Kutoka Jamvi la Habari: Kitabu nilichosoma na Hafidh Kido

Kutoka Jamvi la Habari: Kitabu nilichosoma na Hafidh Kido

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KUTOKA GAZETI LA JAMVI LA HABARI: KITABU NILICHOSOMA
RAJABU KIRAMA JEMEDARI WA VITA KUWA JEMEDARI WA UISLAMU: MOHAMED SAID

Na Hafidh Kido

NIMEKUWA na utaratibu wa kufanya ziara za mara kwa mara kumtembelea mwalimu wangu Mohamed Said, lengo ni kuchota elimu ya historia na masuala mengine katika uandishi.

Mara zote nikikutana naye kwenye mazungumzo yetu huwa namdodosa maswali ya hapa na pale, nikitumia mbinu za kihabari kuchota elimu isiyoisha kwake.

Kila siku nikiondoka sikosi kuambiwa na mwalimu wangu nitafute kitabu hiki au kile cha kusoma ili kuongeza maarifa.

Wakati fulani nilipokwenda kumweleza juu ya kitabu changu kipya ‘Kanzu ya Ukubwa’ akanigusia mswada wa kitabu chake kipya cha maisha ya Jemedari wa Vita aliyesaidia kufikisha Uislamu chini ya Mlima Kilimanjaro, Mzee Rajabu Ibrahim Kirama.

Ni kitabu kidogo chenye kurasa 100 kisichochosha kusoma, kina maarifa mengi yaliyokusanywa mahala pamoja kwa umakini wa hali ya juu.

Kama ilivyo kwa mwalimu wangu Mohamed Said, maandiko yake lazima yatokane na utafiti wa kina, kila alichosema kilihusu nyaraka alizozipata kutoka kwa watoto na wajukuu wa Mzee Kirama.

Utangulizi wa kitabu umeandikwa na Profesa Issa Haji Ziddy kutoka Zanzibar, ambaye ameutendea haki utangulizi wake kwa kueleza maneno machache yenye kumaliza kila kitu kilichokusudiwa kwenye kurasa 100.

Sura ya kwanza mwandishi anatupitisha katika historia ya Wachagga, akiwaangazia sana watu wawili Mangi Ndeseruo Mamkinga aliyeongoza kabila la Wamachame Kijiji cha Nkuu kati ya mwaka 1855 hadi 1880, wa pili ni Muro Mboyo ambaye ni baba yake Kirama Mboyo ambaye baadaye ndiyo alikuja kutambulika kama Rajabu Kirama alipoupokea Uislamu kutoka Upagani.

Salim Rajabu mtoto wa kwanza wa Rajabu Kirama ndiye aliyehifadhi nyaraka ambazo mwandishi Mohamed Said alifanikiwa kuzichambua na kutuletea historia hii iliyotukuka.

Wengi tumekuwa tukishangazwa na namna Uislamu ulivyochipua katika Mkoa wa Kilimanjaro, tukisema ukiona Mchagga au Mpare ni Muislamu basi anakuwa Muislamu kweli kweli.

Nadhani hii inatokana na magumu waliyopitia babu zao kina Rajabu Kirama, waliteswa, walifungwa na kudhalilishwa na watawala wa kimila wakisaidiwa na wageni, Wajerumani na Waingereza.

Kazi kubwa ya Muro Mboyo ilikuwa ni kumlinda Mangi Ndesaruo Mamkinga, alikuwa ndiye Jemedari wa Jeshi la kabila la Wamachame.

Utaona alikuwa mtu muhimu katika historia ya Wachagga.

Baadaye ilikuja kutokea fitina kubwa ya kitawala, ambapo Muro Mboyo alitakiwa kumuua Mangi Ngamini.

Fitna ilianzia wakati Mangi Ndeseruo akiwa mgonjwa, akataka wazee wa kimila wamrithishe kiti cha umangi mtoto wake mdogo Shangali ambaye kwa wakati huo alikuwa mtoto wa miaka mitatu.

Hata hivyo, Ngamini akachukua madaraka kwa kufuata taratibu zote za kimila, lakini baadaye kilizuka kikundi kumtaka auawe.

Aliyekuwa na taarifa za kuuawawa kwa Mangi Ngamini ni Mangi Sina wa Kibosho, ambaye inaelezwa katika nyaraka hizi alilelewa na Mangi Ndesaruo tangu utotoni kisha akapewa eneo la kutawala Kibosho.

Habari za sababu za kulelewa nyumba ya Mangi Ndesaruo zipo pia kwenye kitabu hiki chenye historia kubwa ya Wachagga.

Aidha, kwa kuwa Muro Mboyo kazi yake ilikuwa kumlinda Mangi, akaona si busara kumuua atakuwa hajatimiza wajibu wake, akaamua kutoroka naye hadi Old Moshi kwa Mangi Rindi Mandara.

Hata hivyo, inaelezwa safari yao hii haikufanikiwa bali palitokea vita kubwa ya kiukoo iliyoleta uhasama wa hali ya juu, ambapo inaelezwa Mangi Ngamini aliuawawa katika vita hii. Ndipo Muro Mboyo akakimbilia uhamishoni Old Moshi.

Habari ni ndefu, kubwa na ya kusisimua; kwa mfano mwaka 1945 Sheikh Hassan bin Ameir alifanya ziara Machame, miongoni mwa matunda ya ziara hiyo ni kupelekwa walimu wanne kwenda kusomesha dini Kilimanjaro.

Waalimu hao ni Sheikh Saleh Mwamba, Shariff Alawi, Sheikh Mahmud Mshinda na Sheikh Abdallah Minhaji.

Ambapo wawili walikwenda Upareni ambao wanatajwa Sheikh Salehe Mwamba alieda Usangi na Shariff Alawi alienda Ugweno, huku Sheikh Mahmud Mshinda alienda Moshi na Sheikh Abdallah Minhaj alipelekwa Machame.

Nakushauri msomaji wangu ukitafute kitabu hiki murua, kina historia kubwa si tu katika dini ya Uislamu na Ukristo namna ulivyowasili Kilimanjaro, lakini pia kinaeleza kwa mapana yake historia ya kabila la Wachagga.

Mwisho


 
naamini mwandishi wa kitabu hajaitendea haki jamii yetu ya WAPARE. Dini ya Kiislamu ilikuwa imeota mizizi Upareni miaka mingi kabla ya nyakati za Rajabu Kirama, au zama za Sheikh Hassan Bin Ameir. Mwandishi anakosea kuziweka katika kundi moja jamii za Wapare na Wachaga anapoangazia masuala ya imani za dini haswa Uislamu. Kwa taarifa tu, ktk jamii ya Wapare Waislamu ni wengi kuliko ndugu zao Wakristo. Hiyo ni tofauti ya kwanza katika masuala ya imani kati ya Wapare na watani zao Wachaga. Kinachofanya jambo hilo lisijulikane ni ile hali waumini wa Kiislamu na Kikristo kuishi bila mikwaruzano ktk jamii ya Wapare. Kwa kuongeza tu, Wafumwa au Machifu wengi ktk jamii ya Wapare walikuwa ni waumini wa dini ya Kiislamu. Usangi ambayo mwandishi anasema walipelekewa Waalimu wa dini mwaka 1945 tayari walikuwa na Wafumwa Waislamu kama Mfumwa Sabuni Naguvu, na Shabani Mtengeti Sangiwa. Kosa la mwisho alilofanya mwandishi ni kushindwa kutambua kwamba wilaya za Same na Mwanga ambazo wenyeji wake ni Wapare kabla ya uhuru wa Tanganyika zilikuwa sehemu ya jimbo la Tanga.
 
naamini mwandishi wa kitabu hajaitendea haki jamii yetu ya WAPARE. Dini ya Kiislamu ilikuwa imeota mizizi Upareni miaka mingi kabla ya nyakati za Rajabu Kirama, au zama za Sheikh Hassan Bin Ameir. Mwandishi anakosea kuziweka katika kundi moja jamii za Wapare na Wachaga anapoangazia masuala ya imani za dini haswa Uislamu. Kwa taarifa tu, ktk jamii ya Wapare Waislamu ni wengi kuliko ndugu zao Wakristo. Hiyo ni tofauti ya kwanza katika masuala ya imani kati ya Wapare na watani zao Wachaga. Kinachofanya jambo hilo lisijulikane ni ile hali waumini wa Kiislamu na Kikristo kuishi bila mikwaruzano ktk jamii ya Wapare. Kwa kuongeza tu, Wafumwa au Machifu wengi ktk jamii ya Wapare walikuwa ni waumini wa dini ya Kiislamu. Usangi ambayo mwandishi anasema walipelekewa Waalimu wa dini mwaka 1945 tayari walikuwa na Wafumwa Waislamu kama Mfumwa Sabuni Naguvu, na Shabani Mtengeti Sangiwa. Kosa la mwisho alilofanya mwandishi ni kushindwa kutambua kwamba wilaya za Same na Mwanga ambazo wenyeji wake ni Wapare kabla ya uhuru wa Tanganyika zilikuwa sehemu ya jimbo la Tanga.
Bangusule,
Ahsante kwa mchango wako huu kuhusu Uislam Upareni.

Ikiwa una ithibati na kauli yako kuwa wakati Rajabu Ibrahim Kirama analeta walimu kusomesha Qur'an Upare "...dini ya Kiislam ilikuwa imeota mizizi miaka mingi Upareni..." hakika utakuwa na historia ya kuvutia kupita kiasi.

Ningependa sana kujua historia vipi Uislam uliingia Upare na majina ya masheikh wa miaka hiyo na juhudi zao katika kujenga madrasa na misikiti.

Ningependa pia kujua kujua historia na uhusiano wa masheikh hawa waliokuwapo Upare na harakati za Mzee Rajabu zilizotokea Machame.

Ningependa kujua ni mambo gani walifanya pamoja katika kuujenga Uislam.

Nimesoma katika Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama barua ya tarehe 23 May, 1956 kutoka kwa Sheikh K.S. Kiangi Mswia wa Muslim Association, Ugweno Pare akimwandikia Secretary Abubakar Mariko wa Msikiti Machame, Kalali, Member Muslim Association, Salim Rajabu.

Maudhui ya barua hii ni mkutano ulioandaliwa na Waislam wa Upare kwa madhumuni ya kuimarisha dini kati ya Wachagga na Wapare.

Huyu Salim Rajabu anaeandikiwa barua hii ni mtoto mkubwa wa Rajabu Ibrahim Kirama.

Nimesoma barua nyingine zinazoelezea juhudi za Waislam wa Kilimanjaro, Upare na Usambaa kujenga Muslim Schools na aliyekuwa akisukuma haya yote alikuwa Rajabu Kirama na mwanae Salim.

Historia hii niliyoandika ambayo unaona imepungukiwa itanufaika sana kwa kupata maelezo kutoka kwako kuwa wapo katika historia ya Waislam waliomtangulia Rajabu Kirama Upareni.
 
Mzee mruma ni muislam tangu mwaka 1900, sasa unanchanganya kusema uislam upareni ni 1950s

JE WAJUA UKRISTO NDIYO ILIKUWA DINI YA KWAZA PWANI YA AFRICA MASHARIKI NA VISIWANI IKIWEPO ZANZIBAR KABLA YA UISLAM???
 
Mzee mruma ni muislam tangu mwaka 1900, sasa unanchanganya kusema uislam upareni ni 1950s

JE WAJUA UKRISTO NDIYO ILIKUWA DINI YA KWAZA PWANI YA AFRICA MASHARIKI NA VISIWANI IKIWEPO ZANZIBAR KABLA YA UISLAM???

Seriously?
Sijui historia hiyo uliisoma kutoka vitabu gani, hebu tupe reference tafadhali
 
Mzee mruma ni muislam tangu mwaka 1900, sasa unanchanganya kusema uislam upareni ni 1950s

JE WAJUA UKRISTO NDIYO ILIKUWA DINI YA KWAZA PWANI YA AFRICA MASHARIKI NA VISIWANI IKIWEPO ZANZIBAR KABLA YA UISLAM???
Jay...
Ikiwa una taarifa za Mzee Mruma tuandikie historia yake vipi aliingia Uislam mwaka wa 1900.
 
Mzee mruma ni muislam tangu mwaka 1900, sasa unanchanganya kusema uislam upareni ni 1950s

JE WAJUA UKRISTO NDIYO ILIKUWA DINI YA KWAZA PWANI YA AFRICA MASHARIKI NA VISIWANI IKIWEPO ZANZIBAR KABLA YA UISLAM???
Kama nimeelewa vizuri ni kwamba uislamu ulikuwepo huko tangu mwanzo
Ila walimu wa dini walipelekwa baadae.sijasoma kwamba uislamu uliingia 1900s
 
Kama nimeelewa vizuri ni kwamba uislamu ulikuwepo huko tangu mwanzo
Ila walimu wa dini walipelekwa baadae.sijasoma kwamba uislamu uliingia 1900s
Kinoamiguu,
Ningependa sana kupata historia ya hawa Waislam wa mwanzo Upare na Ugweno kama walijenga misikiti, madrasa nk.

Ikiwa kama taasisi hizi za misikiti na madrasa ilitoa masheikh gani katika historia ya Uislam Tanganyika.

Machame Muislam wa kwanza alikuwa Ngulelo Ndesaruo Mamkinga.

Huyu Ngulelo alisilimu Kismayu wengine wanasema Lamu ambako Wajerumani walimpeleka kifungoni.

Hii ilikuwa mwaka wa 1890.
Ngulelo alikuja kufahamika kama Mangi Selemani.

Mjukuu wake Mangi Selemani nimezungumzanae katika utafiti wa hiki kitabu na alinieleza historia yote ya ukoo wake na uhusiano wao katika dini ya Kiislam.

Narudia tena ningependa sana kupata historia ya Uislam huko Upare ambayo ni tofauti na hii ya Rajabu Kirama.
 
Kinoamiguu,
Ningependa sana kupata historia ya hawa Waislam wa mwanzo Upare na Ugweno kama walijenga misikiti, madrasa nk.

Ikiwa kama taasisi hizi za misikiti na madrasa ilitoa masheikh gani katika historia ya Uislam Tanganyika.

Machame Muislam wa kwanza alikuwa Ngulelo Ndesaruo Mamkinga.

Huyu Ngulelo alisilimu Kismayu wengine wanasema Lamu ambako Wajerumani walimpeleka kifungoni.

Hii ilikuwa mwaka wa 1890.
Ngulelo alikuja kufahamika kama Mangi Selemani.

Mjukuu wake Mangi Selemani nimezungumzanae katika utafiti wa hiki kitabu na alinieleza historia yote ya ukoo wake na uhusiano wao katika dini ya Kiislam.

Narudia tena ningependa sana kupata historia ya Uislam huko Upare ambayo ni tofauti na hii ya Rajabu Kirama.
Umenifundisha mambo makubwa sana.
Hakika wewe ni hazina. Nayapata mafundisho mengi sana
 
Bangusule,
Ahsante kwa mchango wako huu kuhusu Uislam Upareni.

Ikiwa una ithibati na kauli yako kuwa wakati Rajabu Ibrahim Kirama analeta walimu kusomesha Qur'an Upare "...dini ya Kiislam ilikuwa imeota mizizi miaka mingi Upareni..." hakika utakuwa na historia ya kuvutia kupita kiasi.

Ningependa sana kujua historia vipi Uislam uliingia Upare na majina ya masheikh wa miaka hiyo na juhudi zao katika kujenga madrasa na misikiti.

Ningependa pia kujua kujua historia na uhusiano wa masheikh hawa waliokuwapo Upare na harakati za Mzee Rajabu zilizotokea Machame.

Ningependa kujua ni mambo gani walifanya pamoja katika kuujenga Uislam.

Nimesoma katika Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama barua ya tarehe 23 May, 1956 kutoka kwa Sheikh K.S. Kiangi Mswia wa Muslim Association, Ugweno Pare akimwandikia Secretary Abubakar Mariko wa Msikiti Machame, Kalali, Member Muslim Association, Salim Rajabu.

Maudhui ya barua hii ni mkutano ulioandaliwa na Waislam wa Upare kwa madhumuni ya kuimarisha dini kati ya Wachagga na Wapare.

Huyu Salim Rajabu anaeandikiwa barua hii ni mtoto mkubwa wa Rajabu Ibrahim Kirama.

Nimesoma barua nyingine zinazoelezea juhudi za Waislam wa Kilimanjaro, Upare na Usambaa kujenga Muslim Schools na aliyekuwa akisukuma haya yote alikuwa Rajabu Kirama na mwanae Salim.

Historia hii niliyoandika ambayo unaona imepungukiwa itanufaika sana kwa kupata maelezo kutoka kwako kuwa wapo katika historia ya Waislam waliomtangulia Rajabu Kirama Upareni.

wamisionari wa kwanza waliofika upareni wameandika kwamba waliwakuta baadhi ya wapare tayari wakiwa waumini wa dini ya Kiislamu. nitajaribu kuulizia wazee kuhusu kuenea kwa dini ya Kiislamu upareni. kwa kuongezea baadhi Wafumwa / Machifu wa Kipare walikuwa Waislamu hivyo siamini kama harakati za kueneza Uislamu ktk maeneo yetu zilikuwa na changamoto kama alizokutana nazo Rajab Kirama.
 
wamisionari wa kwanza waliofika upareni wameandika kwamba waliwakuta baadhi ya wapare tayari wakiwa waumini wa dini ya Kiislamu. nitajaribu kuulizia wazee kuhusu kuenea kwa dini ya Kiislamu upareni. kwa kuongezea baadhi Wafumwa / Machifu wa Kipare walikuwa Waislamu hivyo siamini kama harakati za kueneza Uislamu ktk maeneo yetu zilikuwa na changamoto kama alizokutana nazo Rajab Kirama.
Bangusule,
Huwezi leo kupata mzee wa kumuuliza historia hii.

Jikite katika kupata nyaraka kama zipo.
Hivi ndivyo utafiti unavyotaka.
 
Bangusule,
Huwezi leo kupata mzee wa kumuuliza historia hii.

Jikite katika kupata nyaraka kama zipo.
Hivi ndivyo utafiti unavyotaka.
kama unataka kuandika historia ya Wapare nakushauri utafute nyaraka za Pare Council ambalo lilikuwa baraza la Wafumwa / Machifu wa Upare.
 
kama unataka kuandika historia ya Wapare nakushauri utafute nyaraka za Pare Council ambalo lilikuwa baraza la Wafumwa / Machifu wa Upare.
Bangusule,
Kwa hivi sasa sina mpango wa kuandika historia ya Wapare.
 
Bangusule,
Kwa hivi sasa sina mpango wa kuandika historia ya Wapare.

basi achana na upotoshaji kwamba Rajabu Kirama ndiye aliyewaingiza Wapare ktk Uislamu. Dini ya Kiislamu iliingia Upareni kabla ya zama za Rajabu Kirama, na kabla ya ujio wa Wamisionari miaka ya 1800.
 
basi achana na upotoshaji kwamba Rajabu Kirama ndiye aliyewaingiza Wapare ktk Uislamu. Dini ya Kiislamu iliingia Upareni kabla ya zama za Rajabu Kirama, na kabla ya ujio wa Wamisionari miaka ya 1800.
Bangusule,
Hapana haja ya kuhamaki.

Ikiwa unaona mimi nimekosea na wewe unazo nyaraka za Pare Council ambazo zina taarifa za historia hii unachotakiwa kufanya ni kuziweka hapa hizo nyaraka.

Ukifanya hivi utakuwa umetusaidia sote ambao tumeegemea Nyaraka za Rajabi Ibrahim Kirama na In Shaa Allah tutakapochapa toleo la pili utaona nimefanya masahihisho na kwa hakika nitataja jina lako katika kitabu kama mtu uliyenisaidia kupatia habari zaidi za historia hii.

Huna sababu ya kuhamaki.
 
Bangusule,
Hapana haja ya kuhamaki.

Ikiwa unaona mimi nimekosea na wewe unazo nyaraka za Pare Council ambazo zina taarifa za historia hii unachotakiwa kufanya ni kuziweka hapa hizo nyaraka.

Ukifanya hivi utakuwa umetusaidia sote ambao tumeegemea Nyaraka za Rajabi Ibrahim Kirama na In Shaa Allah tutakapochapa toleo la pili utaona nimefanya masahihisho na kwa hakika nitataja jina lako katika kitabu kama mtu uliyenisaidia kupatia habari zaidi za historia hii.

Huna sababu ya kuhamaki.

Nimehamaki kwasababu umeandika jambo lisilo la kweli kuhusu Waislamu wa Upareni.
 
Nimehamaki kwasababu umeandika jambo lisilo la kweli kuhusu Waislamu wa Upareni.
Bangusule,
Kama wewe una huo ukweli mbona hujaweka rejea zako kuthibitisha kauli yako?

Mimi nimekuja na kitabu baada ya utafiti.
 
Back
Top Bottom