Kunyoosha mguu wa mtoto mchanga wa wiki

fukutoz

Member
Joined
May 3, 2018
Posts
10
Reaction score
13
Wakuu habari,

Naomba msaada,

Kuna dada yangu amejifungua wiki iliyopita
lakini mtoto mguu wake umepinda ya kwamba pindi akianza kutembea atakuwa anakanyagia kwenye kifundo kwa pembeni.

Naomba msaada wa kunijulisha dokta au hospitali gani itafaa kwa kutatua tatizo hili.
 
Poleni mkuu, ngoja wataalamu waje kutoa maelekezo
 
Wakunga wamemvunja mguu, hata wa kwangu walimfanya hivyo mguu wakushoto, mpeleke Mujimbili pale maternity kama kweli ana wiki moja, watampokea watanyoosha kaguu hako hadi katakuwa sawa,
 
Achana na habari ya CCBRT watakulia hela tu, nenda Muhimbili jengo la wazazi
 
Chalii yangu now ana mwaka na nusu na atachezea Liverpool FC miaka ijayo
 
Ndio maana Hospitali zikawepo, Matatizo mengine kabla hujauliza hapa anza kuwaza kwenda hospitali kwanza.

Humu uliza tu dawa za nguvu za kiume utaambiwa ila tatizo hilo linatakiwa utatuzi wa haraka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…