Kundi lipi ni tajiri zaidi duniani?

Kundi lipi ni tajiri zaidi duniani?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Inafahamika wazi ni mtu gani duniani anawazidi wengine kwa utajiri, umri, uzito, kukimbia, n.k lakini sijasikia ni watu gani duniani kwa ujumla wao wanawazidi watu wengine kwa ujumla wao pia kwa ukwasi wakiwekwa pamoja. Hivyo nani anafahamu ni kundi gani duniani linaloongoza kwa utajiri hapa duniani kati ya makundi yafuatayo kama uchumi wao ukiwekwa pamoja:

1. Wasanii
2. Wanamichezo
3. Wakulima
4. Wafanyabiashara
5. Wafugaji
6. Wafanyakazi (waajiliwa)
7. Watafiti
8. Wanasiasa

Na je, hawa ni waislamu au Wakristo?

Majibu ya swali hili yatabadilisha mipango na uelekeo wangu kwenye maisha
 
inafahamika wazi ni mtu gani duniani anawazidi wengine kwa utajiri, umri, uzito, kukimbia, n.k lakini sijasikia ni watu gani duniani kwa ujumla wao wanawazidi watu wengine kwa ujumla wao pia kwa ukwasi wakiwekwa pamoja. Hivyo nani anafahamu ni kundi gani duniani linaloongoza kwa utajiri hapa duniani kati ya makundi yafuatayo:

1. Wasanii
2. Wanamichezo
3. Wakulima
4. Wafanyabiashara
5. Wafugaji
6. Wafanyakazi (waajiliwa)
7. Watafiti
8. Wanasiasa

majibu ya swali hili yatabadilisha mipango na uelekeo wangu kwenye maisha
hilo kundi halipo hapo.
Kundi tajiri duniani ni wale wafanyabiashara haramu....(ambao ni vigumu kuwatambua pengine wamejificha kwenye sura ya hizo ulizozitaja)
pia majambazi na wezi wa kimataifa,mafia etc.
 
Nadhani wafanyabiashara.Wasaniı nao nadhani ni sehemu ya biashara.
 
Waisrael....matajiri wengi wakubwa Marekani na ktk level ya kidunia wana asili ya Israel
 
mbona ipo waz kabisa kuwa ni No 4...coz kila nyanja ulioitaja apo lazima mwishowe ukute uyo mtu anafanya biashara ili aweze kuwa na ukwasi huo..
 
kundi lingine ni la Wazalishaji bidhaa(Manufacturers) sio wachuuzi(traders)!matajiri wakubwa duniani ni wafanyabiashara wazalishaji tofauti wakati wafanyabiashara wengi kibongobongo ni wachuuzi--wananunua na kuuza!wanaozalisha ndio hao big names kina bakhresa,mengi ect
 
yapo makundi mengine yanayofuatia,hapo nimekutajia makundi matatu makubwa...hivyo ukitaka kuwa top most kuwa muisrael(kiuhalisia huwezi lakini literally unaweza yaani unaamua kuwa kama walivyo waisrael) au kuwa mfanyabiashara na hasa mfanyabiashara mzalishaji bidhaa!asante kila la heri
 
yapo makundi mengine yanayofuatia,hapo nimekutajia makundi matatu makubwa...hivyo ukitaka kuwa top most kuwa muisrael(kiuhalisia huwezi lakini literally unaweza yaani unaamua kuwa kama walivyo waisrael) au kuwa mfanyabiashara na hasa mfanyabiashara mzalishaji bidhaa!asante kila la heri

Eehe, ukitaka kuwa kama walivyo waisrael unafanyaje?
 
Eehe, ukitaka kuwa kama walivyo waisrael unafanyaje?
wanaamini wao ni wateule wa Mungu hivyo hakuna aina nyingine ya wanadamu wanaopaswa kuwa juu yao,wanaamini wana akili kuliko binadamu wengine,wanaamini hakuna swali lisilo na jibu hakuna tatizo lisilo na ufumbuzi mambo hayo kwa pamoja yanawafanya kufanya kazi kwa bidii na matokeo yake wanafanikiwa kuliko jamii yeyote popote walipo duniani
 
wanaamini wao ni wateule wa Mungu hivyo hakuna aina nyingine ya wanadamu wanaopaswa kuwa juu yao,wanaamini wana akili kuliko binadamu wengine,wanaamini hakuna swali lisilo na jibu hakuna tatizo lisilo na ufumbuzi mambo hayo kwa pamoja yanawafanya kufanya kazi kwa bidii na matokeo yake wanafanikiwa kuliko jamii yeyote popote walipo duniani

Hata waliyovyomuua ndugu yao Yesu ilikuwa sehemu ya mafanikio yao? Hata hivyo kwasababu ulizozitaja mimi siamimi na sintaamini kuwa wao ni wateule wa Mungu, ila ninaamini kuwa kuishi kwenye mazingira magumu na uhaba mkubwa ndo chimbuko la kufikiria kwa makini na kufanyakazi kwa bidii hadi kufanikisha na hatimaye inatengeneza culture (utamaduni) ya kufikiria na kufanyakazi kwa bidii, mazingira waliyoishi waisreil zama zao huko Misri na kwingineko yalikuwa maisha magumu sana kwao hivyo kufikiri sana na kufanyakazi kwa bidii ili waweze kusavaivu isingekuwa jambo la hiari kwao, hatimaye yaliwatengenezea culture ya kufanyakazi kwa bidii ili wajiokoe, hivyo hivyo kwa Wachina, Wacuba, Korea n.k. Hata Wachaga wametawanyika kila kona kutokana na maisha magumu kwao ya uhaba wa ardhi, chakula, makazi na baridi kule kwao, hivyo kusoma, kutafuta ajira, kufanya biashara na kuhamia mikoa minginine isingekuwa jambo la hiari kwao. Maisha mikoa ya Pwani, Morogoro, n.k ni rahisi sana kwakua ardhi ipo, mimea inakuwa bila kuhitaji mbolea, mifugo inakula bila kukatiwa majani, hakuna baridi, n.k hali hii inasababisha wasifirikirie sana juu ya maisha na hatima yao, hivyo hawakuhitaji kusoma wala kufanya biashara ili waweze kusavaivu, hatimaye maendeleo yao yamebaki nyuma. Lakini baada ya ardhi kuanza kupungua hata kwenye mikoa ya Pwani na Morogoro na kwingineko ndo wameanza kushtuka na migogoro ya ardhi inajitokeza, watoto wameanza kwenda shule na biashara wanafanya siku hizi ingawa si kwa kiwango cha wachaga na watu wengine kutoka mazingira magumu ya ardhi na baridi kali. Hata Afrika iko siku tutajifunza namna bora ya kufikiria maisha yetu kadiri upatikanaji wa mahitaji yetu unavyoendelea kuwa mgumu na maisha yetu kuendelea kuwa magumu na mabaya, iko siku kututawala haitakuwa kazi rahisi kama ilivyo sasa. Namuomba mungu maisha yetu yazidi kuwa magumu ili tujifunze namna ya kufikiria kwa busara na kufanyakazi kwa bidii na maarifa. Maana hata nyumbani kwako maisha yakiwa mazuri kupita kiasi watoto hawasomi wala kujifunza namna ya kufikiria, house girl anakuwa na maarifa mengi ya kujitegemea kuliko watoto wa boss. Maisha yakiwa magumu sana kwetu iko siku watawala watashindwa kuiba hata kura moja wakati wa uchaguzi na kupata ushindi kwa bao la mkono.
 
Hata waliyovyomuua ndugu yao Yesu ilikuwa sehemu ya mafanikio yao? Hata hivyo kwasababu ulizozitaja mimi siamimi na sintaamini kuwa wao ni wateule wa Mungu, ila ninaamini kuwa kuishi kwenye mazingira magumu na uhaba mkubwa ndo chimbuko la kufikiria kwa makini na kufanyakazi kwa bidii hadi kufanikisha na hatimaye inatengeneza culture (utamaduni) ya kufikiria na kufanyakazi kwa bidii, mazingira waliyoishi waisreil zama zao huko Misri na kwingineko yalikuwa maisha magumu sana kwao hivyo kufikiri sana na kufanyakazi kwa bidii ili waweze kusavaivu isingekuwa jambo la hiari kwao, hatimaye yaliwatengenezea culture ya kufanyakazi kwa bidii ili wajiokoe, hivyo hivyo kwa Wachina, Wacuba, Korea n.k. Hata Wachaga wametawanyika kila kona kutokana na maisha magumu kwao ya uhaba wa ardhi, chakula, makazi na baridi kule kwao, hivyo kusoma, kutafuta ajira, kufanya biashara na kuhamia mikoa minginine isingekuwa jambo la hiari kwao. Maisha mikoa ya Pwani, Morogoro, n.k ni rahisi sana kwakua ardhi ipo, mimea inakuwa bila kuhitaji mbolea, mifugo inakula bila kukatiwa majani, hakuna baridi, n.k hali hii inasababisha wasifirikirie sana juu ya maisha na hatima yao, hivyo hawakuhitaji kusoma wala kufanya biashara ili waweze kusavaivu, hatimaye maendeleo yao yamebaki nyuma. Lakini baada ya ardhi kuanza kupungua hata kwenye mikoa ya Pwani na Morogoro na kwingineko ndo wameanza kushtuka na migogoro ya ardhi inajitokeza, watoto wameanza kwenda shule na biashara wanafanya siku hizi ingawa si kwa kiwango cha wachaga na watu wengine kutoka mazingira magumu ya ardhi na baridi kali. Hata Afrika iko siku tutajifunza namna bora ya kufikiria maisha yetu kadiri upatikanaji wa mahitaji yetu unavyoendelea kuwa mgumu na maisha yetu kuendelea kuwa magumu na mabaya, iko siku kututawala haitakuwa kazi rahisi kama ilivyo sasa. Namuomba mungu maisha yetu yazidi kuwa magumu ili tujifunze namna ya kufikiria kwa busara na kufanyakazi kwa bidii na maarifa. Maana hata nyumbani kwako maisha yakiwa mazuri kupita kiasi watoto hawasomi wala kujifunza namna ya kufikiria, house girl anakuwa na maarifa mengi ya kujitegemea kuliko watoto wa boss.

umeandika vema kabisa mkuu,ila hapo juu mwanzo mimi sikusema wao ni wateule wa Mungu bali WANAAMINI wao ni wateule wa Mungu
 
Inafahamika wazi ni mtu gani duniani anawazidi wengine kwa utajiri, umri, uzito, kukimbia, n.k lakini sijasikia ni watu gani duniani kwa ujumla wao wanawazidi watu wengine kwa ujumla wao pia kwa ukwasi wakiwekwa pamoja. Hivyo nani anafahamu ni kundi gani duniani linaloongoza kwa utajiri hapa duniani kati ya makundi yafuatayo kama uchumi wao ukiwekwa pamoja:

1. Wasanii
2. Wanamichezo
3. Wakulima
4. Wafanyabiashara
5. Wafugaji
6. Wafanyakazi (waajiliwa)
7. Watafiti
8. Wanasiasa

Na je, hawa ni waislamu au Wakristo?

Majibu ya swali hili yatabadilisha mipango na uelekeo wangu kwenye maisha

Hapa utaambiwa mengi lakini ukweli wa wazi kundi tajili duniani na kila nchi tajili inapiga saluti kwao ni kundi la kidini la KIKATOLIKI lenye makao yake makuu VATICAN CITY.fatilia kwa undani utajua
 
Hapa utaambiwa mengi lakini ukweli wa wazi kundi tajili duniani na kila nchi tajili inapiga saluti kwao ni kundi la kidini la KIKATOLIKI lenye makao yake makuu VATICAN CITY.fatilia kwa undani utajua

Silipingi hilo pia maana hawa jamaa wana utawala imara na mtandao unaopokea sadaka na zaka za waumini, na vitega uchumi dunia nzima kwa kisingizio cha Mungu baba, Mwana na Roho.
 
Back
Top Bottom