DR Mambo Jambo
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 11,622
- 26,005
Nawasalimia kwa Jina La JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Kabla ya yote mimi si Mjuzi sana wa mambo ya Uchumi au siasa ya uchumi ila kwa kuwa nimepata ushauri kwa wasomi wa uchumi na mambo haya ya siasa ya uchumi ningependa niwamegee kidogo kuhusu mambo nikiyoelekezwa kuhusu Trending marks iitwayo "UPANDISHWAJI WA BEI ZA MIAMALA YA SIMU" (Kama utaona mapungufu naomba marekebisho).
Kwa rejea nzuri naomba soma Luka 1:1-4 (kwa niliyoongea hapo juu) kwa wale watu wa Dini lakini...
Tuendeleee....
Kwanza ningependa turejee Tafiti mbalimbali zilizo jikita katika kuangalia uhai wa mabenki hasa COBAT,BOT na World Bank (Rejea tafiti mbalimbali kutoka COBAT "wadau wa jumuia ya mabenki ya wananchi")
Mwaka 2017 Serikali kupitia Gavana mkuu wa serikali ilifungia mabenki matano ikiwemo Mbinga Community Bank PLC ikiwa ni kwa kuwa na upungufu mkubwa wa mtaji,Na usalama wa sekta ya fedha na amana za wateja..,Na baadae kutoa onyo kwa mabenki mengine MATATU...
Kabla ya hayo yote naomba kuwapeleka darasani kidogo kuhusu somo la mtaji wa kibenki (Banking capital) ili tuelewe wanaposema mabenki yameishiwa mtaji maana yake nini?
Mtaji wa kibenki(banking capital):-
Mtaji wa kibenki ni tofauti ipatikanayo kati ya miliki za benki (banki assets) na dhamana au dhima ya benki husika (bank liabilities).
Kwa lugha ya wenzetu ningesema;- Banking capital is the different between bank assets and bank liabilities
Bank assets au Milki za benki ni zile shughuri zote za kifedha ambazo benki inazifanya kujiingizia kipato au kile kiasi cha mikopo iliyotolewa na benki kwa serikali u mashirika mengine na vingine vinavyofanana na hivyo.
Mfano mwingine wa assets za benki ni CASH yaani fedha zipatikanazo kutoka kwa watu... yaani chukulia wewe umeemda kuweka pesa banki hiyo kwao inakuwa ni assets yaani mali inazomiliki au wewe umekopa pesa banki hiyo inakuwa ni mali miliki ya benki. Wenyewe wanazitenga kweye solid assets (eg account) na liquid assets (cash).
Na Bank liabilities ni zile dhamana benki iliyonazo kwa mfano Kodi malipo mbalimbali,TRA , malipo ya jengo malipo ya mishahara na mikopo mbalimbali ambayo benki inaweza ikawa imeingia kwa uendeshaji...
Nafikiri kwa hapo juu tutakuwa tumeelewana saana sasa twende tuingia kidogo mwanzo wa mada kabla sijatoa maelezo.
Kutokana na kuzidi kwa gharama za uendeshaji wa benki nyingi ikiwemo malipo ya kodi kuwa makubwa na gharama nyingi ambazo zingine zitazielezea imefanya mabenki mengi kuwa na liabilities nyingi sana wakati huohuo assets kubaki kama zilivyo au kupungua kabisa.. Hivyo kusababisha mashirila mengi ya kibenki kuingia hasara kuliko faida wanayopata.
JINSI BENKI INAVYOWEZA KUFANYA KUONGEZA KIPATO NA KUONGEZA UCHUMI
Benki hukusanya fedha zilizohifadhiwa (bank assets) yaani kutoka kwenye account mbalimbali na kuwakopesha wafanyabiashara,wahisani, Viwanda na hataa serikali kwa riba maalumu ambayo nayo huchangia mzunguko wa pesa ili kurahisisha biashara kuendelea.kwahyo serikali hupata pia pesa kutoka na Income tax inayotokana na benki.
MASHIRIKA YA SIMU YAMECHANGIAJE KUSHUSHA THAMANI YA BENKI(KUPUNGUZA MITAJI YA MABENKI)?
Ni swali ambalo wengi wanajiuliza sana ila nitajatibu kulijibu kutumia maelezo niliyotoa hapo awali.
Jamii nyingi ya kitanzania imeona vyema kuhifadhi pesa kwa njia ya simu ili kwanza kurahisisha miamala ya kifedha ,pili kupunguza makato mengi na kutuma na kupokea pesa tatu urahisi wa kupata huduma hizo za benki za simu (sitazitaja lakini hizi huduma za pesa kwenye simu)
Kwani mara nyingi mtu anaweza kuweka pesa kwenye simu bila kupata makato ya uendesheji ya kila mwezi au pesa ya ATM au mengine yanayofanana na hayo hivyo..kufanya wimbi kubwa la watu kuhamia katika huduma hizi za simu.
Na kuacha huduma za Banki ambazo zimekuwa na makato makubwa ya kiuendeshaji....Watu wengi kuacha kufanya miamala ya kibenki na kuanza kufanya miamala katika mashirika ya simu,Kumepunguza wateja wengi kujiunga au kuendelea kutumia huduma za kibenki hivyo kufanya huduma hizo kushuka kidogo (kwani assets imeshuka au kubaki constant while liabilities kuzidi kupanda).
Kutetereka kwa assets kumefanya benki nyingi kushindwa kujiendesha na nyingine kufilisika.
KUPANDA KWA MIAMALA YA SIMU NI BENKI ECONOMIC STRATEGIES
Sasa kwakuwa serikali ilikuwa ikipata pesa kwa ajili ya kutekeleza ama bajeti au baadhi ya miradi imekuja na hii strategies ili kupata tozo ya miamala moja kwa moja kutoka katika mitandao ya simu hii itarudisha aidha uhai wa benki kwani watu wataona bora waweze kuweka pesa benki kuliko kwenye mitandao ya simu au serikali itapata pesa moja kwa moja na kuongeza pato la uchumi wetu ...kwahiyo Kwa asilimia fulani naona uhainwa Baadhi ya benki ukirudi kwani tozo za Benki bado zipo chini ukilinganisha na tozo za simu..
Yaliyoandikwa juu ni mawazo yangu na ningependa mwenye mawazo makubwa kuliko mimi anisahihishe
Asante
Dr Mambosasa Asante
Kabla ya yote mimi si Mjuzi sana wa mambo ya Uchumi au siasa ya uchumi ila kwa kuwa nimepata ushauri kwa wasomi wa uchumi na mambo haya ya siasa ya uchumi ningependa niwamegee kidogo kuhusu mambo nikiyoelekezwa kuhusu Trending marks iitwayo "UPANDISHWAJI WA BEI ZA MIAMALA YA SIMU" (Kama utaona mapungufu naomba marekebisho).
Kwa rejea nzuri naomba soma Luka 1:1-4 (kwa niliyoongea hapo juu) kwa wale watu wa Dini lakini...
Tuendeleee....
Kwanza ningependa turejee Tafiti mbalimbali zilizo jikita katika kuangalia uhai wa mabenki hasa COBAT,BOT na World Bank (Rejea tafiti mbalimbali kutoka COBAT "wadau wa jumuia ya mabenki ya wananchi")
Mwaka 2017 Serikali kupitia Gavana mkuu wa serikali ilifungia mabenki matano ikiwemo Mbinga Community Bank PLC ikiwa ni kwa kuwa na upungufu mkubwa wa mtaji,Na usalama wa sekta ya fedha na amana za wateja..,Na baadae kutoa onyo kwa mabenki mengine MATATU...
Kabla ya hayo yote naomba kuwapeleka darasani kidogo kuhusu somo la mtaji wa kibenki (Banking capital) ili tuelewe wanaposema mabenki yameishiwa mtaji maana yake nini?
Mtaji wa kibenki(banking capital):-
Mtaji wa kibenki ni tofauti ipatikanayo kati ya miliki za benki (banki assets) na dhamana au dhima ya benki husika (bank liabilities).
Kwa lugha ya wenzetu ningesema;- Banking capital is the different between bank assets and bank liabilities
Bank assets au Milki za benki ni zile shughuri zote za kifedha ambazo benki inazifanya kujiingizia kipato au kile kiasi cha mikopo iliyotolewa na benki kwa serikali u mashirika mengine na vingine vinavyofanana na hivyo.
Mfano mwingine wa assets za benki ni CASH yaani fedha zipatikanazo kutoka kwa watu... yaani chukulia wewe umeemda kuweka pesa banki hiyo kwao inakuwa ni assets yaani mali inazomiliki au wewe umekopa pesa banki hiyo inakuwa ni mali miliki ya benki. Wenyewe wanazitenga kweye solid assets (eg account) na liquid assets (cash).
Na Bank liabilities ni zile dhamana benki iliyonazo kwa mfano Kodi malipo mbalimbali,TRA , malipo ya jengo malipo ya mishahara na mikopo mbalimbali ambayo benki inaweza ikawa imeingia kwa uendeshaji...
Nafikiri kwa hapo juu tutakuwa tumeelewana saana sasa twende tuingia kidogo mwanzo wa mada kabla sijatoa maelezo.
Kutokana na kuzidi kwa gharama za uendeshaji wa benki nyingi ikiwemo malipo ya kodi kuwa makubwa na gharama nyingi ambazo zingine zitazielezea imefanya mabenki mengi kuwa na liabilities nyingi sana wakati huohuo assets kubaki kama zilivyo au kupungua kabisa.. Hivyo kusababisha mashirila mengi ya kibenki kuingia hasara kuliko faida wanayopata.
JINSI BENKI INAVYOWEZA KUFANYA KUONGEZA KIPATO NA KUONGEZA UCHUMI
Benki hukusanya fedha zilizohifadhiwa (bank assets) yaani kutoka kwenye account mbalimbali na kuwakopesha wafanyabiashara,wahisani, Viwanda na hataa serikali kwa riba maalumu ambayo nayo huchangia mzunguko wa pesa ili kurahisisha biashara kuendelea.kwahyo serikali hupata pia pesa kutoka na Income tax inayotokana na benki.
MASHIRIKA YA SIMU YAMECHANGIAJE KUSHUSHA THAMANI YA BENKI(KUPUNGUZA MITAJI YA MABENKI)?
Ni swali ambalo wengi wanajiuliza sana ila nitajatibu kulijibu kutumia maelezo niliyotoa hapo awali.
Jamii nyingi ya kitanzania imeona vyema kuhifadhi pesa kwa njia ya simu ili kwanza kurahisisha miamala ya kifedha ,pili kupunguza makato mengi na kutuma na kupokea pesa tatu urahisi wa kupata huduma hizo za benki za simu (sitazitaja lakini hizi huduma za pesa kwenye simu)
Kwani mara nyingi mtu anaweza kuweka pesa kwenye simu bila kupata makato ya uendesheji ya kila mwezi au pesa ya ATM au mengine yanayofanana na hayo hivyo..kufanya wimbi kubwa la watu kuhamia katika huduma hizi za simu.
Na kuacha huduma za Banki ambazo zimekuwa na makato makubwa ya kiuendeshaji....Watu wengi kuacha kufanya miamala ya kibenki na kuanza kufanya miamala katika mashirika ya simu,Kumepunguza wateja wengi kujiunga au kuendelea kutumia huduma za kibenki hivyo kufanya huduma hizo kushuka kidogo (kwani assets imeshuka au kubaki constant while liabilities kuzidi kupanda).
Kutetereka kwa assets kumefanya benki nyingi kushindwa kujiendesha na nyingine kufilisika.
KUPANDA KWA MIAMALA YA SIMU NI BENKI ECONOMIC STRATEGIES
Sasa kwakuwa serikali ilikuwa ikipata pesa kwa ajili ya kutekeleza ama bajeti au baadhi ya miradi imekuja na hii strategies ili kupata tozo ya miamala moja kwa moja kutoka katika mitandao ya simu hii itarudisha aidha uhai wa benki kwani watu wataona bora waweze kuweka pesa benki kuliko kwenye mitandao ya simu au serikali itapata pesa moja kwa moja na kuongeza pato la uchumi wetu ...kwahiyo Kwa asilimia fulani naona uhainwa Baadhi ya benki ukirudi kwani tozo za Benki bado zipo chini ukilinganisha na tozo za simu..
Yaliyoandikwa juu ni mawazo yangu na ningependa mwenye mawazo makubwa kuliko mimi anisahihishe
Asante
Dr Mambosasa Asante
Upvote
8