Kushuka Kwa Kiwango Cha Elimu Nchini Serikali kurudisha Viboko Mashuleni

Kushuka Kwa Kiwango Cha Elimu Nchini Serikali kurudisha Viboko Mashuleni

Power G

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2011
Posts
3,884
Reaction score
1,198
Naibu waziri wa elimu Mh. Mlugo amesema serikali iko katika mkakati wa kuruhusu viboko mashuleni na kupiga marufuku simu kwa wanafunzi wawapo mashuleni (Startv saa 2 usiku). Je hilo litakuwa suluhisho la kushuka kwa kiwango cha elimu nchini??
 
Naibu waziri wa elimu Mh. Mlugo amesema serikali iko katika mkakati wa kuruhusu viboko mashuleni na kupiga marufuku simu kwa wanafunzi wawapo mashuleni (Startv saa 2 usiku). Je hilo litakuwa suluhisho la kushuka kwa kiwango cha elimu nchini??
Siyo siri kwamba kushuka kwa kiwanja cha elimu mashuleni kunachangiwa pia na kushuka kwa kasi sana kwa nidhamu ya wanafunzi. Wanafunzi enzi hizi hawaadhibiwi kwa viboko baada ya serikali kufuta adhabu ya viboko mashuleni. Sisi tuliosoma zamani nidhamu ilikuwa inadumishwa na viboko na wanafunzi walikuwa hawana mtetezi yeyote wa kuwatetea kutokana na adhabu hiyo. Kiwango cha nidhamu na elimu enzi hizo kilikuwa cha juu sana ukilinganisha na sasa. Hivyo kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, leo namuunga mkono mlugo kwa hilo la viboko na la kupiga marufuku matumizi ya simu kwa wanafunzi.
 
wakuu nkamba sasa hvi kila jambo la kiutendaj linasiasa ndan yake,Mtoto leo si mali ya jamii mchape uone ila wakirudsha!
 
Fimbo muhimu sana, na hizo simu kwa kweli wapige marufuku.Hawa watoto wa dot com wamejisahau sana
 
Shule zenyewe wanazofeli wanafunzi wengi hata mavavi ya shule hawana, wazazi wanaangaika mchana usiku kutafuta pesa ya kusomesha watoto wao. Watoto nao wanawasaidia muda wa kusoma kwa shida utaisha?

Muhimu zaidi eti viboko, hao walimu watachapwa wao na wanafunzi plus wazazi.

Walimu hawafundishi mashuleni wangeenda kuuliza wanafunzi au kuvizia kuona matuition yalivyo mengi na bado hawawafundishi wanafeli. Wanafunzi wanashindwa kulipia ada na mavavi walimu wanataka pesa ya tuition nani anauwezo huo as wengi maisha magumu.

Kweli huyo waziri hafikiri kabisa, na sheria iwekwe mwalimu akimchapa mtoto au kumpa adhabu ya mateso na kumuaribu akili kisaikolojia basi aende mahakamani.

Ak*me kabisa, akachape wanae kwanzam
 
Jamani na hii http://shuledirect.co.tz iko vipi? najua inamilikiwa na Faraja Nyalandu na anasema walimu wake wote ni wanashahada ya elimu na wana experience ya atleast 5 years.

Je mwenye nayo anafaidika vipi?
Na wanafunzi wanafaidika vipi? maana asilimia 75 ya wanafunzi hawana elimu au access ya computer na internet.
 
Walimu wanapata faida gani kwa kuwachapa wanafunzi?
 
makongo,jitegemee high school ni shule ambazo walimu wake wanachapa sana wanafunzi mbona matokeo yao ni mabaya.
tuache siasa kwenye mambo ya msingi.sababu zilizofelisha wanafunzi mnazifahamu na siyo hizo za kipuuzi alizotoa mh.mullugo.
 
Naibu waziri wa elimu Mh. Mlugo amesema serikali iko katika mkakati wa kuruhusu viboko mashuleni na kupiga marufuku simu kwa wanafunzi wawapo mashuleni (Startv saa 2 usiku). Je hilo litakuwa suluhisho la kushuka kwa kiwango cha elimu nchini??

Sio suluhisho.WAWAKUMBUKE WALIMU WAO WA KUUNGAUNGA a.k.a VODA FASTA ndio CHANZO KIKUU CHA KUFELI kwa mf Mtu huyo kwa kipindi cha miaka 10 anarudia mtihan wa kidato cha 4 na kila baada ya miaka 3 ANABAHATISHA ka C KAMOJA tu! HALAFU eti HUYO2 TENA NDO UNAMPA KAZI YA UALIMU HALAFU UNATEGEMEA WANAFUNZI WAFAULU! Kufeli kwa wanafunzi SABABU NI WALIMU PASIPO ELIMU
 
your deviating from the mean mr Waziri, Je waalimu tutapewa allowance za kutoa adhabu? maana ukipiga mtu nawe pia unaumia
 
Tumeingia kichwa kichwa kweli bila hata kujifikirisha kwani hivyo viboko viliwahi kufutwa lini mashuleni au ni kwa baadhi ya mikoa?. Mie nimechunguza shule za msingi wana chapwa kama kawaida na hz shule za kata viboko havikuwahi kufutwa.
 
Hili nalo jambo!

aliye suggest kwamba viboko virudishwe mashuleni nadhani alikuwa usingizini,badala ya kuongezwa kwa vifaa vya kufundishia mashuleni ili wanafunzi wafaulu,yy anataka fimbo ndo ziongezwe !kweli kama fimbo inaongeza akili kijana wangu angekuwa na dozi!
 
Ninapinga maamuzi ya kurudisha fimbo rasmi ingawa ukweli zilikuwa zikiendelea kama kawa!Sababu ni mbili tu za msingi.
1.Kutokana na matatizo ya serikali kupuuza madai ya walimu,walimu wengi wanaishi kwa stress na wakikabiliwa na matatizo lukuki ya kisaikolojia.Hivyo mtoto anaweza kufanya kosa hata dogo tu akapata kichapo cha mbwa mwizi!ama akaadhibiwa kwa makosa ya mtu mwingine.Mfano mie niliwahi kuadhibiwa vikali kwa kosa la kuchelewa shule mchana nikiwa nimetoka nyumbani ambako hata chakula sikuwa nimekula baada ya kukuta chakula hakijawa tayari,niliona nirudi tu shule,ndipo nilipokutana na kichapo kikali nikiwa nimeshika masikio!alitokea mwl mmoja akaingilia kati na baadae nikaja kujua kumbe yule mwl Mkuu aliyeniadhibu,alikuwa na ugomvi binafsi na baba mzazi ambaye eti alimchukulia demu wake!kichapo nikachezea mie!
2.Mtoto anaweza kuwa mtukutu kutokana na migogoro ya ndoa na ikamchanganya kisaikolojia.Watoto kama hawa ni wengi sana.Badala ya kuwasaidia,itakuwa kama kuwafanyia ukatili mara ya pili!most teachers are bitter kutokana na maisha wanayopitia!Nasikitika watu wanasoma sayansi ya jamii lakini wako kimya tu na hawapigii kelele maamuzi haya mabaya.Watoto wamefanyiwa ukatili mwingi ni nani mtetezi wao?Tafakari,kisha chukua hatua!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom