Kutengeneza dawa ya kuku ya kutibu magonjwa yote kwa mitishamba

naongezea
chukua majani mabichi ya mwarobani yaanike kivulini au kibarazani (yasikauke kwa jua) then uje uyatwange then chanyanya kwenye chakula chao ..majani hayo yana antibaotic nyingi.

nyingine ni majani ya mti wa mlingalinga yafanye kama ulivyofanya mwarobaini ,hayo yana vitamin nyingi sana kuzidi ya kwenye aminototal
 
Mkuu, naomba jina lingine la huo mlingalinga, au picha binafsi sifahamu huo mmea
 
Yapata wiki sasa nahangaika na tatizo la Kuku kuvimba macho na kuwa vipofu kabisaa mpaka sasa ni Kuku 22 ndio wamepatwa na tatizo hilo, nimewahamisha banda kabisa ili wasichangamane na Kuku wengine wakaleta maafa zaidi nimeshajaribu kutumia antibiotics mbali mbali kama Piperazine citrate, sevin , Akheri powder kuwatibu lakini wapi yaani tatizo liko palepale kinachoniumiza zaidi hawa Kuku walishaanza kutaga na wengine ndio wanaelekea kuanza kutaga.
Kama kuna wataalamu humu naomba msaada wa cha kufanya maana mambo yanakua magumu sasa,hii ndio biashara pekee ambayo hakika haikuwahi kuniangusha sasa kama nitaanguka kwenye hii Nayo miti yote itakua inateleza kwangu hivyo chini nitaanguka
 
Ili tatizo hata nami naliona kwa kuku wangu.....
 
kamaupo Dar peleka Vetinari utapata ufumbuzi wa tatizo lako
 
Nimafua makali waminye hayo macho kwandani litatokea jitu jeupe gumu na uwasafishe na Maji ya vuguvugu yaliyo na chumvi halafu wapatie indosini vidonge
Nitafanya hivyo Mkuu ,asante kwa ushauri
 
kamaupo Dar peleka Vetinari utapata ufumbuzi wa tatizo lako
Huko nimeenda wamenipa hayo madawa lakini wapi wiki sasa hakuna matumaini,hofu yangu wasije wote wakaugua huu ugonjwa mapaka sasa ni Kuku 22 mkuu
 
Mimi ilitokeaga hivyo nikawapa safar lager .wakapona kabisa.fanyia utafiti kwanza huenda ukawasaidia na wako
 
TIBA ZA MAGONJWA YA KUKU NI KAMA ZA KUBAHATISHA MKUU,MIMI NI MWAKA WA SITA TAUNGU NIMEANZA KUFUGA KUKU,UKITOKEA UGONJWA UTAAMBIWA NUNUA DAWA HII,MARA NUNUA DAWA ILE MWISHOWE WANAKUFA WOTE,AFADHALI KAMA UNA UWEZO UJARIBU KUNUNUA KUKU AMBAO HAWAJAANZA KUTAGA KUTOKA MIKOANI UWAPE DAWA NA KINGA KABLA YA KUWACHANGANYA NA WENGINE.
 
Pole,usikate tamaa my dia
Jaribu kuwaona wataalam
Inawezekana ikawa ndui au wana deficiency ya vit a
 
Yaani acha tu Mkuu, mimi hapa nina mabanda manne ya Kuku nilianza na banda 1 tu wakati huo niliwanunua huko vijijin wakiwa wadogo, yaani hawa ni Kuku original wa kienyeji sio machotara sasa hofu yangu ni kuwapoteza wote na hakika Kuku huwa wananilipa sana na kusaidia familia ambayo kwa sasa kuna wakati mgumu tunapitia,nitajitahidi nipambane kuwaokoa ila hadi nakosa usingizi kwa kweli
 
Huko nimeenda wamenipa hayo madawa lakini wapi wiki sasa hakuna matumaini,hofu yangu wasije wote wakaugua huu ugonjwa mapaka sasa ni Kuku 22 mkuu
Napata mashaka kuamini hizo dawa ulishauriwa ulipoenda veterinari. Labda kama si veterinari nayoijua mie. Piperazine inatibu minyoo na hizo nyingine mbili zinaua vidusia (parasites) wa nje. Tatizo la kuku wako si mojawapo kati ya hayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…