Kutoka pensi ya Zahera mpaka chupi ya Morrison; Kanuni zipi zilitumika kulinda maadili?

Kutoka pensi ya Zahera mpaka chupi ya Morrison; Kanuni zipi zilitumika kulinda maadili?

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
Jana nilimshuhudia Bernard Morrison akivua bukta yake baada ya ushindi na kubakiwa na gguo ya ndani.

Hilo suala la kusherehekea ubingwa kwa staili hiyo si la ajabu machoni mwangu hivyo hata kimjadala halikunistua sana. Kwa haiba ya mchezaji mwenyewe pia halikuwa la ajabu , wengi tunamjua BM23 mambo yake na vituko vyake,"mzee wa kukera".

Leo katika fukunyuafukunyua zangu baada ya hilo suala kuanza kuleta minong`ono nikakutana na kitu kimoja ambacho TFF walishafanya.

Mjadala ulikuwa ni suala alilofanya BM23 nlipo vipi kisheria hapa nchini.

Nilipoenda mbali zaidi nikakutana na adhabu aliyopewa Mwinyi Zahera baada ya kuvaa kaptula uwanjani huko nyuma.

Sasa nimebaki najiuliza itakuwaje kwa mkali BM23 kwa sababu Mwinyi Zahera alikuwa anapenda kuvaa pensi akiwa kocha wa Yanga,kanuni ikatumika,lengo kulinda maadili. Tusubiri tuone nini kitafuata.

Sitaki kuamini kuwa TFF wtakuwa na "Double Standards" , na kama wakimuacha najua watakuja na ufafanuzi mzuri.


Kazi na iendeleee.


pic-kocha.jpg
maxresdefault.jpg
 
KWA SIMBA RUKSA ILA SIO KWA YANGA
TFF ya Wallace Karia imekaa kifala fala sana! Haji Manara anatukana, anakejeli, anatisha watu bila sababu! Lakini hachukuliwi hatua.

Jambo kama hilo hilo akifanya Hassan Bumbuli, anatozwa faini au kufungiwa miaka mitano! Mwamuzi mmoja ndani ya mashindano ya ASFC anachezecha mechi 3 za timu moja! Na mechi zote hiyo timu inashinda!!

Tena kuna mechi moja, anatoa maamuzi ya kutatanisha dk ya 89! Kazi kweli kweli.
 
Nyie lalamikeni tu lakini kombe liko Msimbazi.

Hakuna Mkuu aliyelalamika. Tungejikita kwenye hoja kuliko kwenye Unazi.

uhimu ni kuelimishana hapa zaidi. Sidhani kama Uzi huu umekaa kinazi labda kama wanazi watauingilia
 
Hakuna namna TFF inatakiwa imshushue rungu Morisson bila kupepesa kwani alifanya kitendo cha aibu mbele ya maelfu ya watu waliokuwa uwanjani na mamilioni ya watu walikokuwa wanaufatilia mchezo huo Tanzania na duniani kote kupitia Azam TV. Mbaya zaidi siku hizi mechi za Simba na Yanga huwa zinafuatiliwa watu wa rika mbalimbali mpaka na watoto wadogo kabisa.
 
Yanga mkiishi kwa kuangalia Simba mtaumia sana nafsi zenu,jikiteni kwenye malengo ya timu yenu,Simba ni next level.
 
Jana nilimshuhudia Bernard Morrison akivua bukta yake baada ya ushindi na kubakiwa na gguo ya ndani.

Hilo suala la kusherehekea ubingwa kwa staili hiyo si la ajabu machoni mwangu hivyo hata kimjadala halikunistua sana. Kwa haiba ya mchezaji mwenyewe pia halikuwa la ajabu , wengi tunamjua BM23 mambo yake na vituko vyake,"mzee wa kukera".

Leo katika fukunyuafukunyua zangu baada ya hilo suala kuanza kuleta minong`ono nikakutana na kitu kimoja ambacho TFF walishafanya.

Mjadala ulikuwa ni suala alilofanya BM23 nlipo vipi kisheria hapa nchini.

Nilipoenda mbali zaidi nikakutana na adhabu aliyopewa Mwinyi Zahera baada ya kuvaa kaptula uwanjani huko nyuma.

Sasa nimebaki najiuliza itakuwaje kwa mkali BM23 kwa sababu Mwinyi Zahera alikuwa anapenda kuvaa pensi akiwa kocha wa Yanga,kanuni ikatumika,lengo kulinda maadili. Tusubiri tuone nini kitafuata.

Sitaki kuamini kuwa TFF wtakuwa na "Double Standards" , na kama wakimuacha najua watakuja na ufafanuzi mzuri.

Kazi na iendeleee.

View attachment 1869562 View attachment 1869563
Mi sioni tatizo hapo
 
Watanzania tuna shida sana kichwani; mtu anaulizia suala la kikanuni lakini mwingine anaibukia na picha za wengine wakiwa uchi. Kwahiyo kanuni ya TFF haikujua kua kuna sehemu ukitembea uchi barabarani siyo kosa?
Ujinga ni mzigo.
 
Back
Top Bottom