Titicomb
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 12,823
- 21,210
Habari za weekend wadau wa JF.
Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu kama nilivyo wasilisha kwa mtindo wa swali hapo juu ktk kichwa cha habari.
Kwa jinsi sakata lilivyo zimwa kwa miaka 10 na kuja kuibuka sasa kiasi cha kusababisha kushuka thamani ya hisa za klabu ya Juventus soko la hisa imenipelekea kuwaza kitu cha ajabu.
Kwamba huenda timu ya wale wasiojilikana waliofanikisha kuzimwa kwa tuhuma hizo wanaotambulika kama 'fixers' huenda nyuma ya pazia walifadhiluwa na Real Madrid.
Huenda hawakutambulishwa kama watu waliofanya kazi chini ya maagizo na malipo ya Madrid kwa kukwepa kuiingiza klabu ktk kashifa kubwa hivyo ikatumika mbinu ya kuonekana mchakato mzima uliendeshwa na wanasheria wake binafsi CR7 toka Ureno.
Kilicho pelekea kuwaza hivyo ni hisia tu kwamba Madrid hawakuoendezwa na namna alivyoondoka Ronaldo(CR7) wakaona huyu dogo anajiona mkubwa kuliko klabu yetu basi ngoja tukamstue yule dada binti Mayorga aliamshe dude ili kumchafua Ronaldo na kumfanya wadhamini wake wamtose na klabu ya Juventus waingie hasara kubwa.
Tujiulize kama kweli hii hisia yangu Je, Juve wanaweza kuandaa 'fixer' wao wazime tena sakata hili kuinusuru klabu yao isikumbwe na hasara kubwa ukuzingatia mzigo mkubwa ambao walitumia kumnunua Ronaldo?
Nahisi mambo yakienda vibaya kwa Ronaldo Juve itaingia hasara kubwa sana na kuyumba kwenye mambo ya kifedha na hasa fedha za usajili.
Kama hilo litatokea linaweza kusababisha Juve kukumbana na matatizo ya Uefa financial fair play misimu ijayo.
Wapenzi wa soka bila kujali klabu tunazo shabikia au tunaopenda ushindani wa Messi na jamaa tuombe isiwe hivyo na jambo hili liishe salama na vizuri kwa upande wa CR7.
Alamsiki.
Niende moja kwa moja kwenye hoja yangu kama nilivyo wasilisha kwa mtindo wa swali hapo juu ktk kichwa cha habari.
Kwa jinsi sakata lilivyo zimwa kwa miaka 10 na kuja kuibuka sasa kiasi cha kusababisha kushuka thamani ya hisa za klabu ya Juventus soko la hisa imenipelekea kuwaza kitu cha ajabu.
Kwamba huenda timu ya wale wasiojilikana waliofanikisha kuzimwa kwa tuhuma hizo wanaotambulika kama 'fixers' huenda nyuma ya pazia walifadhiluwa na Real Madrid.
Huenda hawakutambulishwa kama watu waliofanya kazi chini ya maagizo na malipo ya Madrid kwa kukwepa kuiingiza klabu ktk kashifa kubwa hivyo ikatumika mbinu ya kuonekana mchakato mzima uliendeshwa na wanasheria wake binafsi CR7 toka Ureno.
Kilicho pelekea kuwaza hivyo ni hisia tu kwamba Madrid hawakuoendezwa na namna alivyoondoka Ronaldo(CR7) wakaona huyu dogo anajiona mkubwa kuliko klabu yetu basi ngoja tukamstue yule dada binti Mayorga aliamshe dude ili kumchafua Ronaldo na kumfanya wadhamini wake wamtose na klabu ya Juventus waingie hasara kubwa.
Tujiulize kama kweli hii hisia yangu Je, Juve wanaweza kuandaa 'fixer' wao wazime tena sakata hili kuinusuru klabu yao isikumbwe na hasara kubwa ukuzingatia mzigo mkubwa ambao walitumia kumnunua Ronaldo?
Nahisi mambo yakienda vibaya kwa Ronaldo Juve itaingia hasara kubwa sana na kuyumba kwenye mambo ya kifedha na hasa fedha za usajili.
Kama hilo litatokea linaweza kusababisha Juve kukumbana na matatizo ya Uefa financial fair play misimu ijayo.
Wapenzi wa soka bila kujali klabu tunazo shabikia au tunaopenda ushindani wa Messi na jamaa tuombe isiwe hivyo na jambo hili liishe salama na vizuri kwa upande wa CR7.
Alamsiki.