Kalamu Nzito
JF-Expert Member
- Aug 13, 2015
- 349
- 805
Mahakama imekua na utaratibu wa kuandaa Guidelines (Miongozo) kwenye taratibu mbalimbali za kisheria.
Mathalani mpaka sasa kuna guidelines kama;
1. Bail Guidelines (2020)
2. Execution Guidelines (2020)
3. The Tanzania Sentencing Guidelines (2023)
4. Exhibit Management Guidelines(2020)
Hii ni baadhi tu ya miongozo. Kwamba, japo taratibu zipo ndani ya sheria husika, Mahakama iliona ni vyema kudadavua taratibu hizo ili kuepusha mkanganyiko.
Nashauri sasa Mahakama ituletee ARREST GUIDELINES (Miongozi ya ukamataji) Taratibu za ukamataji wa washukiwa wa uhalifu zidadavuliwe na ziwekwe sawa ili tujue kutofautisha kati ya Utekaji na ukamatwaji unaofanywa na vyombo vya ulinzi na usalama.
Ikumbukwe kuwa kanuni moja wapo ya haki inaeleza kuwa, ni bora kuwaachia watu mia wenye hatia, kuliko kumfunga mmoja asiye na hatia.
Kwa namna hii tutakomesha matukio ya utekaji yanayofanywa na Askari waliokosa weledi na wanaotumika kisiasa.
Mathalani mpaka sasa kuna guidelines kama;
1. Bail Guidelines (2020)
2. Execution Guidelines (2020)
3. The Tanzania Sentencing Guidelines (2023)
4. Exhibit Management Guidelines(2020)
Hii ni baadhi tu ya miongozo. Kwamba, japo taratibu zipo ndani ya sheria husika, Mahakama iliona ni vyema kudadavua taratibu hizo ili kuepusha mkanganyiko.
Nashauri sasa Mahakama ituletee ARREST GUIDELINES (Miongozi ya ukamataji) Taratibu za ukamataji wa washukiwa wa uhalifu zidadavuliwe na ziwekwe sawa ili tujue kutofautisha kati ya Utekaji na ukamatwaji unaofanywa na vyombo vya ulinzi na usalama.
Ikumbukwe kuwa kanuni moja wapo ya haki inaeleza kuwa, ni bora kuwaachia watu mia wenye hatia, kuliko kumfunga mmoja asiye na hatia.
Kwa namna hii tutakomesha matukio ya utekaji yanayofanywa na Askari waliokosa weledi na wanaotumika kisiasa.