Kupigwa marufuku kwa Micron kwailetea Marekani wasiwasi mkubwa

Hiyo ni internal affairs watamaliza wenyewe, hakuna nchi isiyo na matatizo ya ndani, waacheni wenyewe ndio wanawajibika kwa nchi yao, sioni kama kuna jambo kubwa la kujadili, ni kama hapa kwetu tunavyo maliza matatizo ya Zanzibar wakati wa uchaguzi wala hakuna anae tuingilia
 
Fatilia mkasa wa Urygur, falun Gong, na Tibet.

Wachina wenyewe ndio wanaprotest kule USA na Europe kwa kinachoendelea kule wakilalamika mataifa yako kimya kutokana na uvynjwaji wa haki za binadamu unaoendelea.

Kama ni internal affairs, why the same Chinese protest over their own government?

Kwa kifupi haki za binadamu ni haki za kila mmoja, kila mtu ana haki ya kuishi, ukishakuwa unapora haki za kuishi za watu maana yake ww haufai tena.

Kila Mwanadamu anatakiwa achukuliwe kama mwanadamu na sio Commodity, China mtu anaweza kuwa mtu au commodity..!, hawajali utu wa mtu mifano tunayo kwenye makampuni yao hata yaliyopo Tanzania, hawathamini utu kabisa.
 
Narudia tena haya ni mambo ya ndani, nchi ikiingia kwenye machafuko serikali ndio itabeba lawama kwahiyo lazima waje Na solution, hapa kwenye solution kuna watakao umia sasa serikali haiwezi kuacha kuokoa watu 1000 kwasababu ya kelele za mtu 1, lakini linapo kuja suala la uharibifu huwezi kumtoa US ameharibu kila pembe ya Dunia, ameweka base kila pembe ya Dunia, lakini mchina akitaka kujitanua inakuwa kosa haya ni maajabu makubwa, anataka kufanya yeye ndio mwenye hati miliki ya Dunia wengine hawana haki hapana
 
Unakumbuka kipindi cha Magufuli, yaliyokuwa yanafanywa na makonda mpaka akapigwa ban ya kukanyaga US.

Wewe unaona ni sawa, asikemewe kwa kuwa ni mambo ya ndani.

Unaelewa vizuri chanzo cha covid 19, unajua kama sio usiri na kama kungekuwa na uwazi covid 19 isingeweza kuenea pote Dunia na kupelekea vifo vya zaidi ya watu milion 6. Unaona jinsi mambo ya ndani ya nchi moja tu yalivyoitaabisha Dunia.

Narudia hakuna Mataifa ya kidemokrasia yatakubaliana na uvamizi wa China kwa Taiwani, Never! umoja wa kujihami wa ulaya, NATO anangalia namna ya kufungua ofisi zao Japan mahsusi kudili na haya maswala.

Hauwezi ukatishia usalama wa watu zaidi ya milion 25 halafu basi tu watu wakuangalie, ina maana hamna namna nyingine ya amani ya kuwezesha reunion mpaka vita?

Xi anawaponza wachina, from the moment atakapoagiza uvamizi Taiwan ndipo atakuwa ameitumbukiza China shimoni.
 
Mzee acha Propaganda, umoja wa mataifa una heshimu mamlaka ya kila mtu, sasa US anapo mkataza Makonda asiende US ndio nini?hayo ni maamuzi yao ya ndani, hata Ukraine walifanya mapinduzi kumtoa Rais aliechaguliwa kidemokrasia lakini hakuna alie waingilia utaambiwa hizo ni internal Affairs, China ina katiba yake waacheni wafanye mambo yao kwa mujibu wa katiba zao Na sera zao, narudi pale US hana cha kumfunza Mchina maana yeye ndio muharibifu nambari moja tumeona kavamia Iraq, Afghanistan, vile vile yupo Syria wakati hakuna alie mpa mualiko, hivyo basi US hana cha kuwafunza wengine
 
Mzee human rights abuse haikubaliki popote pale ulimwenguni,

Fanya mambo yako yote kama utakuwa unavunja haki za binadamu hapo lazima watu wadili na ww.
 
Mzee human rights abuse haikubaliki popote pale ulimwenguni,

Fanya mambo yako yote kama utakuwa unavunja haki za binadamu hapo lazima watu wadili na ww.
Human right ipi? huwezi kulazimisha nchi ikubali mashoga, kila nchi ina mambo yake , ndio maana hata US yenyewe haipo kwenye mahakama ya kihalifu ya Kivita (ICC), kwahiyo uharibifu wowote atakao fanya kwenye vita hakuna pa kumshtaki, haya mambo ni uamuzi wa nchi kuyaendea
 
Falun Gong? Waisilam wa Urygur? Tibet? Hong Kong? Forced labour kwa human right activist?

Hayo yote ni urembo?
 
Falun Gong? Waisilam wa Urygur? Tibet? Hong Kong? Forced labour?
Mbona US kaenda kuwavamia waislamu wa Taliban , cha kuchekesha kaondoka hata wiki bado wamerudi tena, sasa unataka Mchina atulie mpaka mambo yaharibike? halafu mtakuja kumsaidia vikundi kama al shabab vikianza? Haya yote ni mambo ya ndani wala sio jambo la US Na wengine kuingilia, wenye nchi ndio jukumu lao kulinda nchi maana wana intelejensia ya kutosha kugundua hatari, sasa Forced Labour hayo ni mambo binafsi ambayo hata serikali inahitaji kupokea taarifa kama ipo
 
Mkuu unapropaganda za kizamani sana. Unafahamu one china policy?
Je unajua inafahamika maifa yote including UN ndio maana Taiwani haina kiti UN.

Hilo tu linakuonesha hujui unachosema kuhusu China.

Pia unafahamu makampuni yanazaliwa, yanakuwa na yanakufa? Kama unafahamu hii principle ya uhai wa makampuni usingetoa hayo uliyosema, eti makampuni yanahama au kufungwa ni natural phenomena.

Je unafahamu kukua kwa makampuni kunategemea principle kuu mbili Supply and Demand. Hivyo kama kuna mahitaji biashara itafanyika tu.
Pia kuna suala la cost of production (production function) ukivijua hivi pia hutaona sababu ya huyu kuingia au kutoka kwenye soko fulani, its a natural phenomena. Hapa Tanzania Game, Shoprite, Nakumat.... wameondoka. Je walikorofishana na nani? Lakini wakati hao wanaondoka Rafiki supermarket, Kilimanjaro, na wameingia... ni kawaida.

Mwisho unajua China kwa sasa ndio mzalishaji na muuzaji mkubwa wa magari duniani Japan amekuwa wa pili.

Kama unajua hesabu vizuri nataka ujibu hilo ongezeko la uuzaji magari limepelekea kupungua kwa ajira au ongezeko?

Uchumi kudorora duniani lazima ajira zitashuka (one of lockdown effect) kwa sasa China amefungua uchumi na bado haiujafikia pre covid level hivyo tegemea high level of unemployment
 
Mbona wachina ndo mnateseka kuliko Marekani?
 
Mzee mi nafatilia kwa ukaribu sana haya mambo more than you think,

Nafahamu kabisa one China policy, na Nia yao ya rejuvenation but, why Taiwan? Kwanini vita? Kwani hamna Nia nyongine?

Unasema uchumi unategemea supply and demand, sawa sikatai na pia sikatai China ndio mzalishaki mkubwa wa magari, ninachozungumzia mm hapa ni kwamba sera mbaya zinaweza kutishia uwekezaji na ukapelekea biashara kudorora

Unemployment rate kwa sasa China ipo juu kuliko kipindi vyote tangu China wafungue nchi yao, estimation zinasema 20.4% ya watu kati ya umri wa miaka 16 mpaka 24 hawana ajira, vyanzo vingine vinadai zaidi ya wachina milion 200 hawana ajira rasmi kwa ujumla, hivyo ni vyanzo vyao wenyewe.

Sasa kama watu wanaajiriwa na kuacha why wao wenyewe wawe na wasiwasi haswa kwa kipindi hiki?
 
Kama unafahamu One China Policy kinachomfanya marekani aingilie mambo ya ndani ya China ni kitu gani. Nashukuru umesema unafuatilia mambo ua China. Kwa vyovyote China lazima atumie nguvu na hata military force siiti vita maana ni internal operation. Yaani Zaznibar ianze kupewa vifaru, magari vita pasipo approval ya URT, unafikiri Madam President atakaa kimya.

Hii ndio maana nasema tuache propaganda za nchi za watu
 
Unafatilia yaliyotokea na yanayoendela Hong Kong?

Uingiliaji unakuja pale ambapo haki za binadamu zinavunjwa, hauwezi ukavunja haki za binadamu watu wakuangalie tu.?

CCp Ameshanyanyasa waamini wa dini tofauti tofauti, ana scandle ya forced organ harvesting kwa waamini wa falun Gong, na waislamu wa Urygur, bado tena anataka kuextend huu ushenzi mpaka Taiwan kisa watu wamemkalia kimya. Dunia haitoweza kukubaliana na hilo
 
Ukiona hivi ujue China ame break through kwenye semiconductors. Usishangae kusikia tayari wana chip za 4nm. Vikwazo vya US kwa China kwenye semiconductor vime backfire.
 
Acha uongo mkuu ....hongkong alipokuwa chini ya waingereza haikuwa na demokrasia yoyote Tena wachina waliuwawa walipojaribu kuprotest.....hongkong imeachiliwa juzi tu na makubaliano yalikuwa ni kujiunganisha na main land within 50 years of independence.......kwahiyo ukisikia UK itawasaidia sijui tutaganya nini. ....ni uongo tu watu wametawaliwa mpaka miaka ya tisini(ukoloni wa kweli).
 
Nmeona wanalalamika eti china ina target makampuni yao na hilo hawawezi kuruhusu nikashangaa mbona wao waliganya same kwa huawei. Micron ilikuwa inaiza 10% ya chips zake kwa china
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…