Kuto kujua taratibu ndiyo sababu ya mahusiano / ndoa kuvunjika

Kuto kujua taratibu ndiyo sababu ya mahusiano / ndoa kuvunjika

Anyisile Obheli

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2009
Posts
3,400
Reaction score
320
Ndoa nyingi zina matatizo kwa kuwa wengi wetu wa wanandoa tumeingia na zile tabia zetu za ujana, pasi na kujua kuwa ndoa ni mlango mwingine ambao ili uweze kupita na kumudu sheria zake ni lazima ulazimike kukua kimawazo na kiakili
pia uweze kuvua baadhi ya mavazi ya umimi na kuyavaa mavazi ya sisi yaani wawili
kuna haja ya kubadirika tu uingiapo kwenye mlango huu wa nyumba inayoitwa ndoa na humo utakutana na mavazi mengine mazuri aina ya uvumilivu, utii, heshima, adabu, na kujifanya mjinga mwelevu.
Mavazi ya ujuaji mwingi kwenye ndoa hayatakiwi kabisa, na kama unaona kuwa bado unayahitaji na yanakufaa basi ni vema ukaendelea kwanza kuyavaa ili ukijaingia humo usilete usumbufu kwa mweza wako, kwani huchafua sana utu wa mtu, maana hakuna sifa mbaya ya kuitwa aliachika akaolewa tena, aliacha akaoa tena.
Kama unaona duka lako linahitaji wateja wengi, basi ni wakati mzuri wa kuwahudumia kwanza mpaka utosheke na ndipo uingie katika ndoa maana humo mteja ni mmoja tu, wala hahitaji kupanga foleni kutaka kuhudumiwa, nasema haya kwa waume na wake.
 
This is the ideal situation, practically ni tofauti mkuu.
 
This is the ideal situation, practically ni tofauti mkuu.

What are u talking about???? Life must be built on principles some of which may appear tough. We unataka mambo rahisirahisi tu. Unapoamua kuoa/kuolewa lazima kuna vitu vya kuacha. Usipoviacha huwezi kuwa na ndoa imara. No wonder devorce rate is increasing maana kuna watu wanataka kula keki halafu waendelee kuwa nayo
 
Mara nyingi mwanaume humuoa mwanamke akitegemea kuwa atabaki hivyohivyo na sio kubadilika, wakati mwanamke humkubali mwanaume akitarajia kuwa yule mwanaume atabadilika na kuachana na vitendo visivyompendeza anavyofanya. Lakini mara nyingi pia haya huwa tofauti kabisa...!
 
Ndoa nyingi zina matatizo kwa kuwa wengi wetu wa wanandoa tumeingia na zile tabia zetu za ujana, pasi na kujua kuwa ndoa ni mlango mwingine ambao ili uweze kupita na kumudu sheria zake ni lazima ulazimike kukua kimawazo na kiakili
pia uweze kuvua baadhi ya mavazi ya umimi na kuyavaa mavazi ya sisi yaani wawili
kuna haja ya kubadirika tu uingiapo kwenye mlango huu wa nyumba inayoitwa ndoa na humo utakutana na mavazi mengine mazuri aina ya uvumilivu, utii, heshima, adabu, na kujifanya mjinga mwelevu.
Mavazi ya ujuaji mwingi kwenye ndoa hayatakiwi kabisa, na kama unaona kuwa bado unayahitaji na yanakufaa basi ni vema ukaendelea kwanza kuyavaa ili ukijaingia humo usilete usumbufu kwa mweza wako, kwani huchafua sana utu wa mtu, maana hakuna sifa mbaya ya kuitwa aliachika akaolewa tena, aliacha akaoa tena.
Kama unaona duka lako linahitaji wateja wengi, basi ni wakati mzuri wa kuwahudumia kwanza mpaka utosheke na ndipo uingie katika ndoa maana humo mteja ni mmoja tu, wala hahitaji kupanga foleni kutaka kuhudumiwa, nasema haya kwa waume na wake.

Mkuu Anyisile,
Naomba ruhusa yako niiprint hii thread nimpelekee wife wangu hard copy ili awe anaisoma mara kwa mara.
Tafadhali.
 
Ndoa nyingi zina matatizo kwa kuwa wengi wetu wa wanandoa tumeingia na zile tabia zetu za ujana, pasi na kujua kuwa ndoa ni mlango mwingine ambao ili uweze kupita na kumudu sheria zake ni lazima ulazimike kukua kimawazo na kiakili
pia uweze kuvua baadhi ya mavazi ya umimi na kuyavaa mavazi ya sisi yaani wawili
kuna haja ya kubadirika tu uingiapo kwenye mlango huu wa nyumba inayoitwa ndoa na humo utakutana na mavazi mengine mazuri aina ya uvumilivu, utii, heshima, adabu, na kujifanya mjinga mwelevu.
Mavazi ya ujuaji mwingi kwenye ndoa hayatakiwi kabisa, na kama unaona kuwa bado unayahitaji na yanakufaa basi ni vema ukaendelea kwanza kuyavaa ili ukijaingia humo usilete usumbufu kwa mweza wako, kwani huchafua sana utu wa mtu, maana hakuna sifa mbaya ya kuitwa aliachika akaolewa tena, aliacha akaoa tena.
Kama unaona duka lako linahitaji wateja wengi, basi ni wakati mzuri wa kuwahudumia kwanza mpaka utosheke na ndipo uingie katika ndoa maana humo mteja ni mmoja tu, wala hahitaji kupanga foleni kutaka kuhudumiwa, nasema haya kwa waume na wake.

Wengi wanatenda bila kufikiri na pia na ukawa na umimi katika ndoa ni moja wapo ya mahusiano mengi kutokufika mbali nakumbuka nikiwa kanisani padri alisema dhumuni hasa la ndoa ni kumfanya mumeo au mkeo awe mtakatifu watoto ni matokeo lini kitu cha muhimu ni kumfanya mwenzako awe mtakatifu.
 
Mkuu Anyisile,
Naomba ruhusa yako niiprint hii thread nimpelekee wife wangu hard copy ili awe anaisoma mara kwa mara.
Tafadhali.
uwe huru tu wala haina neno, umuhimu mkubwa wa jf kwangu ni kujifunza,
kwa kile ukionacho kinakufaa kwa thread kutumia we tumia tu hahaaaahaaa
 
Wengi wanatenda bila kufikiri na pia na ukawa na umimi katika ndoa ni moja wapo ya mahusiano mengi kutokufika mbali nakumbuka nikiwa kanisani padri alisema dhumuni hasa la ndoa ni kumfanya mumeo au mkeo awe mtakatifu watoto ni matokeo lini kitu cha muhimu ni kumfanya mwenzako awe mtakatifu.

hii inatokana na watu ama wanandoa wenyewe kuingia humo bila kuwa na uelewa wa ni wapi wanatoka na wapi
wanakwenda, ndoa ni kama chombo cha moto, ambacho kwa bahati mbaya huendeshwa na madereva wawili,
ambao kila mmoja ana ujuzi wa chuo tofauti na mwenziye,
kuna haja ya kila mmoja kujua sheria za barabara hiyo ambayo hicho chombo ndoa hutumia kwa kupita, ili kuweza kuweza
kutoa nafasi kwa madereva hao kuweza kuimudu vilivyo,
 
Ndoa nyingi zina matatizo kwa kuwa wengi wetu wa wanandoa tumeingia na zile tabia zetu za ujana, pasi na kujua kuwa ndoa ni mlango mwingine ambao ili uweze kupita na kumudu sheria zake ni lazima ulazimike kukua kimawazo na kiakili
pia uweze kuvua baadhi ya mavazi ya umimi na kuyavaa mavazi ya sisi yaani wawili
kuna haja ya kubadirika tu uingiapo kwenye mlango huu wa nyumba inayoitwa ndoa na humo utakutana na mavazi mengine mazuri aina ya uvumilivu, utii, heshima, adabu, na kujifanya mjinga mwelevu.
Mavazi ya ujuaji mwingi kwenye ndoa hayatakiwi kabisa, na kama unaona kuwa bado unayahitaji na yanakufaa basi ni vema ukaendelea kwanza kuyavaa ili ukijaingia humo usilete usumbufu kwa mweza wako, kwani huchafua sana utu wa mtu, maana hakuna sifa mbaya ya kuitwa aliachika akaolewa tena, aliacha akaoa tena.
Kama unaona duka lako linahitaji wateja wengi, basi ni wakati mzuri wa kuwahudumia kwanza mpaka utosheke na ndipo uingie katika ndoa maana humo mteja ni mmoja tu, wala hahitaji kupanga foleni kutaka kuhudumiwa, nasema haya kwa waume na wake.

ni kweli kabisa mkuu!!! kama bado hujaamua kuacha baadhi ya vitu unavovipenda ni bora uwepo uwepo kwanza aisee.
tusikimbilie vitu ambavyo bado hatujajitolea kuvimudu ipasavyo.:thumb:
 
ni kweli kabisa mkuu!!! kama bado hujaamua kuacha baadhi ya vitu unavovipenda ni bora uwepo uwepo kwanza aisee.
tusikimbilie vitu ambavyo bado hatujajitolea kuvimudu ipasavyo.:thumb:
sawasawa kabisa kiukweli kitu ndoa kinahitaji miili iliyopoa ili kuimwagilia na kuistawisha,
lakini miili ambayo bado ni moto kwa mambo ya tamaa, hiyo haiwezi kabisa ndoa,
kila leo lawama na kusutana hakuishi, maana kabla hujaingia kwenye huo mlango wa ndoa
lazima ukubali na kusaini mkataba wa kufunga mapazia yako ya madirisha ya tamaa na kukubari kuwa uko tayari kuwa kipofu kwa yaliyo nje ya ndoa bali unaona sana kwa yale ya ndani ya ndoa yako
 
Anyisile, Hayo yote yanajulikana, utekelezaji ndo unasumbua
 
Kinachomfanya mtu ashindwe kutekeleza ni nini hasa? Maana sidhani kama kuna sababu ya msingi

sababu ya msingi ipo na hata ukisoma sana hiyo thread kwa makini utakuta ndani kuna baadhi ya vitu vunavyopaswa kuviangalia
ili vikusaidie mala uingiapo huo mlango wa ndoa, nadhani pengine umeisoma kwa haraka sana,
maana kubwa la maelezo yaliyopo humo ni jinsi gani watu/wanandoa/ wameziharibu na kuzivunja ndoa zao kwa kukiuka taratibu
 
Asante sana mpendwa ni somo fupi lakini limebeba ujumbe mzito ..ubalikiwe na bwana
 
Back
Top Bottom