Kupatikana Katiba Mpya katika taifa lolote huambatana na matukio mabaya, maumivu makali

Kupatikana Katiba Mpya katika taifa lolote huambatana na matukio mabaya, maumivu makali

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,252
Reaction score
8,003
Mimi nawashangaa sana wanachama CHADEMA na wafuasi wao kwa ujumla kulalamika mitandaoni kwa kukamatwa kwa sababu ya kudai katiba mpya, katiba mpya duniani kote hupatikana kwa maumivu makali sana yanayoambatana na watu kuumizwa na hata wengine kupotea.Kama mnadai katiba mpya haifikirii haya bora muache kucheza sarakasi zenu.

Itazameni katiba ya Kenya iliyopatikana baada ya maumivu makali ya 2007, itazameni katiba ya Afrika kusini iliyopatikana baada ya maumivu makali vile vile. Hizi katiba kwa sasa zinasifiwa kua ni bora kwa ukanda huu wa Afrika. Katiba ya Zanzibar ilipatikana vipi hadi kufikia kua na serikali ya umoja wa kitaifa?

Mnashindwa kuelewa kua na asilimia ya katiba ni makubaliano na maelewano baada ya watu kuumizwa ndipo wakae mezani wakubaliane. Hakuna katiba rahisi, JK alikwama kwa sababu njia iliyotumika ya kuipata katiba mpya ilikua si ya kawaida na pengine ingefanikiwa Tanzania tungevunja rekodi ya dunia.

Watawala hawako tayari kuunda katiba iwapunguzie power, eleweni hivyo.Hii bit ya kujenga uchumi kwanza ni geresha na Hadaa kwa wananchi wenye akili ndogo.
 
Wala sio lazima mbona uhuru tukipata smoothly tu

Tuachane na hizi classical idea
 
Wala sio lazima mbona uhuru tukipata smoothly tu

Tuachane na hizi classical idea
Kwa hiyo kwa akili zako hizo nusu kijiko unafikiri maccm yatalala kisha yaamke na kusema leo tunawaletea watanzania Katiba bora,thubutu nchi hii mpaka tutoane ngeu ndio kitaeleweka.
 
Kwa hiyo kwa akili zako hizo nusu kijiko unafikiri maccm yatalala kisha yaamke na kusema leo tunawaletea watanzania Katiba bora,thubutu nchi hii mpaka tutoane ngeu ndio kitaeleweka.
Kutoana ngeu mkuu ni kitu kigumu nchi hii
Just imagine nani na nani watajuana ngeu kwaajili ya nani ?
 
Si lazima usituletee ujinga wenu hapa, tunaweza kupata katiba bila maumivu hatuko kwenye vita


USSR
 
Kwa hiyo kwa akili zako hizo nusu kijiko unafikiri maccm yatalala kisha yaamke na kusema leo tunawaletea watanzania Katiba bora,thubutu nchi hii mpaka tutoane ngeu ndio kitaeleweka.
So unapambana na nguvu huna


USSR
 
Back
Top Bottom