Kuolewa SIO bahati...USIBAHATISHE!


MP ukiangalia tu hapa jamvini wapo wanaune wanaodai kwamba hawawezi ingia kwenye ndoa na wanawake wenye pesa au elimu zaidi yao. Kwahiyo pamoja na kwamba wapo wanawake wanaoona elimu na pesa ni kila kitu wapo wanaoona kinyume na hapo. Tatizo sasa ni kumpata mwanaume asiye na elimu/kipato sawa na dada aliyesoma na bado akawa tayari kuishi nae kama mke na mume.

Hata hivyo pole kwa yaliyokusibu. . . wa kukufaa utampata tu.
 
OK ngoja niidanike hapa
MTU MPUMBAVU HATA UKIMTWANGA KWENYE KINU PAMOJA NA NGANO UPUMBAVU WAKE HAUMTOKI
umeiona?
Nimeona. Japo sijaelewa kwanini uhusishe na kutwangana badala ya kumuelimisha na kureplace huo upumbavu wake na elimu. Nwy nna yangu inaenda hivi "Ujinga haina bei, yeyote anaweza aka'afford."
 
Nimeona. Japo sijaelewa kwanini uhusishe na kutwangana badala ya kumuelimisha na kureplace huo upumbavu wake na elimu. Nwy nna yangu inaenda hivi "Ujinga haina bei, yeyote anaweza aka'afford."
Mpumbavu ni mtu anayejifanya anajua kumbe hajui. Na nikimbelembele na hataki kuelimishwa hata kwa kutumia nguvu ya namna gani.
Ndio maana yake kwa ufupi sana.
Kheri ukawa mjinga kuliko Mpumbavu
Mjinga hufundishika. FUNGUKA
 
Mpumbavu ni mtu anayejifanya anajua kumbe hajui. Na nikimbelembele na hataki kuelimishwa hata kwa kutumia nguvu ya namna gani.
Ndio maana yake kwa ufupi sana.
Kheri ukawa mjinga kuliko Mpumbavu
Mjinga hufundishika. FUNGUKA
Owwkey. .

Nifunguke wapi tena?
 
Owwkey. .

Nifunguke wapi tena?
Kuolewa ni bahati bali kuoa ni mipango yako tu. Ila sasa kazi ipo who is right. Mpaka ukae nae mda kidogo.
Kwetu wanaume tunamahitaji machache sana kwa mwanamke
1. Kitanda kiwe kizuri
2.Utii
 
Hapa wenye ndoa zetu tunaruhusiwa kuchangia mada?

Kama tunaruhusiwa basi napenda kuwafahamisheni kuwa uzoefu na kaumri nlikonako nimeshayaona mengi ambayo nimeamua mwenyewe kukonkludi kuwa:

KUOLEWA NI BAHATI NA KUOA NI UAMUZI.
 
Kuolewa ni bahati bali kuoa ni mipango yako tu. Ila sasa kazi ipo who is right. Mpaka ukae nae mda kidogo.
Kwetu wanaume tunamahitaji machache sana kwa mwanamke
1. Kitanda kiwe kizuri
2.Utii
Owwkey.

Nshakua mtiifu kwahiyo kila kitu naitikia rabeka bwana.
 
Hapa wenye ndoa zetu tunaruhusiwa kuchangia mada?

Kama tunaruhusiwa basi napenda kuwafahamisheni kuwa uzoefu na kaumri nlikonako nimeshayaona mengi ambayo nimeamua mwenyewe kukonkludi kuwa:

KUOLEWA NI BAHATI NA KUOA NI UAMUZI.

Haya bana. . . I guess siku nikiamua kuolewa hutotaka kadi ya mwaliko.
 
Jaribu kuwa muelewa, nilichosema ni kwamba kitendo cha kuolewa tu pekee(na mtu yeyote yule) sio bahati, bahati ipo kwenye kumpata mtu ambae anaelewa maana ya mahusiano yake (mwenye heshima, kujali, mwaminifu n.k).
Swali, kama kuolewa si bahati utaishi/ataishi kwenye ndoa? ndoa zote ni bahati nasibu ama upate...au upatikane. Ukipata bahati unabaki kwenye ndoa, ukikosa unapigwa talaka.
 
...madhali mwanaume ndiye anayetamka "nakuoa!..."
kuolewa itaendelea kuwa bahati.
 
Haya bana. . . I guess siku nikiamua kuolewa hutotaka kadi ya mwaliko.
Unaweza kuamua kuolewa, kama ndoa unayoizungumzia ni ile ya jinsia moja. Lakini kama ni ya kuolewa na mwanamme nahofu hutakuwa na kuamua kuolewa ila utabahatika.

BILA YA KUJALISHA CHOCHOTE kadi ya mwaliko ni haki yangu na naihitaji sana.
 
Kuolewa si bahati lakini kuolewa na klorokwini ni bonge la bahati
Haya kinadada nichangamkieni kabla sijachenji maindi
 
Kwanza siamini katika kitu kinachoitwa bahati kwani haipo!Pia kwenye kuoana,kwanza sio lazima kuingia kwenye ndoa(mtazamo wa kikristo),hivyo unaweza kuacha pia!
 
Kusema kwamba ndoa sio ‘bahati’ inaashiria kwamba kutoolewa ni nuksi, kwani kila jambo lazima kulitazama je, kinyume chake ni nini? Ebu tuone ndoa maana yake ni nini ili tubaini iwapo kama utaikosa basi kuna nuski. Maana rahisi ya ndoa ni muungano ya watu wawili (kwa kawaida mwanaume na mwanamke), au mkataba wa kisheria baina ya watu hawa wawili, inayopelekea kuzinduliwa rasmi kwa familia mpya. Katika jamii, ndoa ni moja ya taasisi muhimu ambapo mahusiano ya baina ya mwanaume na mwanamke yanahalalishwa na kutambulika kisheria na vilevile kidini. Muungano huu uhalalishwa na sherehe, yani harusi. Kuna sababu kadhaa zinazopelekea ndoa kutokea, sababu kubwa ni pamoja na – kuhalalisha uhusiano wa kimapenzi baina ya mwanaume na mwanamke kisheria na kidini, kutekeleza utamadani katika jamii husika kwamba binadamu akifikia umri fulani lazima aoe/aoelewe, vinginevyo hatokuwa anaendana na utamaduni husika, sababu nyingine pia ni kukidhi matamanio ya kukutana kimwili, haswa kwa wale wanaosubiri ndoa kabla ya kufanikisha hilo, ndoa pia hutokana na hisia za watu wawili kutaka kuishi pamoja (mapenzi au mazoea) ili kujenga familia mpya, lakini pia ndoa hutokana na sababu za kiuchumi ambapo katika jamii fulani fulani, ndoa huleta unafuu kiuchumi kulingana na sheria kama vile za kodi n.k, lakini pia wapo wanaooa au olewa kwa kufuata mali. Sasa, kuwa na mtazamo kwamba ndoa ni bahati au sio bahati ni kutokana na malengo yako nini haswa katika kufikia hatua ya kuwa ndani ya ndoa.
 

 
Last edited by a moderator:

kwako wewe waweza kufikiri utakavyo lakini Muumba aliweka angalizo ya kuwa mwanamke ataolewa na mwanaumme yeyote yule awe na hizo sifa au la.............kwa hiyo akimbahatisha mwenye sifa tajwa hiyo ni bahati kwake lakini kwa mwanaumme Mwenyezi Mungu ameshurutisha lazima aoe mwanamke ambaye atakuwa amemfanyia utaifiti wa kutosha asioe tu bora liende..........Soma Biblia kitabu cha SIRACHI 36: 18-25..........

"Choosing a wife.

Any kind of food can be eaten, but some foods are better than others. And just as a tongue can distinguish the flavours of different kinds of meat, so is a sharp mind can detect lies. A person with a warped mind causes trouble, but an experienced person knows how to pay it back.

A woman has to take any man as a husband, but a man must choose his wife carefully.
A woman's beauty makes a man happy; there is no fairer sight for the human eye to see. If the woman is kind and gentle in her speech her husband is the most fortunate of men. When a man marries, he gets the finest thing he will ever have-a wife to help and encourage him.

If property is not fenced in, thieves will wander in and help themselves. And if a man has no wife, he is a sighting wanderer, people have no more trust in a homeless person who sleeps in a different place every night than they have in a wandering thief who goes from town to town."
 
katika jamii yoyote ile wanawake ni wengi kulikoni wanaumme..........na sheria ya ndoa hususani kwa siye wakristu ya "one man, one wife" au ndoa ya mke mmoja......pia inachangia kuhakikisha idadi kubwa ya wanawake kutoolewa maishani mwao............na kuishia kuwa mistresses khali ambayo hubidi kuivumilia kulingana na mazingira halisi...........................kwa hiyo katika mazingira ya namna hii kuolewa lazima kuwe bakhati hata kama kaolewa na "kapurwa".....................................mengineyo yatafuata baadaye......................ya kama kaolewa na anayemfaa au la................................hiyo ndiyo khali halisi...............too may gals but few bachelors to tie the knot with them..............

wako wanawake wengi ambao baada ya kukata tamaa ya kuolewa basi huamua kuzaa na mwanaumme yeyote yule ajae mlangoni kwao na ukiwahoji utasikia wakijibu kwa huzuni ya kuwa..........................nilitaka bwana wa kuzaa naye tu sina shughuli naye baada ya hapo..............mambo siyo mepesi hata chembe..........
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…