Kupanda ghafla kwa bei ya nyanya na mbogamboga iwe funzo kwetu

mitale na midimu

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2015
Posts
10,420
Reaction score
17,735
Bei ya nyanya iko juu. Mtaani kwetu wameacha kabisa kuuza.

Wakina mama wapika mihogo nimeona sehemu wanatumia matango kama nyanya Ktk kachumbari.

Leo nimeshangaa pia eti bamia moja inauzwa 100 mtaani.
Vitunguu na mbogamboga poa ziko juu.

Sababu
Nimefuatilia sababu wanasema mvua zilizozidi ndio chanzo.

Utatuzi wa kudumu na ushauri

Ule utamaduni wa kupanda maua majumbani ubadilishwe Kwa kupanda mbogamboga.

Mfano ukipanda kaeneo kadogo matembere yatastawi hata ukimwagilia maji ya sabuni.

Panda mbogamboga, nyanya, Vitunguu, karoti Ktk makopo.


Hii itasaidia kupunguza gharama ndogondogo zinazoepukika.

Mkeo, housegirl, ndugu unaoishi nao, watoto wako au wewe mwenyewe badala ya kufanya jogging gym, au barabarani, au kuangalia movies kuhudumia bustani ya nyumbani hata nusu saa ni zoezi tosha Kwa wenye Muda.
 
Kwa kuongezea pia unaweza kukausha mbogamboga kipindi cha mavuno na kuweka kwenye container ukatumia kwa mwaka. Waweza kukausha nyanya, vitunguu, tangawizi, tembele, majani ya kunde, n.k
 
Kwa kuongezea pia unaweza kukausha mbogamboga kipindi cha mavuno na kuweka kwenye container ukatumia kwa mwaka. Waweza kukausha nyanya, vitunguu, tangawizi, tembele, majani ya kunde, n.k
Wengi watakubishia wakisema vikikaushwa hukosa virutubisho.

Waroho watakuambia sio tamu.

Kuna jamaa Mmoja US hununua Apples wakati bei ni ya kutupwa. Anablend anapaki kwenye jars na hanunui tena mwaka mzima hadi msimu ujao.

Elimu hii isisitizwe kuanzia shuleni
 
CC: Carleen ukuje huku,
Upate somo, kachumbari na mihogo kila weekend.
Nyanya za kachumbari unachuma toka ktk garden yako ya makopo.
 

Na kwa wapangaji chumba kimoja nao unawashauri nini?
 
Mkuu vipi kuhusu sie tunaoishi kkoo



Sent using Jamii Forums mobile app
 


Asante mkuu.
 
Kikaushio kama iko kwa dar kinapatikana wapi?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…