Kundi la wabunge CCM lasuka zengwe la EPA

Halisi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2007
Posts
2,802
Reaction score
614
Jamani hii habari imenishitua sana, nadhani huko CCM mambo si shwari na hili ni gazeti la serikali.

HabariLeo: Gwiji la habari Tanzania | Kundi la wabunge CCM lasuka zengwe la EPA

 
Wiki hii naona media Bongo wana mengi ya kuandika
 
Kichwa cha habari kinahusu wabunge na EPA. Content ya habari ni JK na mitambo mipya ya gesi ya TANESCO. Halisi mbona unakuwa kama wale wa magazeti ya udaku?
 
Kichwa cha habari kinahusu wabunge na EPA. Content ya habari ni JK na mitambo mipya ya gesi ya TANESCO. Halisi mbona unakuwa kama wale wa magazeti ya udaku?


Huyo ndo Mwana HALISI bwana.....kichwa cha habari kingine na habari tofauti. Gud enough hatununui ili tusome habari zake hapa.
 
“Msipoangalia wanaweza hata kuandamana kwa hili,” alisema.

Ain't this a b i t c h! I can not believe he could utter such statement.
 
Anaendelea na porojo...


Hivi walioliibia na kulihujumu Taifa kwa uzembe na ufisadi uliotuletea IPTL, Richmonds, Dowans na Kiwira umewachukulia hatua gani?

Je unataka tuandamane utuelewe?

Zaidi ni kwa nini Rais mzima anaishia kulalamika na si kutua amri kwa Ngeleja kazsi ifanyike? yaani anawasihi wizara na waziri wafanye kazi zao? damn it!

Samahanini furaha ya ushindi wa Obama inachafuliwa na kusoma upuuzi unaofanywa na Mwankupuli!
 

That is typical JK. Rais anasema kuna watu wamemtumia sms kuhusu kelele na moshi wa mitambo mipya ya gesi ya TANESCO. Huu ni mfano wa utendaji mbovu. Rais anakuwa na baraza la mawaziri ambao hata yeye mwenyewe hawaamini kama wanaweza kumsaidia. What was the point of appointing them in the first place? Kama watu hawakusaidii, wanini hawa? Rais atakuwa msemaji wa kila wizara mpaka lini? Issues kama OIC, Membe amekurupuka na kuja na upuuzi wake, wakristo walipochachamaa, ikabidi Rais aingilie kati na kutuliza mambo. Hili mpaka lini? Keshokutwa utasikia Maghembe ameshindwa kutatua migomo ya wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma, na itabidi Raisi aingilie. Matatizo ya walimu, wastaafu wa EAC, vifo vya maalbino. Huku kote lazima Rais aingilie. Mawaziri husika wanafanya nini? Kawachagua wanini? Kutumia kodi zetu kuzunguka mikoani? Au safari za nje kila siku?
 
Kichwa cha habari kinahusu wabunge na EPA. Content ya habari ni JK na mitambo mipya ya gesi ya TANESCO. Halisi mbona unakuwa kama wale wa magazeti ya udaku?

Nadhani hujanielewa, nimesema walioko nyumbani wanunue habari leo la jana Jumatano kwani katika mtandao kichwa ni "Re: Kundi la wabunge CCM lasuka zengwe la EPA" lakini habari ni "JK na IPTL" habari yenyewe imetungwa kwa lengo la kumuokoa Makamba ikiambatana na sms

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/20154-soma-hii-sms.html

ZOte zikiwa na lengo moja, kuwachonganisha wabunge wapinga ufisadi na JK na CCM halafu kumuokoa Makamba wakisahau kwamba mabadiliko ya Katiba haimtaji Spika

.....soma hapa....

HabariLeo: Gwiji la habari Tanzania | Kundi la wabunge CCM lasuka zengwe la EPA
 


Halisi

Hiyo habari ilikuwepo kwenye gazeti, labda wamekosea tu jinsi ya kuiweka kwenye website. Ni ile iliyoandaliwa na Salva Rweymamu kwa kushauriana na mmoja wa watuhumiwa wa ufisadi. Imeandika kwamba kuna kundi la wabunge wa CCM wanaotaka kuzusha hoja ya kutaka hata wale walirudisha fedha washtakiwa. Wameliita kundi hilo kuwa linatumiwa na wapinzani kwa lengo la kumuuabisha Rais Kikwete. Ni mkakati wa mafisadi wa kulenga kuwatia hofu wabunge wa CCM kuungana na wazalendo wenzao kwenye hii ajenda nyeti kwa usalama wa nchi

PM
 

Nashukuru ndugu yangu umeliona hilo maana hata huko Habari Leo kuna kigugumizi cha jinsi habari hiyo ilivyopenyezwa. Ama kweli JK ana kazi kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…