Kutendewa vibaya na nduguyo hakuumizi kama kudharauliwa na mgeni

Kutendewa vibaya na nduguyo hakuumizi kama kudharauliwa na mgeni

Hamatan

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2020
Posts
3,197
Reaction score
7,677
Kuna wakati, niliwahi kufanya kazi kwenye kampuni ya Barrick, nikiwa senior officer.

Tukataarifiwa kuwa plant imesimama, kuna kikao cha dharula. Kusimama plant kwa mgodi mkubwa siyo jambo dogo. Ndani ya saa moja, Head Office, Toronto ilikuwa tayari imejulishwa.

Kwenye kikao tukajulishwa kuwa sababu ya kusimama plant ni mgomo wa wafanyakazi wote Watanzania, kugoma kufanya kazi kwa madai kuwa kuna Kaburu katoa kauli ya ubaguzi.

Ilikuwa hivi:

Supervisor, ambaye ni mzungu aliona mfanyakazi Mtanzania amefanya kazi vibaya. Yule supervisor akasema, "that is why I do not trust you black people". Waliokuwa karibu na kuisikia kauli ile waliwajulisha Watanzania wengine, na wote wakaweka tools down. Plant ikasimama.

Taarifa ilipofika toronto, swali lilikuwa, "that has happenned, what do they want?" Meneja wa mgodi akawaambia, "they want him fired". Naye akawauliza, "then what is the problem? Do what they want, it is their country"

Hoja ni nini? Wafanyakazi wa kiTanzania kukosea, kusemwa, kuonywa na hata kukaripiwa na Watanzania wenzao haikuwa kitu cha ajabu, na hakuna wakati wafanyakazi walipogoma kwa sababu mfanyakazi mwenzao Mtanzania alikuwa amefokewa na Mtanzania mwenzao.

Kudhalilishwa na mgeni inaumiza sana, maana huleta tafsiri ya ninyi nyote mmedharauliwa. Kudharauliwa na mgeni kunaleta mshikamano na umoja, kama haukuwepo.

Marehemu Magufuli alikuwa anafokea sana. Wengi walivumilia maana ni kudhalilishwa na mwenzenu. Ingekuwaje kama kudhalilishwa kule kungekuwa kunafanywa na asiye Mtanzania au asiye Mtanganyika, kwa lugha ya Mtikila?

Ubaguzi wa kikanda au kikabila, ni mbaya sawa kama ubaguzi wa kidini au kieneo. Lakini unakuwa mbaya zaidi kama unafanywa na mgeni dhidi ya mwenyeji. Wazanzibari kuteuliwa kufanya kazi kwenye nafasi zisizo za muungano sawa, lakini mtanganyika kuteuliwa Zanzibar, hapana. Mzanzibari kupata ardhi bara sawa, Mtanganyika hata kumiliki square foot moja Zanzibar, hapana. Mzanzibari kuteua majaji Tanganyika sawa, lakini Mtanganyika kuteua hata sheha Zanzibar hapana. List ni ndefu, siwezi kumaliza.

IPO HIVI
Mtawala akitoka kwenye jamii ndogo tena ya ugenini, atakuwa muoga dhidi jamii kubwa ya wenyeji. Lakini anaweza kupata nguvu kubwa ya ajabu ya kutenda chochote anachotaka dhidi ya jamii kubwa, kama akiweza kuwagawa au akawakuta wamegawanyika maana atawapeleka kwenye mapambano wakapambane wenyewe kwa wenyewe, yeye akiwa raha mstarehe.

Yaliyotokea wakati wa Magufuli yalikwishatokea, tunatakiwa tutazame mbele kama Watanzania na kama Watanganyika, ili nguvu yetu ya pamoja iogopwe na ijitetee katika kuyalinda maslahi yetu.

Mambo sijui ya Sukuma gang, mara Kanda Pendwa au Chagadema na wachaga, hayataiacha Tanganyika salama wala Tanzania salama. Tukiyaendeleza haya niliyoyasema, anaweza kuja mtawala hata kutoka Comoro akatutawala kwa namna yoyote aipendayo, bila hofu kwa sababu atatumia mgawanyiko wetu.

Ni mchanganyiko wa hoja wenye dhamira moja. Wenye akili watanielewa maana lugha iliyotumika ni rahisi na mazingira yaliyotumika ni tunayoyaishi.
 
Unaweza kujiona MKOMAVU na MJUZI wa mambo kwa kuandika waraka mrefu ila UKACHEKESHA TU WALIONUNA....🤣🤣🤣

FYI Kaisome vyema historia ya TAIFA LETU PENDWA....yaani umekaa kwa kujiachia na kuongea kana kwamba ZANZIBAR ni nchi ya mbali sana....iko huko katikati ya bahari kupita MADAGASCAR huko Khaaa 😲😲🤣

Kwa UANDISHI wako inaonekana una ELIMU...cha ajabu ni kumuona mwenye elimu hiyo HAIJUI VYEMA HISTORIA YA TAIFA HILI....amejaa CHUKI KOKO ZA UBARA NA UZANZIBARI.

IMHO Baba wa Taifa ndiye aliyeasisi mfumo huu wa muungano na kuifuta Tanganyika kwa kutoa sababu njema zenye kueleweka vyema tu!

Hakuna Mtanzania aliye huku bara ambaye atasema ana haki zaidi ya Mzanzibari.....huu ni UJINGA NA UPUMBAVU wa KIWANGO kilichopitiliza.

BTW kule Zanzibar kuna Rais mwenye historia na MKURANGA....hili ni funzo kuwa MUUNGANO WETU NI WA KIPEKEE NA NI LAZIMA TUULINDE KWA NJIA ZOZOTE ZILE ZIWAZO.

N.B Mh.SSH si Rais wa kwanza wa JMT mwenye asili ya Zanzibar....swali fikirishi....ni kwanini MANENO "MBOFUMBOFU" yanakuja kipindi hiki?

Siempre JMT
Siempre Chifu Mkuu Hangaya aaamin🙏
JMT Kwanza
 
Tanganyika haipo.....
Tanganyika ilishazikwa.....

Ni maagano adhimu kuzilinda SERIKALI MBILI ZA JMT kwani bila ya hizo serikali mbili huu muungano "katu" haudumu/hautodumu.....

Hayati Mwalimu Nyerere aliliona hilo....wenye akili wakamuelewa.....

Wachache akina G55 wakaweka pamba masikioni.....mwishoni MSIMAMO WA DHAHABU WA MWALIMU NYERERE UKABAKI NA UTAENDELEA KUBAKIA MILELE aaamin aaaaamin🙏


Siempre JMT
 
yaani mtu anisononeshe kisa kaniita sukumagang!!!!!

akatiwe huko.
 
Tanganyika haipo.....
Tanganyika ilishazikwa.....

Ni maagano adhimu kuzilinda SERIKALI MBILI ZA JMT kwani bila ya hizo serikali mbili huu muungano "katu" haudumu/hautodumu.....

Hayati Mwalimu Nyerere aliliona hilo....wenye akili wakamuelewa.....

Wachache akina G55 wakaweka pamba masikioni.....mwishoni MSIMAMO WA DHAHABU WA MWALIMU NYERERE UKABAKI NA UTAENDELEA KUBAKIA MILELE aaamin aaaaamin[emoji120]


Siempre JMT
Wewe nawe una kera sana aiseee ... Watu kama ninyi ndio mnatuharibia Nchi hii. Jamaa kaja na hoja muhimu wewe unaanza kuleta UCCM na kutetea ugali wako. Shame on you
 
Wewe nawe una kera sana aiseee ... Watu kama ninyi ndio mnatuharibia Nchi hii. Jamaa kaja na hoja muhimu wewe unaanza kuleta UCCM na kutetea ugali wako. Shame on you
Hapo juu uliponiquote wapi nimeitaja CCM ?!!!

Hoja muhimu ni kuitaja Tanganyika na maslahi yake nje ya muungano ?!!!! Khaaa 😲😲😲

Ninyi ndio mnaotaka kutuharibia hii nchi.....

Shame on you too for failing to understand what I have meant!!!

Siempre JMT
 
Tanganyika haipo.....
Tanganyika ilishazikwa.....

Ni maagano adhimu kuzilinda SERIKALI MBILI ZA JMT kwani bila ya hizo serikali mbili huu muungano "katu" haudumu/hautodumu.....

Hayati Mwalimu Nyerere aliliona hilo....wenye akili wakamuelewa.....

Wachache akina G55 wakaweka pamba masikioni.....mwishoni MSIMAMO WA DHAHABU WA MWALIMU NYERERE UKABAKI NA UTAENDELEA KUBAKIA MILELE aaamin aaaaamin[emoji120]


Siempre JMT
Kinadharia Tanganyika haipo, kiuhalisia Serikali ya Tanganyika ndiyo Serikali ya Tanzania. Mambo ya Tanganyika, yasiyokuwa ya muungano, yanasimamiwa na serikali gani? Hiyo ndiyo Serikali ya Tanganyika iliyofutiwa jina lake.
 
Unaweza kujiona MKOMAVU na MJUZI wa mambo kwa kuandika waraka mrefu ila UKACHEKESHA TU WALIONUNA....[emoji1787][emoji1787][emoji1787]

FYI Kaisome vyema historia ya TAIFA LETU PENDWA....yaani umekaa kwa kujiachia na kuongea kana kwamba ZANZIBAR ni nchi ya mbali sana....iko huko katikati ya bahari kupita MADAGASCAR huko Khaaa [emoji44][emoji44][emoji1787]

Kwa UANDISHI wako inaonekana una ELIMU...cha ajabu ni kumuona mwenye elimu hiyo HAIJUI VYEMA HISTORIA YA TAIFA HILI....amejaa CHUKI KOKO ZA UBARA NA UZANZIBARI......

IMHO Baba wa Taifa ndiye aliyeasisi mfumo huu wa muungano na kuifuta Tanganyika kwa kutoa sababu njema zenye kueleweka vyema tu!!!!

Hakuna Mtanzania aliye huku bara ambaye atasema ana haki zaidi ya Mzanzibari.....huu ni UJINGA NA UPUMBAVU wa KIWANGO kilichopitiliza.........

BTW kule Zanzibar kuna Rais mwenye historia na MKURANGA....hili ni funzo kuwa MUUNGANO WETU NI WA KIPEKEE NA NI LAZIMA TUULINDE KWA NJIA ZOZOTE ZILE ZIWAZO......

N.B Mh.SSH si Rais wa kwanza wa JMT mwenye asili ya Zanzibar....swali fikirishi....ni kwanini MANENO "MBOFUMBOFU" yanakuja kipindi hiki?!!!

Siempre JMT
Siempre Chifu Mkuu Hangaya aaamin[emoji120]
JMT Kwanza
Ningependa hata Afrika iwe nchi moja, lakini yenye fomulae iliyo sahihi.

Bila ya kuwa na fomulae sahihi ya muungano, unauweka muungano wenyewe katika mazingira dhaifu.
 
Kinadharia Tanganyika haipo, kiuhalisia Serikali ya Tanganyika ndiyo Serikali ya Tanzania. Mambo ya Tanganyika, yasiyokuwa ya muungano, yanasimamiwa na Aerikali gani? Hiyo ndiyo Serikali ya Tanganyika iliyofutiwa jina lake.
Kwa hiyo unatuletea somo jipya kabisa lisilopata kufikiriwa na yeyote yule isipokuwa wewe na wala kutopata kufundishwa na hayati Mwalimu Nyerere?

Kwa uandishi wako naona hata aibu kukukumbusha mafunzo ya baba wa taifa juu ya MUUNGANO WETU WA KIPEKEE.

Rejea Hotuba zake Mwalimu Nyerere utajua ni serikali ipi isimamiayo Mambo yasiyo ya kimuungano!

Siempre JMT
 
Back
Top Bottom