Kupima mirija ya uzazi na mbegu za kiume

Kupima mirija ya uzazi na mbegu za kiume

Mkombozi

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2008
Posts
844
Reaction score
476
Wakuu naomba kujua je kupima mirija kama imeziba au la,ya kupitishia mayai ya uzazi ya mwanamama.

Je mirija hupimwaje?

Pili je kupima mbegu za kiume,nazo hupimwaje?

Mbegu zipi nzuri,za kuchua au zinazopatikana wakati wa tendo?
 
niliwahi kuandikiwa na kuwa nipime hiko kipimo cha kucheck mirija aghakhan Hosp, kina masharti yake ya siku za kupima, na ni dawa inainginzwa huku ndani kwa bibi, ukienda hosp watakuelekeza zaidi
 
upimaji mbegu za kiume unaitwa male factor au Seminalysis. Huwa zinatakiwa shahawa za mwanamme kwenda kupimwa. Masharti: kabla ya kuchukua shahawa,mwanamme anatakiwa asiwe ame sex na kumwaga shahawa kwa siku 4-5. Lengo ni kupata shahawa zenye mbegu zilizokomaa. Inatakiwa lisivuke muda wa saa 1 toka umezipata shahawa na kuzifikisha maabara hivyo JIPANGE jinsi ya kuendana na muda huo.Wakati wa kuzipeleka,zinatakiwa zisipate ubaridi wowote bali zipate joto la mwili,hivyo unashauriwa uhifadhi kichupa cha mbegu aidha kwapani au kati ya mapaja(hapa napo JIPANGE).Njia kuu za kupata shahawa ni mbili.1. Kufanya mastabesheni na kumwagia goli la kwanza kwenye kichupa maalum utakachopewa. 2. Kufanya mapenzi namkeo,na kuwa makini kuchomoa dushe na kumwaga shahawa za goli la kwanza kwenye kichupa maalum utakachopewa. Kumbuka ni shahawa za bao moja la kwanza tu ndio zinatakiwa. Majibu kwamba mbegu zipi ni bora ni ya kitaalamu zaidi na nikiweka hapa tutajaza seva lakini huwa zinaangaliwa uwezo wa kuogelea ukeni,ubora wake,PH yake nk. Mengineyo dokta wako aweza kukufafanulia. Kama kuna mengine sensitive wataka jua,ni PM.
 
Wakuu bila shaka mko poa. Naona hii ya upimaji imeelezea upande mmoja wa mwanaume. Je, kwa mwanamke kipimo kinafanyikaje?

Shukran.
 
Back
Top Bottom