#COVID19 Kushuka athari za Corona India kwawashangaza Wataalam wa Afya

#COVID19 Kushuka athari za Corona India kwawashangaza Wataalam wa Afya

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Imeelezwa kuwa athari za corona nchini India ikiwemo idadi ya maambukizi na vifo imeshuka kwa kiwango cha juu bila kupatiwa maelezo ya kitaalamu.

Awali ugonjwa huu ulipoanza hapo mwaka jana ilikisiwa kuwa taifa hilo la pili kwa idadi ya watu duniani lingeathirika zaidi.Kuna kipindi maambukizi kwa waliopimwa ilifika watu laki moja kwa siku lakini kwa sasa ni watu elfu 10 tu na vifu vimepungua sana miongoni mwa walioambukizika.

Baadhi ya wataalamu wametaja hali hiyo huenda ni mafanikio ya uvaaji barakoa ambao umefanywa kuwa ni lazima kwenye miji mingi ya nchi hiyo.Hata hivyo hoja hiyo imekinzana na ukweli kuwa utekelezaji wake katika baadhi ya miji ni wenye kulegalega wakati kushuka kwa maambukizi hayo kuko karibu sawa kwenye miji yote.

Hoja nyengine imesema kuwa kushuka kwa athari za maradhi hayo ni kutokana na kuwa idadi kubwa ya wananchi wa India hasa vijijini wanafanya kazi zao maeneo ya wazi na wanalala majumba ya wazi.

Maelezo mengine ya baadhi ya watafiti ni kuwa kwa vile watu wengi tayari wamepata maradhi ya corona na kupona basi kumepatikana kinga za vikundi dhidi ya maambukizi mapya.

Wengine wamesema hali hiyo inatokana na kuwa wananchi wa nchi hiyo tangu wanapokuwa wadogo huwa wanaugua maradhi mengi ya maambukizi kama vile kifua kikuu na hivyo miili yao huwa imejenga kinga ya ndani kwa ndani ambapo wadudu wa corona wanapata shida kupenya kikamilifu kwenye mifumo yao.

Kubwa zaidi kuhusu hali hii ya janga la corona nchini humo imetokea hata kabla ya kuanza kutumika chanjo mwezi uliopita ambazo mpaka muda huu zimewafikia watu wachache sana kati ya idadi ya watu wote wa nchi hiyo wanaotakiwa kupewa chanjo.

Ikumbukwe kuwa taifa la India ndilo linaloongoza duniani kwa matumizi ya vyakula asilia na viungo vikali katika vyakula vyao.

Chanzo: India's dramatic fall in virus cases leaves experts stumped
 
Wapi source?

Mi Lumumba kwa kufariji wajinga ipo kazi.

Kama kuna hadithi ya vyakula vya asili na usugu wa miili kwa suluba za wagonjwa. Umejiuliza kama athari zimeshuka ni vipi ziliwahi kuwa juu?

Au kama yameshuka kweli huyo kirusi amekumbuka kuwa mapema alikuwa kakosea njia? Sasa ndiyo kakumbuka na kushika adabu yake?

Kamwambieni pole pole - holaaa!
 
Ndugu zangu corona sasa basi, dawa imepatikana India. Baada ya kufiwa na ndugu zake wengi kwa corona, Dr. Zinth akaweka kuhudi kubwa kwenye dawa za asili. Akachukua binzali, mchaichai, tangawizi na maziwa na kumnywesha bibi yake ambae alikua anapumua kwa tabu. Baada ya siku 3 yule bibi akawa anapumua kawaida na baada ya siku 3 zingine akawa amepona kabisa. Dr. Zinth akaanza kuwapa watu wa kijijini kwao na wote wakapona. Kuanzia tarehe 11 Serekali ya India imechukua hiyo dawa na kuwanywesha wagonjwa wa corona. Hadi sasa wagonjwa 1200 wamepona. Unangoja nini? Chukua huo mchanganyiko na anza kunywa ili uokoe maisha yako na ndugu zako.
 

Chanjoooooo

Imeelezwa kuwa athari za corona nchini Indiaikiwemo idadi ya maambukizi na vifo imeshuka kwa kiwango cha juu bila kupatiwa maelezo ya kitaalamu.


Awali ugonjwa huu ulipoanza hapo mwaka jana ilikisiwa kuwa taifa hilo la pili kwa idadi ya watu duniani lingeathirika zaidi.Kuna kipindi maambukizi kwa waliopimwa ilifika watu laki moja kwa siku lakini kwa sasa ni watu elfu 10 tu na vifu vimepungua sana miongoni mwa walioambukizika.

Baadhi ya wataalamu wametaja hali hiyo huenda ni mafanikio ya uvaaji barakoa ambao umefanywa kuwa ni lazima kwenye miji mingi ya nchi hiyo.Hata hivyo hoja hiyo imekinzana na ukweli kuwa utekelezaji wake katika baadhi ya miji ni wenye kulegalega wakati kushuka kwa maambukizi hayo kuko karibu sawa kwenye miji yote.

Hoja nyengine imesema kuwa kushuka kwa athari za maradhi hayo ni kutokana na kuwa idadi kubwa ya wananchi wa India hasa vijijini wanafanya kazi zao maeneo ya wazi na wanalala majumba ya wazi.

Maelezo mengine ya baadhi ya watafiti ni kuwa kwa vile watu wengi tayari wamepata maradhi ya corona na kupona basi kumepatikana kinga za vikundi dhidi ya maambukizi mapya.

Wengine wamesema hali hiyo inatokana na kuwa wananchi wa nchi hiyo tangu wanapokuwa wadogo huwa wanaugua maradhi mengi ya maambukizi kama vile kifua kikuu na hivyo miili yao huwa imejenga kinga ya ndani kwa ndani ambapo wadudu wa corona wanapata shida kupenya kikamilifu kwenye mifumo yao.

Kubwa zaidi kuhusu hali hii ya janga la corona nchini humo imetokea hata kabla ya kuanza kutumika chanjo mwezi uliopita ambazo mpaka muda huu zimewafikia watu wachache sana kati ya idadi ya watu wote wa nchi hiyo wanaotakiwa kupewa chanjo.

Ikumbukwe kuwa taifa la India ndilo linaloongoza duniani kwa matumizi ya vyakula asilia na viungo vikali katika vyakula vyao.

Chanzo: India's dramatic fall in virus cases leaves experts stumped
 

Imeelezwa kuwa athari za corona nchini Indiaikiwemo idadi ya maambukizi na vifo imeshuka kwa kiwango cha juu bila kupatiwa maelezo ya kitaalamu.


Awali ugonjwa huu ulipoanza hapo mwaka jana ilikisiwa kuwa taifa hilo la pili kwa idadi ya watu duniani lingeathirika zaidi.Kuna kipindi maambukizi kwa waliopimwa ilifika watu laki moja kwa siku lakini kwa sasa ni watu elfu 10 tu na vifu vimepungua sana miongoni mwa walioambukizika.

Baadhi ya wataalamu wametaja hali hiyo huenda ni mafanikio ya uvaaji barakoa ambao umefanywa kuwa ni lazima kwenye miji mingi ya nchi hiyo.Hata hivyo hoja hiyo imekinzana na ukweli kuwa utekelezaji wake katika baadhi ya miji ni wenye kulegalega wakati kushuka kwa maambukizi hayo kuko karibu sawa kwenye miji yote.

Hoja nyengine imesema kuwa kushuka kwa athari za maradhi hayo ni kutokana na kuwa idadi kubwa ya wananchi wa India hasa vijijini wanafanya kazi zao maeneo ya wazi na wanalala majumba ya wazi.

Maelezo mengine ya baadhi ya watafiti ni kuwa kwa vile watu wengi tayari wamepata maradhi ya corona na kupona basi kumepatikana kinga za vikundi dhidi ya maambukizi mapya.

Wengine wamesema hali hiyo inatokana na kuwa wananchi wa nchi hiyo tangu wanapokuwa wadogo huwa wanaugua maradhi mengi ya maambukizi kama vile kifua kikuu na hivyo miili yao huwa imejenga kinga ya ndani kwa ndani ambapo wadudu wa corona wanapata shida kupenya kikamilifu kwenye mifumo yao.

Kubwa zaidi kuhusu hali hii ya janga la corona nchini humo imetokea hata kabla ya kuanza kutumika chanjo mwezi uliopita ambazo mpaka muda huu zimewafikia watu wachache sana kati ya idadi ya watu wote wa nchi hiyo wanaotakiwa kupewa chanjo.

Ikumbukwe kuwa taifa la India ndilo linaloongoza duniani kwa matumizi ya vyakula asilia na viungo vikali katika vyakula vyao.

Chanzo: India's dramatic fall in virus cases leaves experts stumped
 
Ndugu zangu corona sasa basi, dawa imepatikana India. Baada ya kufiwa na ndugu zake wengi kwa corona, Dr. Zinth akaweka kuhudi kubwa kwenye dawa za asili. Akachukua binzali, mchaichai, tangawizi na maziwa na kumnywesha bibi yake ambae alikua anapumua kwa tabu. Baada ya siku 3 yule bibi akawa anapumua kawaida na baada ya siku 3 zingine akawa amepona kabisa. Dr. Zinth akaanza kuwapa watu wa kijijini kwao na wote wakapona. Kuanzia tarehe 11 Serekali ya India imechukua hiyo dawa na kuwanywesha wagonjwa wa corona. Hadi sasa wagonjwa 1200 wamepona. Unangoja nini? Chukua huo mchanganyiko na anza kunywa ili uokoe maisha yako na ndugu zako.
Wale wanaosubiri chanjo za pfizer nawasubiri wengine tumewekeza kwenye michanganyiko ya mititshamba zaidi.
 
Wabongo mnajifanya wajanja hamfuati masharti...madhara yake mnayaona
 
Wabongo mnajifanya wajanja hamfuati masharti...madhara yake mnayaona
Hatuna ujanja wowote na pia hakuna mjanja mbele ya kifo.Kilichomuhimu ni kufanya kilicho dhahiri na vyengine turidhike na hukumu ya Mwenyezi Mungu. Wale wanaotaka kulazimisha masharti magumu na dawa ngumu kabla ya zile za rahisi watachangia kuharibu mifumo ya maisha ambayo tangu hapo ni migumu.
India maambukizi yameshuka sababu hii hapa


Hiyo picha hapo juu ni ya zamani na hawakuwacha kuingia misikitini kwa ajili ya corona.
Hatuna ujanja wowote na pia hakuna mjanja mbele ya kifo.Kilichomuhimu ni kufanya kilicho dhahiri na vyengine turidhike na hukumu ya Mwenyezi Mungu. Wale wanaotaka kulazimisha masharti magumu na dawa ngumu kabla ya zile za rahisi watachangia kuharibu mifumo ya maisha ambayo tangu hapo ni migumu.
 
Katika nchi kubwa kama ile ya pila kwa idadi ya watu duniani waliokufa ni laki moja na nusu tu.Na hapo takwimu zaweza kuwa zimechanganyika na vifo vya sababu nyengine.
 
Imeelezwa kuwa athari za corona nchini India ikiwemo idadi ya maambukizi na vifo imeshuka kwa kiwango cha juu bila kupatiwa maelezo ya kitaalamu.

Awali ugonjwa huu ulipoanza hapo mwaka jana ilikisiwa kuwa taifa hilo la pili kwa idadi ya watu duniani lingeathirika zaidi.Kuna kipindi maambukizi kwa waliopimwa ilifika watu laki moja kwa siku lakini kwa sasa ni watu elfu 10 tu na vifu vimepungua sana miongoni mwa walioambukizika.

Baadhi ya wataalamu wametaja hali hiyo huenda ni mafanikio ya uvaaji barakoa ambao umefanywa kuwa ni lazima kwenye miji mingi ya nchi hiyo.Hata hivyo hoja hiyo imekinzana na ukweli kuwa utekelezaji wake katika baadhi ya miji ni wenye kulegalega wakati kushuka kwa maambukizi hayo kuko karibu sawa kwenye miji yote.

Hoja nyengine imesema kuwa kushuka kwa athari za maradhi hayo ni kutokana na kuwa idadi kubwa ya wananchi wa India hasa vijijini wanafanya kazi zao maeneo ya wazi na wanalala majumba ya wazi.

Maelezo mengine ya baadhi ya watafiti ni kuwa kwa vile watu wengi tayari wamepata maradhi ya corona na kupona basi kumepatikana kinga za vikundi dhidi ya maambukizi mapya.

Wengine wamesema hali hiyo inatokana na kuwa wananchi wa nchi hiyo tangu wanapokuwa wadogo huwa wanaugua maradhi mengi ya maambukizi kama vile kifua kikuu na hivyo miili yao huwa imejenga kinga ya ndani kwa ndani ambapo wadudu wa corona wanapata shida kupenya kikamilifu kwenye mifumo yao.

Kubwa zaidi kuhusu hali hii ya janga la corona nchini humo imetokea hata kabla ya kuanza kutumika chanjo mwezi uliopita ambazo mpaka muda huu zimewafikia watu wachache sana kati ya idadi ya watu wote wa nchi hiyo wanaotakiwa kupewa chanjo.

Ikumbukwe kuwa taifa la India ndilo linaloongoza duniani kwa matumizi ya vyakula asilia na viungo vikali katika vyakula vyao.

Chanzo: India's dramatic fall in virus cases leaves experts stumped
Wanaficha data kama meko
 
Back
Top Bottom