Kutoka Arusha - Vita Kati ya Kampuni ya Kilimanjaro Parking Sistem vis Barrick Parking Sistem

Kutoka Arusha - Vita Kati ya Kampuni ya Kilimanjaro Parking Sistem vis Barrick Parking Sistem

Ndallo

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2010
Posts
7,619
Reaction score
4,299
Hapa Arusha leo ni kelele mji mzima kupitia vipaza sauti kwenye magari mawili yanayotangaza zoezi la ukusanyaji wa kutoza ushuru wa magari yanayopaki Arusha mjini pamoja na viunga vyote vya jijini hapa!

Kulikoni? nikwamba kampuni ambayo ilikua inaendelea na ukusanyaji ushuru ya Barrick Printers Parking Sistem wanatakiwa kuondoka kwenye maeneo ya ukusanyaji ushuru na kuwapisha wakusanyaji wapya wanaojiita Kilimanjaro Parking Sistem, ukipita kwenye viunga vyote vya mjini utaona wakusanya ushuru wa aina mbili kwenye hizi Uniform zao, wale ambao wanaendelea na zoezi hili wao wamevaa Jacket za rangi ya Chungwa (Barrick Printers Parking Sistem), na hawa ambao wanadai sasa ndio wanayohaki ya kutoza ushuru, wao wamevaa Jacket za rangi ya Light Blue (Kilimanjaro Parking Sistem).

Hali hii imeshawachanganya hata waendeshao magari kua kwasasa wamlipe nani? nimeuliza kutoka kwa mkusanya ushuru mmoja kulikoni? akaniambia kua kuna kesi iko mahakamani na mahakama imeshatoa amri kua hawa Barrick Printers Parking Sistem waendelee na zoezi hili la utoza ushuru, na hawa wa kampuni ya Kilimanjaro Parking Sistem nao wanadai wanahaki ya kukusanya ushuru na kibali wapepata kutoka halmashauri yaani Manispaa. Sasa basi kutokana na kelele hizi za maspika barabarani na kua kero, madereva nao wamedai zoezi hili likiendelea na wao pia watagoma kulipa ushuru kutokana na hawajui ni nani mwenye dhamana hii ya kukusanya ushuru. Haya ndio mambo Mseto kutoka jijini Arusha.
 
nimewaona hata mm ila sikuwa najua poa asnte kwa taarifa
 
Wizi mtupu!
Hapo ujue kila kampuni inapigiwa debe na mtu fulani anayesimama nyuma!
 
basi na sisi tunagoma.....hatupaki.....
 
kupaki tutapaki lakin hatulipi,wakija wawil ntawauliza,nani ana haki ya kulipwa,wakiendelea kubishana nawasha gari nasepa...
 
Hizi kazi za Halmashauri zina walakini sana; huwezi mpa mtu kazi inayohitaji kuajiri zaidi ya watu mia kwa mkataba wa mwaka mmoja; shida ni Watanzania (wanaoajiriwa) hawahui haki zao vinginevyo hakuna kampuni ingeomba kazi za Halmashauri kama siyo za miaka mitatu na kuendelea
 
Hii nchi inahitaji kiongozi Shujaa, kila sehemu ni kulipa ushuru halafu hizo pesa zenyewe tunazotozwa hawazitumii kwa maendeleo yetu ni bora tusilipe kabisa. Ushuru kila sehemu, kulima ushuru, kuvuna ushuru, kununua gari ushuru, kupark gari ushuru, kupitisha mushumaa wa mwenge ushuru, mashuleni ushuru kila sehemu ya hii nchi ni ushuru ushuru. Sisi walalahoi tupo kwenye hali mbaya sana kwa kuwa huu ushuru unatulenga sisi.
 
Hapa Arusha leo ni kelele mji mzima kupitia vipaza sauti kwenye magari mawili yanayotangaza zoezi la ukusanyaji wa kutoza ushuru wa magari yanayopaki Arusha mjini pamoja na viunga vyote vya jijini hapa!

Kulikoni? nikwamba kampuni ambayo ilikua inaendelea na ukusanyaji ushuru ya Barrick Printers Parking Sistem wanatakiwa kuondoka kwenye maeneo ya ukusanyaji ushuru na kuwapisha wakusanyaji wapya wanaojiita Kilimanjaro Parking Sistem, ukipita kwenye viunga vyote vya mjini utaona wakusanya ushuru wa aina mbili kwenye hizi Uniform zao, wale ambao wanaendelea na zoezi hili wao wamevaa Jacket za rangi ya Chungwa (Barrick Printers Parking Sistem), na hawa ambao wanadai sasa ndio wanayohaki ya kutoza ushuru, wao wamevaa Jacket za rangi ya Light Blue (Kilimanjaro Parking Sistem).

Hali hii imeshawachanganya hata waendeshao magari kua kwasasa wamlipe nani? nimeuliza kutoka kwa mkusanya ushuru mmoja kulikoni? akaniambia kua kuna kesi iko mahakamani na mahakama imeshatoa amri kua hawa Barrick Printers Parking Sistem waendelee na zoezi hili la utoza ushuru, na hawa wa kampuni ya Kilimanjaro Parking Sistem nao wanadai wanahaki ya kukusanya ushuru na kibali wapepata kutoka halmashauri yaani Manispaa. Sasa basi kutokana na kelele hizi za maspika barabarani na kua kero, madereva nao wamedai zoezi hili likiendelea na wao pia watagoma kulipa ushuru kutokana na hawajui ni nani mwenye dhamana hii ya kukusanya ushuru. Haya ndio mambo Mseto kutoka jijini Arusha.
nlilifikiri tangu mh. raisi aliposema sasa arusha amani na mikutano ya kimataifa imerudi ilikuwa ni kweli, kuna ni tene?//
 
Back
Top Bottom