Kutofuta katiba Je, itakuwa ajenda ya kuwabeba wapinzani?

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,030
Reaction score
20,391
Umoja wa Katiba ya Wananchi wa vyama vya upinzani (UKAWA) uliibuka kutokana na minyukano ya kimaslahi ya siasa huku ukinasibu kutetea maoniya wananchi, na ndio waliosikilizwa zaidi kuliko serikali na chama na tawala.

Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 vyama vya siasa vya ACT Wazalendo, Chadema, NCCR Mageuzi kupitia ilani zao na mikutano ya kampeni vyote vilinadi kurejesha mchakato wa katiba mpya kupitia Bunge la Katiba.

NCCR Mageuzi walieleza kuwa iwapo wangeshinda wangehakikisha wanaitisha muafaka wa kitaifa ili kutengeneza matakwa na kupatikana kwa katiba mpya ya Tanzania.

Wakati serikali ya awamu ya nne chini ya rais Jakaya Kikwete ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa CCM ilipoanzisha mchakato wa Katiba mpya suala hilo halikuwa miongoni mwa sera za chama hicho katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010-2015.

Hata hivyo shinikizo la wananchi, wanazuoni, wanaharakati,wadau wa maendeleo lilichangia pakubwa kushuhudia uongozi wa Kikwete kuanzisha mchakato huo.

Vyovyote itakavyokuwa upepo wa mchakato wa katiba mpya utabaki kuwa ajenda ya vyama vya upinzani kama sehemu ya kunyukana kisiasa na chama na serikali iliyopo madarakani. Kukinzana kwa wabunge wawili tajwa ni ishara ya awali kuelekea kwenye mnyukano halisi.

Haifahamiki namna CCM na serikali ya Rais Samia itachukua hatua gani au itatafsiri vipi upepo huo ikiwa utavuma kwa kasi na kupokelewa vizuri kwa mara nyingine wananchi wa Tanzania.

Wanasiasa wa vyama vyote, tawala na upinzani wanaonekana kumsoma kwanza rais mpya Samia Suluhu kabla ya kutumbukiza miguu yao kwenye utawala wake huku mchakato wa Katiba ni miongoni mwa mambo yatakayoibuliwa.

Upepo wa sasa unaonekana kumwendea vizuri Rais Samia kwa sababu wanasiasa wa vyama vyote wamefurahishwa na mwenendo wake wa awali kupitia hotuba kadhaa alizozitoa zikidaiwa kujaa mamlaka,diplomasia na kuunganisha Taifa hilo pamoja na mwanzo wa muundo wa serikali yake.

Hata hivyo Wanasiasa kwa asili wakimaliza kusoma mtindo wa mtawala wao kwa kawaida huanza mizungu na kupenyeza ajenda zao. Huko ndiko uliko uwezekano wa kuzaliwa UKAWA ya pili katika madai ya katiba mpya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…