Uchaguzi 2020 Kususia Bunge la Bajeti kunawanyima kura Upinzani

Uchaguzi 2020 Kususia Bunge la Bajeti kunawanyima kura Upinzani

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Wakati Taifa limeilungana kupambana na shambulio la COVID-19, vyama vya upinzani nchini wakiongozwa na CHADEMA na ACT walisusia Bunge la Bajeti kwa kisingizio wanajiweka karantini dhidi ya CORONA

Ikumbukwe kwamba viongozi na wabunge wa vyama hivyo walianzisha kampeni ya kushambulia juhudi za serikali na umma za kupambana na kuenea kwa maambukizi hayo. Wafuasi wao ndani na nje ya nchi walisimama kidete kuishambulia serikali hasa wakielekeza mashambulizi kwa rais JPM pale alipoliomba Taifa kuingia katika maombi ya siku tatu kuomba Mungu aingilie kati na kulilinda taifa dhidi ya janga la COVID 19.

Freeman Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa CHADEMA na kiiongozi wa kambi ya upinzani Bungeni alitangaza mgomo wa Bunge na hatimaye wabunge kususia Bunge la Bajeti. Hata walipobembelezwa walijibu kwa kiburi na jeuri huku wakijiaminisha kwamba wabunge wa CCM watakufa kwa mamia kutokana na maambukizi ya Corona.

Endapo Bunge liingeingia mtego wa CHADEMA kujiweka karantini ilihali hakukuwepo na tishio dhahiri la Corona ina maana bajeti ya 2020/2021 isingepitishwa na leo tusingekuwepo na uchaguzi kwa sababu ya COROna.

1. Je kuna haja gani ya kuwaamini vyama vya upinzani ambavyo kutwa wanahangaika kuibua mitafaruku na taharuki kwenye Taifa letu,

2. CHADEMA wana uhalali gani kuomba kura zetu wakati tunajua walitukimbia wakati wa shida?

3. Mgombea wao wa urais ameonyesha dharau ya hali ya juu kwa mahakama baada ya kutohudhuria ktk kesi yake na kuidanganya kwamba anajiweka karantini ilihali alikuwa anashiriki public gatherings bila hata kuvaa barakoa na social distancing.

4. ACT kupitia kiongozi wao Zitto alijitahidi sana kuiambia dunia kwamba serikali ya Tanzania hususani JPM wanaficha taarifa za Corona na wagonjwa wanakufa hovyo mitaani.

Kwa yote hayo na mengine, vyama vya upinzani wanakosa uhalali wa kushika usukani wa maongozi ya nchi yetu.

Wananchi wanaenda kuonyesha mshikamano wao kwa Magufuli na CCM kupitia sanduku la kura hapo Oktoba 28.

Wakatabahu
Msanii JF
 
Wapinzani hawawezi kunyimwa kura na wananchi, ndio maana CCM inatumia NEC kuwaengua maana wanajua hakuna mbunge wa ccm haiwezi kushinda bila kubebwa na NEC.
 
Sisi huku kwetu kura zetu zote ni kwa hao upinzani.Mbona hilo bunge la bajeti lilijaa mipasho,vijembe,kugonga meza na kujipendekeza tu.
 
Wapinzani hawawezi kunyimwa kura na wananchi, ndio maana ccm inatumia NEC kuwaengua maana wanajua hakuna mbunge wa ccm haiwezi kushinda bila kubebwa na nec
Fanya utafiti kidogo utapata jibu.

Upinzani ni wasaliti na hawana uzalendo
 
Fanya utafiti kidogo utapata jibu.

Upinzani ni wasaliti na hawana uzalendo
Mzalendo ni yule aliye waagiza watu wampige risasi Lissu na kuwaondoa askari wa getini pamoja na kuzuia wabunge wasiende kumuangalia Lisu na kumvua ubunge lissu na kumzuia asitibiwe ili Lissu afe.

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Mzalendo ni yule aliye waagiza watu wampige risasi lisu na kuwaondoa askari wa getini pamoja na kuzuia wabunge wasiende kumuangalia lisu na kumvua ubunge lisu na kumzuia asitibiwe ili lisu afe

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
Unaongea kama mlevi wa mnazi tena mchana jua kali.

Mgonjwa wenu wa akili anavyojidhalilisha majukwaani kuwa aliamriwa auawe na nyie mnaitikia kinyumbu ni dalili mmeshakata tamaa ya huu uchaguzi.
 
Umesahau kuandika namba za simu , hivi nyinyi mataga mnafikiri watanzania Ni wajinga kiasi hicho? Nchi imeongozwa na CCM miaka 59 hamna mlichofanya watu wanaelewa vizuri sana. Haya nyie mliokuwemo bungeni ndio mmefanya nini? Kuna bajeti ya wizara yoyote toka 2016 unaweza kuitaja hapa imetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 35? Ipo?
 
Wanajua Oktoba hali ni ngumu, sasa wanapambania kupata ruzuku

Post yako namba, watanzania walikuwa wanafuatilia bunge la Ana Makinda, sio hili la gizani kama wachawi. Kwa maneno marahisi watanzania wanaingia kwenye uchaguzi huu, huku mchango wa bunge hilo ukiwa ni chini ya asilimia tano ya maamuzi yao. Hiyo October unayotishia nayo watu hakuna uchaguzi, bali ni kilele cha maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
 
Post yako namba, watanzania walikuwa wanafuatilia bunge la Ana Makinda, sio hili la gizani kama wachawi. Kwa maneno marahisi watanzania wanaingia kwenye uchaguzi huu, huku mchango wa bunge hilo ukiwa ni chini ya asilimia tano ya maamuzi yao. Hiyo October unayotishia nayo watu hakuna uchaguzi, bali ni kilele cha maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Huna ujualo. Piga kimya
 
Ewee muumba mbingu na nchi fanya miujiza Chadema wapate wabunge chini ya watano na hao watano baada ya muda waunge mkono juhudi.

Wote tuseme Aaaamin.
 
Back
Top Bottom