Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Kama mmeona sasa hivi upande wa CCM kila wakifanya mkutano kiongozi husika anapotishwa bila kupingwa kienyeji ama anaombewa kisayansi kupitishwa bila kupigwa!
Ilianza kwa Samia na Mwinyi, Diwani akataka Silaa apitishwa bila kupingwa, Rufiji nao wakampitisha Mchengerwa bila kupingwa na kwa Biteko leo limepenyezwa pia kisayansi!
Haya hayafanywi kwa bahati mbaya, kila kitu kimepangwa vizuri. Taratibu itaonekana kama kawaida kwa kuwa CCM wanafanya na watataka hili lifanyike hivyo hivyo kwenye Uchaguzi Mkuu, ya 2020 yajirudie tena. Baada ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuwa ovyo kuwahi kutokea Uchaguzi Mkuu utaenda kuwa wa kipuuzi zaidi.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Sheria ya uchaguzi imesema hilo limekoma 2020, hakutakuwa na kupitwa bila kupingwa tena kwanini lianze kupenyezwa sasa hivi?
Wnanatengeneza njia kwa wale vigogo serikalini kurudi wote serikalini 2025, wameona bila janja janja hawawezi kupita, tukemee haya mapema. Sheria isimamiwe.
Sina hakika hili likoje kutokana na katiba ya CCM Pascal Mayalla, Kiranga na wengine naomba mwongozo hapa.
Februari
Kama mmeona sasa hivi upande wa CCM kila wakifanya mkutano kiongozi husika anapotishwa bila kupingwa kienyeji ama anaombewa kisayansi kupitishwa bila kupigwa!
Ilianza kwa Samia na Mwinyi, Diwani akataka Silaa apitishwa bila kupingwa, Rufiji nao wakampitisha Mchengerwa bila kupingwa na kwa Biteko leo limepenyezwa pia kisayansi!
Haya hayafanywi kwa bahati mbaya, kila kitu kimepangwa vizuri. Taratibu itaonekana kama kawaida kwa kuwa CCM wanafanya na watataka hili lifanyike hivyo hivyo kwenye Uchaguzi Mkuu, ya 2020 yajirudie tena. Baada ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuwa ovyo kuwahi kutokea Uchaguzi Mkuu utaenda kuwa wa kipuuzi zaidi.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Sheria ya uchaguzi imesema hilo limekoma 2020, hakutakuwa na kupitwa bila kupingwa tena kwanini lianze kupenyezwa sasa hivi?
Wnanatengeneza njia kwa wale vigogo serikalini kurudi wote serikalini 2025, wameona bila janja janja hawawezi kupita, tukemee haya mapema. Sheria isimamiwe.
Sina hakika hili likoje kutokana na katiba ya CCM Pascal Mayalla, Kiranga na wengine naomba mwongozo hapa.
Februari