Kupiga Picha ukiwa ama umeshika Gari la Kifahari au umekalia katika Kiti cha Dereva huku ukijijua kabisa kuwa hujui hata Kuendesha kuna maanisha nini?

Kupiga Picha ukiwa ama umeshika Gari la Kifahari au umekalia katika Kiti cha Dereva huku ukijijua kabisa kuwa hujui hata Kuendesha kuna maanisha nini?

Mzukulu

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2020
Posts
1,401
Reaction score
2,641
Mliosoma na Kubobea hasa katika Saikolojia hii hali huwa mnaiitaje na Kitendo husika pia huwa kina maana gani kwa Mhusika?
 
Kwa wengine inaweza ikawa ni motivational/driving factor akitamani kufikia mafanikio hayo kwa siku za usoni..
..Wengine hupiga ili kutry kufit in kwenye class ambayo hayupo ili aonekane na ye yumoo(Kujimwambafai)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wazazi wako kijijini wanakuona fb na insta wanakuwekea kinyongo kijana wao wanaumwa unashindwa hata kuwanunulia hata panadol za kutuliza maumivu kumbe sio gari yako hata oni ujui inakaa wapi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi sio magari tu, hata nyumba kali huwa sipendi shobo nazo kupiga picha.
Hata Mlimani City siingii, achana na kupiga picha kule. Siwezi toka hapa niende kupeleka mikojo yangu kwenye ofisi za watu na hakuna kitu naenda nunua. Nikienda sehemu nakuwa nahitajika, nikipiga picha na kitu huwa kinanihusu.

Mimi najua class yangu na ndo nakaa nayo, nahangaika kutoka na najua ni suala la muda tu. Unakuta mtu anajikomba kwa marafiki zake walioenda Singapore, India, SA, Canada. Akipata shida au akiwa na event hawana shobo nae.
Unakuta mtu anajizungusha na mademu wakali ila mara zote anadate na kina miss Buza tu.
Ni sawa na hizo gari, pata shida ya kwenda hospitali uone kama kuna Mark X au Subaru itatoka uko kukubeba. Utabebwa na bajaj ukibahatika ist.
Huwa sina kiherehere na vitu vya level ya juu yangu.

NB: Nawasema wenzangu na mimi ambao wengi humu hawapo. Humu wengi wana magari na maisha mazuri.
 
😂😂
Unapiga picha kwenye mjengo wa watu alafu unaandika "home sweet home"....mburaaaa
 
Back
Top Bottom