KWELI Kushiba sana usiku na kulala Chali huongeza nafasi ya kukabwa na Majinamizi

KWELI Kushiba sana usiku na kulala Chali huongeza nafasi ya kukabwa na Majinamizi

Taarifa hii imethibitika kuwa ya kweli baada ya kufanya tathmini ya kina
Hivi ni kweli kuwa kula chakula kingi wakati wa usiku pamoja na kulala chali huongeza nafasi ya kukabwa na majinamizi shingoni?

sleep-paralyss-istock-1174294433-1.jpg
 
Tunachokijua
Jinamizi la Usingizi kwa lugha ya kitaalam hufahamika kama Sleep Paralysis, ni kipindi cha mpito kinachoufanya mwili ukose udhibiti wa misuli. Hali hii inaweza kutokea muda mfupi baada ya kulala au kuamka.

Wakati wa tukio hili, mwili hutawaliwa na hisia mbaya, hofu na kupoteza uwezo wa kutumia viungo vya mwili kujinasua kwenye mtanziko wa mawazo hasi yanayokuwepo. Mathalani, mtu aliye kwenye hali hii anaweza huhisi kukabwa na kiumbe chenye nguvu kubwa kuliko yeye lakini huwa hana uwezo wowote wa kupambana au kukimbia.

Pia, unaweza kuwa macho lakini usiwe na uwezo wa kusimama, kuzungumza au kufungua macho.

Chanzo cha Jinamizi la usingizi
Sleep Paralysis ama Jinamizi la Usingizi huhusianishwa na mambo mengi ikiwemo wasiwasi, changamoto za kisaikolojia, kutokuwa na usingizi mzuri, matumizi ya pombe Pamoja na uwepo wa kumbukumbu ya matukio mabaya.

Pia, kwa mujibu wa Taasisi ya NHS, ulaji wa chakula kingi kabla ya kupumzika pamoja na kulalia mgongo (kulala chali) huongeza nafasi ya kutokea kwa jinamizi la usingizi.

Mbinu za kuepuka hali hii
Hadi sasa, hakuna tiba ya moja kwa moja inayoweza kutumika ili kuondoa changamoto hii. Hata hivyo, mbinu zifuatazo zinaweza kusaidia kuikabili;
  • Kutunza ratiba ya usingizi
  • Kutunza usafi wa chumba cha kulala pamoja na kutumia godoro zuri
  • Lala kwenye chumba kisicho na usumbufu wa mwanga mkali na kelele
  • Epuka kutazama TV ukiwa chumbani Pamoja na kusitisha matumizi ya vifaa vya kidigitali walau nusu saa kabla ya mud awa kulala.
Pia, wataalamu wa afya hushauri kutokula chakula kingi, kuvuta sigara au kunywa vinywaji vyenye caffeine muda mfupi kabla ya kwenda kulala ili kujiepusha na kutokea kwa hali hii.
Hivi ni kweli kuwa kukabwa na majinamizi shingoni husababishwa na kushiba sana haiku, kula muda umeenda na kulala chali?
Kitaalamu wanaita "sleep paralysis" hii hutokea mara chache na ina maelezo yake kitaalamu kama ifuatavyo.

Unapokuwa unataka kulala ,ukiwa sasa umejiweka kitandani bado usingizi haujakuchukua mwili huwa unazalisha paralysis hormone hii husaidia kuulinda mwili na mitikisiko isiyo na maana usiku mfano kurusha mikono ukiwa unaota hii inakukinga na ajali zisizo na maana pia inaufanya mwili uweze ku relax na ubongo ufanye kazi nzuri ya ku repair viungo kutokana na ufanyaji kazi wa siku nzima.

Kikawaida unapokuwa unaamka kabla hata ya kufungua macho (soma kuhusiana na circadian rythims) hormone hiyo ya paralysis huwa inaondolewa kwenye mwili ndani ya sekunde chache mno.

Sasa baadhi ya watu wanaweza kuamka kabla ya hormone hii kuondolewa kwenye mwili ndipo hapo unakuta sasa mwili unakuwa mzito akili na macho vinafanya kazi lakini mwili hausogei na unaanza kuona mambo ambayo hayapo pia.

Hivyo huwa haisababishwi na kushiba sana .
 
Kama umeshiba sana kile chakula ndiyo kina kukaba,usilale chali lalia mkono wa kulia.
 
Kitaalamu wanaita "sleep paralysis" hii hutokea mara chache na ina maelezo yake kitaalamu kama ifuatavyo.

Unapokuwa unataka kulala ,ukiwa sasa umejiweka kitandani bado usingizi haujakuchukua mwili huwa unazalisha paralysis hormone hii husaidia kuulinda mwili na mitikisiko isiyo na maana usiku mfano kurusha mikono ukiwa unaota hii inakukinga na ajali zisizo na maana pia inaufanya mwili uweze ku relax na ubongo ufanye kazi nzuri ya ku repair viungo kutokana na ufanyaji kazi wa siku nzima.

Kikawaida unapokuwa unaamka kabla hata ya kufungua macho (soma kuhusiana na circadian rythims) hormone hiyo ya paralysis huwa inaondolewa kwenye mwili ndani ya sekunde chache mno.

Sasa baadhi ya watu wanaweza kuamka kabla ya hormone hii kuondolewa kwenye mwili ndipo hapo unakuta sasa mwili unakuwa mzito akili na macho vinafanya kazi lakini mwili hausogei na unaanza kuona mambo ambayo hayapo pia.

Hivyo huwa haisababishwi na kushiba sana .
Wewe utakuwa unakula kidogo usiku.
 
Duh ni juzi tu hali hii ilinitokea nilipiga kelele sana lakini wapi nikanyanyua mkono lakini wapi nikabaki kusema kimoyo moyo kwa jina la yesu....kwa jina la yesu hali hii ikitokea unapaswa ufanye nini ilikuiondoa na je inaweza kuduma takribani kwa dakika ngapi au masaa mapangi.Ahsnte
 
Duh ni juzi tu hali hii ilinitokea nilipiga kelele sana lakini wapi nikanyanyua mkono lakini wapi nikabaki kusema kimoyo moyo kwa jina la yesu....kwa jina la yesu hali hii ikitokea unapaswa ufanye nini ilikuiondoa na je inaweza kuduma takribani kwa dakika ngapi au masaa mapangi.Ahsnte
Mkuu, lipo kati ya haya lilikuwa sahihi?
• Ulilala chali
• Ulikula sana na kulala muda huo huo
• Ulilala muda umeenda tofauti na siku nyingine
• Una dalili za ugonjwa ma malaria, au unaumwa na mbu mara kwa mara

Funguka mkuu usaidiwe
 
Hivi ni kweli kuwa kula chakula kingi wakati wa usiku pamoja na kulala chali huongeza nafasi ya kukabwa na majinamizi shingoni?

Pia kuna matatizo ya kiafya kama:
1: Matatizo ya moyo
2: GERD
3: Unene uliopitiliza
4: Matatizo y mapafu (mfumo wa upumuaji).
5: Matumizi ya dawa za usingizi

NB: Msingi mkuu uko kwenye mifumo ya mwili kutopat oksijeni ya kutosha hasa ubongo.
 
Kitaalamu wanaita "sleep paralysis" hii hutokea mara chache na ina maelezo yake kitaalamu kama ifuatavyo.

Unapokuwa unataka kulala ,ukiwa sasa umejiweka kitandani bado usingizi haujakuchukua mwili huwa unazalisha paralysis hormone hii husaidia kuulinda mwili na mitikisiko isiyo na maana usiku mfano kurusha mikono ukiwa unaota hii inakukinga na ajali zisizo na maana pia inaufanya mwili uweze ku relax na ubongo ufanye kazi nzuri ya ku repair viungo kutokana na ufanyaji kazi wa siku nzima.

Kikawaida unapokuwa unaamka kabla hata ya kufungua macho (soma kuhusiana na circadian rythims) hormone hiyo ya paralysis huwa inaondolewa kwenye mwili ndani ya sekunde chache mno.

Sasa baadhi ya watu wanaweza kuamka kabla ya hormone hii kuondolewa kwenye mwili ndipo hapo unakuta sasa mwili unakuwa mzito akili na macho vinafanya kazi lakini mwili hausogei na unaanza kuona mambo ambayo hayapo pia.

Hivyo huwa haisababishwi na kushiba sana .
Sio kweli jinamizi lipo??
 
Back
Top Bottom