Kutoka kuwa kiongozi wa mashabiki, hadi scout wa Simba

Kosoa taaluma yake watu waone sababu tujue ni kweli haja qualify kushika nafasi hiyo?

Hayo maswala ya uongozi wa mashabiki sidhani kama yanaweza kumuondolea sifa za kitaaluma ambaza anazo
 
Hili ndio swali ambalo lilitakiwa liulizwe.

By the way nimesoma mahala nimeona ametajwa kuwa ni mzoefu wa ligi hii na soka ka Africa mashariki na kati.
Je kuna jopo la watu wa scouting halafu ndiye mkuu wao, au yeye pekee ndiye atakuwa ana husika kwa moja kwa moja katika scouting?

Kwa sehemu aliyokuwa anaishi kufatilia ligi kuu ya Tanzania moja kwa moja ni ngumu, kwasababu ligi yetu inarushwa na kituo kimoja tu na kina mipaka yake ya kuonekana, ukija kwenye online stream ndio kabisa siku mechi zinakuwepi siku mechi hazioneshwi kwenye Azam max. Watu walishalipiaga kelele humu.

Kuchaguliwa kwa huyu ni labda kwavile ni mpenzi mkubwa wa Simba hivyo pengine atakuwa na uchungu wa klabu na pia labda wameona mzungu mambo yake safi hana shida ndogo ndogo hivyo hawezi kuwa mtu wa 10%
 
Scout bila pesa ni kuwapoza mashabiki na kutoka kapa misimu miwili!, Kwani Simba wanatatizo la scouting? Au Wanatatizo la pesa?

Kama huna pesa hata ungekuwa na scout wa Madrid ni sawa na bure😅, pesa pekee ndio huifanya accounting ya timu kuwa Bora.
 
Je kuna jopo la watu wa scouting halafu ndiye mkuu wao, au yeye pekee ndiye atakuwa ana husika kwa moja kwa moja katika scouting...
Kwa mujibu wa taarifa ilivyowekwa ni kwamba yeye ni mkuu wa scouting ikimaanisha kuna scout wengine zaidi ila yeye ndio muidhinishaji wa mwisho

Huyu hata ukienda kwenye page yake utaona ana uzoefu na ligi yetu, kafanya tour nyingi kwenye timu za hapa nyumbani.

Wasiwasi wangu ni kwamba anaweza kufanya maamuzi sahihi?
 
Kwa mujibu wa taarifa ilivyowekwa ni kwamba yeye ni mkuu wa scouting ikimaanisha kuna scout wengine zaidi ila yeye ndio muidhinishaji wa mwisho....
Kwavile anaipenda timu hilo linawezekana, ila tu jiulize je boss atakuwa yupo taayari kuingia mfukoni kwa wale sahihi watakaopendekezwa? Maana mfuko unavyonona ndipo na watu wa maana unaweza kuwapata.
 
Kwavile anaipenda timu hilo linawezekana, ila tu jiulize je boss atakuwa yupo taayari kuingia mfukoni kwa wale sahihi watakaopendekezwa? Maana mfuko unavyonona ndipo na watu wa maana unaweza kuwapata.
Hivi nyie watu wa Uto mnamchukuliaje Mo?

Mnamuona bahili sana eti?
 
Hivi nyie watu wa Uto mnamchukuliaje Mo?

Mnamuona bahili sana eti?
Hilo limeulizwa katika mfumo wa swali. Na hata hivyo kuna wachezaji waliohusishwa kuja Simba lakini hawakuja sababu ya kutokubaliana katika gharama za usajili. Mfano Manzoki
 
Hilo limeulizwa katika mfumo wa swali. Na hata hivyo kuna wachezaji waliohusishwa kuja Simba lakini hawakuja sababu ya kutokubaliana katika gharama za usajili. Mfano Manzoki
Ishu ya Manzoki ilikuwa ina mambo mengi yaliyoomekana kuwa kikwazo.

Lakini kama ulimsikiliza Mo kwenye zile interviews zake utakuwa ulimsikia alivyosema alitoa bilioni kadhaa kwa ajili ya usajili

Lakini alieleza kuwa kuna tetesi anazisikia ambazo bado yeye hawezi kuzithibitisha zinazodai watu wa ndani ndio waliokuwa wanazipiga hizo hela kwa kuleta wachezaji wa gharama ya chini halafu yeye anaambiwa kuwa amenunuliwa kwa pesa ndefu.

Mpaka hapo utaona ishu sio MO na swala la ubahili, ila kuna watu ambao sio waaminifu ndio wanaokwamisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…