Kunyonya denda huwezi kupata UKIMWI, iweje uweze kupimwa UKIMWI kwa mate?

Kaka Pekee

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2018
Posts
336
Reaction score
564
Habari Wadau!,
Jana Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Inmi K. Patterson na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa na Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu katika kampeni ya maadhimisho ya miaka 15 ya ubia kati ya Marekani na Tanzania katika kupambana na janga la VVU/UKIMWI chini ya Mpango wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR) Walionyesha kifaa cha kujipima VVU/UKIMWI mwenyewe nyumbani kwa kutumia Mate...kifaa cha OraQuick ( Alichokishika Waziri Ummy Pichani) ambacho kitazinduliwa na Waziri Mkuu Majaliwa Dodoma hivi karibuni.


Swahi ni je?...Wataalamu hutuambia kuwa huwezi kupata maambukizi ya Virusi vya Ukimwi kupitia busu at Wet Kiss (Denda) labda kwa asilimia ndogo iwapo mna michubuko/Vidonda mdomoni, Sasa hii ya kupima Maambukizi kupitia mdomo (Mate) iweje uweze kugundulika na Virusi kwa njia hii hususani kama hatuna Michubuko, au ni mimi sijaelewa?
 
Mambo ya kitaalamu yanatuchanganya sana, ama kipindi cha nyuma walikuwa na lengo la kuwa tuambukizane kirahisi maana haohao ndo walisema hivyo kuwa kupiga denda siyo rahisi kupata maambukizi, leo hii wanasema tupime ukimwi kwa kupitia mate. Tusubiri wataalamu watuletee siasa zingine.
 
Itakua virusi vina athiri tezi na mate na kutengeneza kemikali fulani inayochanganyika na mate.

Sasa kemikali hiyo ikipimwa ndio inadhihirisha una maambukizi ya VVU.

Kwa Biolojia yangu ya A-level nimewaza hvyo.
 
I am not an expert.
Lakini najua kwenye kupima kuna vitu viwili vinavyotafutwa......either virus yenyewe ya HIV au antibodies zinazozalishwa na mwili kupambana na virus endapo ipo kwenye damu yako.
I think hiki kipimo kitakuwa kina detect antibodies?
NOTE: I AM NO DOCTOR AND HAVE ZERO EXPERIENCE NA HAYA MAMBO haha
 
Itakua virusi vina athiri tezi na mate na kutengeneza kemikali fulani inayochanganyika na mate.

Sasa kemikali hiyo ikipimwa ndio inadhihirisha una maambukizi ya VVU.

Kwa Biolojia yangu ya A-level nimewaza hvyo.
Wanasayansi wanatuchanganya na sayansi yao kwa kweli!
 
kwa Hizi sayansi aisee Naanza kupata mashaka na mashemeji zako wote waliokuwa wakinipa kiss.
 
Kupima ni jambo moja, kuangalia hayo majibu ndio mtihani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…