo wenyeji kutoka miji wanayoishi raia wenyewe.
Wenye ajira nzuri, wamachinga, wasio na ajira, walalahoi, waliopigika, wanaoujua mpira, ambao hawaujui na wanaojifanya kuujua mpira wote content kubwa kila siku ni Liverpool, Chelsea, Simba na Yanga.
Hatuna mambo mengine tunayoweza kuyazungumza na kuyafanya makubwa na muhimu kama mpira?