Pre GE2025 Kutakuwa na sare ya wanawake wote kitaifa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Machi 8 2025

Pre GE2025 Kutakuwa na sare ya wanawake wote kitaifa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Machi 8 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
1000021657.jpg

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mheshimiwa Dr. Dorothy Gwajima amesema kuwa kutakuwa na Sare ya Kitaifa tarehe 8 Machi 2025, kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani na pia;

Kabla ya tarehe 8 Machi, maadhimisho yataanza mikoani kwa kila mkoa kuandaa Sare yake ya alama ya eneo la mafanikio yake kwenye maendeleo ya wanawake mfano labda madini, kilimo, mifugo nk

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kitaifa mkoani Arusha, kutakuwa na sare maalumu ya kitaifa ambayo itapatikana kila mkoa.

Pia soma:

Sare hiyo itakuwa ni kitenge ambacho kitakuwa na rangi mbalimbali, ambapo kila mwanamke atachagua kitakachompendeza, na kwamba rangi za kitenge hicho zinaunda Bendera ya Tanzania.

Sare hiyo itasambazwa mikoa yote nchini, na itapatikana kwa mtu anayetaka kwa shilingi elfu 25 na kutozidi shilingi elfu 30 kwa rejareja.

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka huu ni ya kipekee, ikiwa ni mwaka wa 30 tangu safari ya Azimio la Beijing, China litolewe.

Kutakuwa na mikutano ya kimkakati ya mitandaoni ili jamii ijue mafanikio yaliyopatikana katika miaka hiyo 30.

Machi 7, 2025 kutakuwa na Usiku Maalumu wa Wanawake utakaofanyika mkoani Arusha, ambapo wanawake takribani 1,500 watashiriki.

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Bora mwaka huu Arusha watu wa dar kupendelewa sana
 
Kwanini kuna kichwa cha mtu kwenye kitenge?

Je, hiyo kusema sare zitasambazwa nchi nzima na kupatikana kwa shilingi 25 na 30 elfu je ni nani anasambaza? Kuna kampuni imepata tender hiyo ya kutengeneza na kusambaza? Je tender ilitangazwa kama taratibu zinavyotaka? Je, hii sio dalili ya kukiuka utaratibu wa INEC kwa kuanza kampeni mapema kwa kuanza kusambaza nguo za mgombea nchi nzima?
 
Embu nipite vile. Hii nchi bwana. #hjyvdhdfgddfubkfdsgfu
 
Back
Top Bottom