Elections 2010 Kura za maoni Voice of America (VoA)

sikatai vyama vya upinzani ni maarufu sana sehemu za mijini.. kulipo jaa utandawazi wa kila aina, lakini mjue ushindi wa ccm utatoka kule kwenye Mizizi yake Vijijini, kwa wale wazee amabo bado wanamuona nyerere kama mungu!, huku mjini mtaishia kusema mmeibiwa kura mbona mmeongoza katika kura za mitandaoni.. wa tz wapo milion 40, na wote hawakai mijini
 
voiced of amerca haisililizwi hata na 1% of watanzania
Mwikimbi,
Katika figures za 2007 Voice of America ilikuwa inasikilizwa na 28% ya wakazi wa Dar-es-Salaam na 22% ya Watanzania wote. Lakini ninachotaka kusema ni kwamba hawa VOA wamekuwa waoga katika kura zao za maoni. Kwa nini hawakuuliza the obvious? Kati ya wagombea urais mwaka huu ni nani unayeona anafaa kuwa rais? Obviously Slaa angeongoza.
 

Cha ajabu walikuwa wanatuuliza hata sisi tusio wamarekani nani atashinda kati ya Obama na Mccain
 

the issue here is hao watanzania watakao piga kura ni proportion ipi ya population ina access na mtandao ili iweze kupiga kura na je hii sample sio bias kweli kwa sababu inajumuisha a certain type of sample unit na haijumuishi characteristics zote zilizopo katika industry, mimi na hisi mbali namapenzi yangu kuiona tanzania yenye neema ni vyema tusi wa miss read watu pale tunapozungumzia technical issue is better misimamo na mapenzi yetu ya kisiasa tukaiweka pembeni kwa maslai ya taifa.
 

Ndugu yangu Ibrah afadhali umempa darasa huyo Mwakimbi. Namshangaa kuwa ana umri gani au amekulia Tanzania ipi. Maana watu wanasilikiliza Dutch Welle, BBC na VOAi kuanzia miaka ya 60 mpaka mwishoni mwa miaka ya 90 ndio kuchipuka hizo redio zinazoitwa FM.

Na hata hizo FM baada kuanza pia zilikuwa hazipewi leseni ya kutangaza Tanzania nzima, walikuwa wanapewa leseni ya kanda (eti kwa usalama wa taifaπŸ™‚, kabla haijabadiliswa miaka ya karibuni. Na wakati huo huo RTD ilikuwa ni shida kusikika mikoa kama ya Mwanza Mbeya, Songea, Kigoma, Bukoba kama vile sio sehemu ya nchi.

Lakini Tanzania nzima watu wakawa wanasikiza sauti ya UJerumani (Dutch welle), BBC na VOA. Na mpaka leo Watanzania wengi haswa waishio maeneo ya vijijini kabisa (uswekeni huko) utawakuta jioni watu wamekusanyika kusikiza radio za nje. Ndio maana namuuliza huyu Mwakimbi ana umri gani au amekulia Tanzania gani?
 
yangu macho pale upinzani watakapoipeleka mchakamchaka serikali bungeni,,
oct 31
 
Latest news from VoA Polls in just 5mins ago looks like below !!!

Nini Maoni yako kuhusu jinsi kampeni zinavyoendelea

Kuna malumbano mengi
5%
Hakuna ujumbe au mpango unaoniridhisha.
1%
Chama tawala kina ujumbe mzuri.
4%
Upinzani una ujumbe mzuri.
89%
 
Na msoma wasifu awepo na awe ameuandaa.....
 
Nini Maoni yako kuhusu jinsi kampeni zinavyoendelea

Kuna malumbano mengi
5%
Hakuna ujumbe au mpango unaoniridhisha.
1%
Chama tawala kina ujumbe mzuri.
4%
Upinzani una ujumbe mzuri.
89%



Hiyo hapo juu ni hali halisi ya sasa (10:51am) on 13 Oct.2010
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…