Kuolewa SIO bahati...USIBAHATISHE!

Ni kweli kabisa jamii kwa sehemu kubwa wanaamini kuolewa ni bahati,haijarishi unaeolewa nae, binafsi huwa nashangaa maana siamini kama kuolewa ni bahati, kwa imani hizo ndo maana wanawake wengi wananyanyasika kwenye ndoa zao.
 
Ukitaka kujua kama ni bahata au la jaribu kuongea na wadada wenye umri zaidi ya 35 utasikia malalamiko yao, kuna dada jirani amejaribu mpaka kuokoka ili apate mme lakini la kwa sasa mwenyewe anasema hana bahati.
 
lizzy upo juu na mra nyingi napenda mada na michango yako,hongera dada
 
...madhali mwanaume ndiye anayetamka "nakuoa!..."
kuolewa itaendelea kuwa bahati.
Mbu watu wanapokula kiapo cha ndoa kila mmoja anaulizwa kama "anakubali kumchukua mwenzake" na hamna anaeulizwa kama "anakubali kuchukuliwa na mwenzake". . .
 
Ukitaka kujua kama ni bahata au la jaribu kuongea na wadada wenye umri zaidi ya 35 utasikia malalamiko yao, kuna dada jirani amejaribu mpaka kuokoka ili apate mme lakini la kwa sasa mwenyewe anasema hana bahati.
Uongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…