Kutana na Mhaya Advocate

Kutana na Mhaya Advocate

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2021
Posts
3,211
Reaction score
3,611
Advocate Rwankomez Bushoke Batamuzi, Mhaya wa Ruita Muleba ameenda kwenye harusi ya Muganyizi Byejumula Mulokozi, alivyotaka kuegesha gari yake ikawa hivi:-
  • Mhaya – nionyeshe wenye Harrier wanapaki wapi?
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – lete huku nikuonyeshe. Paki palee…
  • Mhaya – maweee! Wewe Tarishi! Mbona kuna Vogue na VX hapa?
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – VX ni la Mpishi wa chakula cha harusi na Vogue ni la Karani wa kitengo cha majitaka cha Manispaa. Ni watu wa kawaida tu hao usiogope.
  • Mhaya – what do you mean?!
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – mimi sijui lugha wewe paki hapo.
  • Mhaya – impossible kwa kweli, ebu nionyeshe wenye full-tank wanapaki wapi?
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – siyo kazi yangu kuingia kwenye matenki ya magari kujuwa kuna lita ngapi.
  • Mhaya – basi nionyeshe Ma-advocate wanapaki wapi?
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – mbona tunachoshana! Au hutaki kupaki?
  • Mhaya – hapana…, sikiliza…, ukichoshwa ndiyo unalipwa ujira, kazi yako ni kuchoswa, au hujui?
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – sasa nikusaidieje mpaka hapo?
  • Mhaya – nionyeshe wenye Masters ya UK ya Sheria wamepaki wapi. Usinipeleke kwa mafisadi.
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – subiri hapo nikuitie Kamanda wewe.
  • Mhaya – ngoja…, ngoja kwanza…, basi napaki hapahapa, lakini huko ndani ukumbini unionyeshe wanaoongea Oxford English kama mimi wamekaa wapi. Usinipeleke kwa washamba Wajaluo wanaoongea Cambridge English.
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – sihusiki ukumbini, nenda mwenyewe.
  • Mhaya – waambie hao wenye VX na Vogue nitawaundia Tume ya Uchunguzi.
  • Mlinzi (Bageni Bigacho) – kwenda zako, Advocate mzima unaendesha Harrier? Gari la Walimu Wakuu wa kike! Alafu unashoboka povu jiiingi hata haya huna!
Kisa na:
Douglas Majwala.
 
Back
Top Bottom