Kuongezwa mshahara siyo njia sahihi ya kutatua ugumu wa maisha

Kuongezwa mshahara siyo njia sahihi ya kutatua ugumu wa maisha

bhikola

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
1,131
Reaction score
1,663
Habari wana Jamii,

Ninamshukuru sana Mungu kwa kunijaalia kuiona tena siku mpya.

Watu wengi wanapopatwa na matatizo ya kifedha, jambo la kwanza hufikiria ni kwasababu wanapata mishahara midogo. Ukiwauliza wafanyakazi walio wengi kuhusu njia bora ya kuboresha maisha yao, watakwambia ni kuongezewa mishahara, na hata wasio waajiriwa - hasa vijana wanaotoka mashuleni na vyuoni, ndoto yao kubwa juu ya kuwa na uhuru wa kipato hivyo kuwa na maisha mazuri watakwambia ni kupata kazi nzuri yenye mshahara mkubwa.

Changamoto ya jambo hilo ni nini?
1. Kuongeza mishahara kunaongeza gharama katika uzalishaji, kumbuka mshahara ni fixed cost, kwa hiyo ili kuongeza mishahara kuwe na tija ni lazima uzalishaji uongezeka. kwa mfano ukisema mishahara iongezeke kwa asilimia 10, kama ulikuwa unapata 1m utakuwa unapata 1.1m. lakini kutokana na kupanga kwa gharama za bidhaa zalishwa au hudumu, tunategemea pia kutakuwa na ongezeko la bei katika huduma ama bidhaa tajwa. Hivyo utajikuta uwezo wa mshahara wako kununua unapungua kuliko uliokuwa nao mwanzoni. maana umepata ongezeko la laki 1 lakini karibu kila huduma na bidhaa imepanda hivyo nyongeza ya ongezeko lake kwa mwezi ni zaidi ya 1k.

2. Mshahara ni moja ya njia duni kabisa za kupata kipato endelevu - sustainable earning, kwasababu mshahara unaupata ukiwa tayari umeshautumia ama kuupangia matumizi, lakini pia ukikoma kupata mshahara unakuwa duni zaidi. Angalia wastaafu tulio nao utaelewa naongea nini.

3. Kuongezwa mshahara kunaendana na kuongezeka kwa makato mbalimbali hasa yale yanayoendana na asillimia kama kodi, bima na mengine. So kuongezwa mshahara ni kuongezewa kiasi cha makato.

Tufanyeje sasa?

1. Tafuta njia ambayo itatatua matatizo yako ya kifedha - spend less on liabilities and more on assets

2. Punguza wategemezi, tunakulipa mshahara kwaajiri yako na mkeo au mmeo, na watoto 4 tu basi. sasa wewe unataka uwalipe mshahara mashangazi, wajomba, wajukuu, na ukoo mzima kijijini kwenu, it wont work.

3. Ongeza kipato kwa kufanya uzalishaji wa vitu vidogovidogo vya kutumia nyumbani. kwa mfano badala ya kuhangaika na mayai, fuga kuku hata 5 tu utatatua tatizo la mayai kwako. Badala ya kuhangaika na mboga, lima matuta 2 tu nyumbani kwako utapata mboga mboga angalau kwa uchache.

4. Budget fedha zako vizuri, na ufuate bajeti yako. tatizo watz wengi hatuna budget

Kwa leo ni hayo tu.

J3 njema, na Mungu awabariki..
 
Ningependa kujifunza zaidi kwenye hiki kipengele
tufanyeje sasa?
1. Tafuta njia ambayo itatatua matatizo yako ya kifedha - spend less on liabilities and more on assets
Tunaomba mfano/ mifano, kwa manufaa ya wengi

Shukrani
 
Ningependa kujifunza zaidi kwenye hiki kipengele

Tunaomba mfano/ mifano, kwa manufaa ya wengi

Shukrani

Kwanza nimpongeze mtoa Mada sababu ameeleza mambo ya msingi sana kwa Maisha ya sisi tunaonishi kwa Mishahara. Mimi nililiona hili na nmeishaanza lifanyia kazi kwa kiasi nimepata uhuru wa kifedha kwa matatizo madogomadogo..

Sasa nikirudi kwenye mada...nielewapo mimi anaposema "spend less on liabilities and more on assets" anamaanisha punguza vitu ambavyo vinakucost(take money out of your pocket=liability) na kiasi hicho wekeza katika vitu ambavyo vinakuingizia kipato(put money in your pocket=asset)..ukiweza kufanya hivyo ndo unaelekea kuwa financial free....

Note:Ni ngumu sana kuwa tajiri kwa kusubilia mshahara lazima kubuld business(assets)

Ni hayo tuu kwa kifupi.
 
Ningependa kujifunza zaidi kwenye hiki kipengele

Tunaomba mfano/ mifano, kwa manufaa ya wengi

Shukrani

Mwl. RCT shukran sana kwa kufuatilia mada hii,
na unachohitaji kujifunza ni kweli kabisa kuwa ni tattizo kwa watu wengi, na shida kubwa ni vile hatujui asset ni nini na liability ni nini, lakini jamaa yangu jonas2011 amejibu vyema kabisa. sasa jambo la msingi ni nini? jambo la msingi ni kutambua liabilities zako na kuanza kuziepuka
ili kuzitambua fanya jambo moja, andaa petty cash yako ambako utakuwa unarekodi transaction zako zote za siku. ukifanya hivyo kwa mwezi mzima utashangaa mwenyewe kinachokumalizia fedha zako ni kitu gani.
ukishakifahamu hicho ki liability chako, step ya pili ni kukikimbia (to avoid your cash predator or your liability) hapo utakuwa umefanikiwa kwa kiasi fulani maana utaanza kujenga uwezo wa kifedha, hata fursa za asset zikijitokeza utakuwa na uwezo wa kuzipata maana uko liquid
mengineyo fuatilia post ya Jonas2011
 
Kwanza nimpongeze mtoa Mada sababu ameeleza mambo ya msingi sana kwa Maisha ya sisi tunaonishi kwa Mishahara. Mimi nililiona hili na nmeishaanza lifanyia kazi kwa kiasi nimepata uhuru wa kifedha kwa matatizo madogomadogo..

Sasa nikirudi kwenye mada...nielewapo mimi anaposema "spend less on liabilities and more on assets" anamaanisha punguza vitu ambavyo vinakucost(take money out of your pocket=liability) na kiasi hicho wekeza katika vitu ambavyo vinakuingizia kipato(put money in your pocket=asset)..ukiweza kufanya hivyo ndo unaelekea kuwa financial free....

Note:Ni ngumu sana kuwa tajiri kwa kusubilia mshahara lazima kubuld business(assets)

Ni hayo tuu kwa kifupi.

umenikumbusha rich dady..poor dady!! ukiishi kwenye hii misingi unatoboa faster!
 
Back
Top Bottom