Wakati Trump amesitisha kugharamia shughuli nyingi ambazo zilikuwa zinafanywa na USAID ni wakati wa kujiuliza kwa umakini kitu gani ni muhimu. Hii pesa ilikuwa inasaidia kutoa dawa wa wagojwa wa ukimwi na elimu huko kusini na kusaidia lishe kwa zile kaya ambazo watoto wana dalili za mtapia mlo
Lakini cha kushangaza ni serikali hiyo hiyo inayo saidiwa dawa na kuokoa maisha kwa upande mmoja ndiyo tena inatumia milioni 400 kununua gari moja la wanasiasa ambao kazi zao hazieleweki umuhimu wake mfano wakuu wa wilaya. Je Watanzania tunaona ni muhimu kununua magari ya milioni mia nne wakati tungeweza kupata magari ya milioni 100 mazuri?.
Je kwanini tusingegeuza na kuomba msaada wa magari na kutumia hiyo pesa kusaidia afya za Watanzania wenzetu ili hata msaada ukikatwa ni magari tu badala ya dawa ambazo zinaisha muda na zinahitaji kununuliwa mara kwa mara. Je ni kipi muhimu zaidi?. Tatizo leo kila kitu tukihoji hapa hata cha maslahi tunaitwa Chadema! au tunashuturiwa kwamba hatupendi serikali. Ukweli ni kwamba tunapenda ndugu zetu na ni wakati wa kuacha mazoea na kuanza kuweka nchi mbele. Hivi tunaendaje Marekani kuwaeleza walipa kodi wao kwamba viongozi tena wa ngazi za chini wanaishi kifalme wakati badala ya kununua dawa na kusaidia jamii zao badala yake pesa inaenda kwenye magari na vitu vya kianasa kama kulipa wasanii mabilioni kumuimbia Raisi birthday au mambo ya kisiasa.
zitto junior
Pascal Mayalla
ChoiceVariable
Lakini cha kushangaza ni serikali hiyo hiyo inayo saidiwa dawa na kuokoa maisha kwa upande mmoja ndiyo tena inatumia milioni 400 kununua gari moja la wanasiasa ambao kazi zao hazieleweki umuhimu wake mfano wakuu wa wilaya. Je Watanzania tunaona ni muhimu kununua magari ya milioni mia nne wakati tungeweza kupata magari ya milioni 100 mazuri?.
Je kwanini tusingegeuza na kuomba msaada wa magari na kutumia hiyo pesa kusaidia afya za Watanzania wenzetu ili hata msaada ukikatwa ni magari tu badala ya dawa ambazo zinaisha muda na zinahitaji kununuliwa mara kwa mara. Je ni kipi muhimu zaidi?. Tatizo leo kila kitu tukihoji hapa hata cha maslahi tunaitwa Chadema! au tunashuturiwa kwamba hatupendi serikali. Ukweli ni kwamba tunapenda ndugu zetu na ni wakati wa kuacha mazoea na kuanza kuweka nchi mbele. Hivi tunaendaje Marekani kuwaeleza walipa kodi wao kwamba viongozi tena wa ngazi za chini wanaishi kifalme wakati badala ya kununua dawa na kusaidia jamii zao badala yake pesa inaenda kwenye magari na vitu vya kianasa kama kulipa wasanii mabilioni kumuimbia Raisi birthday au mambo ya kisiasa.
zitto junior
Pascal Mayalla
ChoiceVariable