Duh, hili nilikuwa silijui;
Mwalim anaetumikia tuition centre zaidi kuliko shule huyo ni mzembe binafsi, maana kunawalim hawana hizo centre na watoto wanafeli, watoto kufeli masomo ya sayansi kwa hapa tz ni suala la saikolojia.
Pia masomo haya yanahitaji kujitolea kwa mwalim na mwanafunzi maana si mchezo,
Kitu kingine ni kwamba masomo haya yanahitaji constant learning la sivyo unasahau kila kitu, je ni wangapi wanapenda kujisomea?
Pia masomo haya yanahitaji resource nyingi tu hasa vitabu na bahati mbaya vitabu vya masomo ya sayansi vinauzwa bei ghari sana, je nani anaweza kununua? (mfano Abbot, Lambert, nelkon nk)
si hayo tu na sababu nyingine nyingi, mfano idadi ya hao walimu na mikondo anayotakiwa kufundisha per kidato (unakuta walimu wa somo moja wanaweza wakawa wawili form 1-4 na kila kidato kina mikondo zaidi ya miwili, je wataweza na hata kama wakiweza, je ni kwa mshahara upi?
Kumbuka siku hizi walimu tunasema "FUNDISHA KADRI UNAVYOLIPWA-(FUKU)"