Kusubiri kushindwa kwa Rais Magufuli au serikali ni Kamari mbaya sana. Serikali ya awamu ya tano ni itashinda kwa sababu…

Kusubiri kushindwa kwa Rais Magufuli au serikali ni Kamari mbaya sana. Serikali ya awamu ya tano ni itashinda kwa sababu…

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Tangu Zitto Kabwe ajitoe ufahamu wa kuandika barua WB ili mkopo kwa ajili ya elimu tulioomba tusipewe, baadhi ya watu wameanza kuujadili usaliti wa Zitto Kabwe kwa Taifa lake kama uzalendo na yeye kujiona kafanya kitendo cha kishujaa kwa watanzania maskini.

Mashaka ya wengi ni kwa nini Zitto kaamua kuwa sehemu ya unyonyaji badala ya kutumia kalamu yake kulisaidia taifa lake? Zitto anajulikana kwa sifa moja kubwa nayo ni kusaka umaarufu na ukuu kwa gharama yoyote bila kujali athari kwa watu wake, kwa taifa lake na kila mmoja mwenye mapenzi mema, rejea cheo alichonacho ACT cha kiongozi mkuu wa chama ambacho kinaonesha ni mtu mwenye utu na tamaa ya ukuu na mamlaka yasiyo na mipaka.

Ninaamini Zitto ni moja ya watu wanaosubiri anguko la Rais Magufuli au serikali kwa sababu anaamini haitaji kuwa kiongozi mkuu wa chama bali kuweza kuwa hata kiongozi mkuu wa nchi ambaye hatotamani katiba na sheria imwambie nini cha kufanya Zaidi ya utashi wake binafsi. Namuona kama mtu mwenye uchu wa kutawala na si kuongoza, amekosa sifa za kuwa kiongozi Zaidi ana sifa zote za kuwa mtawala ambaye sheria na katiba ataiweka pembeni kama akipata mamlaka makubwa Zaidi.

Zitto na wapinzani wengine wanashindwa kujua kwamba watanzania kwa umoja wetu bila kujali itikadi, dini, Imani, kabila na rangi zetu tunamuona Rais Magufuli katika jicho la uchapakazi, uadilifu, uzalendo na matumaini makubwa kwa Tanzania ya kesho. Tanzania ya ndoto zetu na hatutaacha kuwa pamoja naye kwa sababu ushindi wake ni ushindi wetu na kushindwa kwake ni kushindwa kwetu, hatutakuwa tayari kuona akishindwa na hizi ndio sababu za kushinda kwa serikali ya awamu ya tano:

  • Rais Magufuli anamtanguliza Mungu popote
Imani zetu zinaamini katika uweza upitayo uwezo wote naye ni Mungu. Kitendo cha Rais Maguguli kumtanguliza Mungu katika kila jambo ni kuamini kuwa Mungu ni muweza wa yote na hakuna jambo lolote linalomshinda, hivyo siamini seikali ya Rais Magufuli itashindwa kama anamtanguliza Mungu katika maamuzi yake. Wanaotaka Rais Magufuli ashindwe ni kutaka Mungu ashindwe, hakika nawaambieni anguko lenu ni kubwa kuliko hilo la Rais Magufuli mnalolisubiri.

  • Wananchi tupo naye
Nchi yetu ni ya kidemokrasia hivyo uongozi uliopo umewekwa na watu kwa ridhaa yao wenyewe na kwa sababu ni serikali iliyochaguliwa na watu basi serikali inafanya yale waliyoahidi kwa watu wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu kupitia ilani ya uchaguzi. Kwa kuwa sisi ndio tunaichagua serikali basi na sisi ndio wenye uamuzi wa kumkataa kiongozi au serikali kwa ujumla. Yote yali/nayofanywa na Rais Magufuli na serikali yake yamepata kibali kutoka kwetu wanachi. Kusubiri anguko la seikali yenye kujali na kuwapenda wananchi wake kama serikali ya awamu ya tano ni kucheza Kamari hatari sana.

  • CCM imekuwa imara sana
Nakiri kusema kwa miaka michache ya uongozi wake kama mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli amekiunda upya chama cha mapinduzi na imekuwa imara sana. Ni katika kipindi hiki kila mwanaCCM anajivunia kuwa CCM , ni kipindi hiki sare za CCM zinapendwa kuliko sare ya chama kingine chochote katika JMT, ni katika kipindi hiki uwajibikaji wa serikali kwa chama umekuwa marudufu, ni katika kipindi CCM inazungumziwa kama chama chenye kubeba maono ya muda mrefu ya taifa hili na ni katika kipindi hiki CCM imerejesha matumaini ya watanzania juu ya hatima yao kiuongozi, hatima ya rasilimali zao na hatima katika uchumi wao. CCM ya namna hii ni ngumu sana kuanguka na CCM ya namna hii ni tegemeo kubwa la Rais Magufuli katika ujenzi wan chi yetu hivyo kusubiri anguko la serikali au Rais Magufuli chini ya CCM hii ni kucheza Kamari hatari

  • Tishio la maadui wa kupora rasilimali zetu
Baada ya Rais Magufuli kuonesha nia ya dhati ya kudhibiti unyonyaji na uporaji wa rasilimali zetu, kumekuwa na matishio na mazuio mbalimbali ambayo wananchi hatukubaliani nayo. Kutokana na matishio na mazuio hayo, wananchi wametambua dhamira aliyonayo Rais wetu ni ya kweli juu ya kulinda rasilimali zetu hivyo tunaamini vita aliyoanznisha Rais wetu ya kulinda na kutetea rasilimali zetu inatuhitaji sisi wananchi kuiunga mkono hivyo tumeamua kuungana na Rais wetu asishindwe. Ushindi wake ni wetu sote.
 
Back
Top Bottom