Kutokana na mwenendo wa Spika wa bunge , Je, kuna haja ya Raia kuendelea kuiheshimu Katiba ya Tanzania ?

Kutokana na mwenendo wa Spika wa bunge , Je, kuna haja ya Raia kuendelea kuiheshimu Katiba ya Tanzania ?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Wakuu naomba kukiri kwamba mimi si mtaalam wa sheria za Tanzania , hivyo uzi wangu waweza kuwa na mapungufu kadhaa , lakini ni dhahiri kwamba kwenye nchi hii sheria za uchaguzi zinawataka wagombea kudhaminiwa na chama cha siasa , kwa maana kwamba ili uweze kukubaliwa na Tume ya uchaguzi kuwa mgombea wa ubunge , udiwani ama Urais unapaswa kuwa mwanachama wa chama cha siasa kilichosajiliwa na Msajili wa vyama vya siasa .

Na kwamba ikiwa utavuliwa uanachama na chama hicho ama wewe binafsi kujivua uanachama basi bila shaka utakuwa umepoteza Ubunge wako na kutotambuliwa kama mbunge .

Cecil Mwambe tunataarifiwa kwamba amerejea bungeni ambako yeye mwenyewe aliondoka baada ya kujivua uanachama wa chama kilichomdhamini baada ya kumuokota barabarani 2015 na kumpa nafasi ya kugombea ubunge wa Ndanda baada ya kutupwa na ccm , na amerejea kwa hisani ya Spika wa bunge hilo Mtukufu Ndugai , kwa kadri ya ufahamu wangu huku ni sawa na kudharau na kusigina kabisa katiba ya nchi , yawezekana mimi labda sielewi , naomba wanasheria mnisaidie , na ikiwa kama spika wa bunge anaamua kunyea katiba ya nchi mnadhani kuna haja ya raia wa kawaida kuiheshimu ?

Nakala : Tundu Lissu
 
....Na kwamba ikiwa utavuliwa uanachama na chama hicho ama wewe binafsi kujivua uanachama basi bila shaka utakuwa umepoteza Ubunge wako na kutotambuliwa kama mbunge .Nakala : Tundu Lissu
Mbali na maneno ya mtandaoni ni nani alimwandikia spika barua rasmi akitoa taarifa ya kujiuzuru au kufukuzwa kwa mbunge!
 
Mbali na maneno ya mtandaoni ni nani alimwandikia spika barua rasmi akitoa taarifa ya kujiuzuru au kufukuzwa kwa mbunge!
ikiwa kama spika anamtambua kama mbunge kwanini asimuadhibu kwa utoro kama alivyoadhibu wabunge wengine ?
 
Lakini ni kiongozi wa bunge ambao ni Mhimili na unafanya maamuzi kwenye nchi , ikiwa kama anaugua kwanini asiondolewe ?

Mbona hata na huo Mhimili mwingine nao una matatizo hayo hayo tu ya Kuugua lakini hauondolewi Ndugu? au hulijui na hili?
 
Unakiri kwamba sheria hufahamu, lakini unatoa conclusions sasa umepataje conclusions pasipo kufahamu sheria husika kwenye hiyo mada yako? Typical JF style ya upotoshaji na majungu. Enjoy it while it lasts.
 
Nyie kikundi cha wahuni ufipa mwisho wenu ni October
 
Unakiri kwamba sheria hufahamu, lakini unatoa conclusions sasa umepataje conclusions pasipo kufahamu sheria husika kwenye hiyo mada yako? Typical JF style ya upotoshaji na majungu. Enjoy it while it lasts.
Uzi unaomba mwongozo wa wanasheria
 
Hakuna kufuta Uchaguzi, hawa walizoea siasa za kudekezwa, this time ni kazi tu, hatuwezi kukubali Tanzania iharibike kisa kikundi cha watu 50 waliopo Ufipa NEVER
Hahaha...kwa mala ya kwanza katika historia ya nchi yetu wapinzani wanatamani Rais afute uchaguzi ili waendelee kuwa wabunge.
 
Hakuna kufuta Uchaguzi, hawa walizoea siasa za kudekezwa, this time ni kazi tu, hatuwezi kukubali Tanzania iharibike kisa kikundi cha watu 50 waliopo Ufipa NEVER
Usibadili ID tu mjomba
 
Wakuu naomba kukiri kwamba mimi si mtaalam wa sheria za Tanzania , hivyo uzi wangu waweza kuwa na mapungufu kadhaa , lakini ni dhahiri kwamba kwenye nchi hii sheria za uchaguzi zinawataka wagombea kudhaminiwa na chama cha siasa , kwa maana kwamba ili uweze kukubaliwa na Tume ya uchaguzi kuwa mgombea wa ubunge , udiwani ama Urais unapaswa kuwa mwanachama wa chama cha siasa kilichosajiliwa na Msajili wa vyama vya siasa .

Na kwamba ikiwa utavuliwa uanachama na chama hicho ama wewe binafsi kujivua uanachama basi bila shaka utakuwa umepoteza Ubunge wako na kutotambuliwa kama mbunge .

Cecil Mwambe tunataarifiwa kwamba amerejea bungeni ambako yeye mwenyewe aliondoka baada ya kujivua uanachama wa chama kilichomdhamini baada ya kumuokota barabarani 2015 na kumpa nafasi ya kugombea ubunge wa Ndada baada ya kutupwa na ccm , na amerejea kwa hisani ya Spika wa bunge hilo Mtukufu Ndugai , kwa kadri ya ufahamu wangu huku ni sawa na kudharau na kusigina kabisa katiba ya nchi , yawezekana mimi labda sielewi , naomba wanasheria mnisaidie , na ikiwa kama spika wa bunge anaamua kunyea katiba ya nchi mnadhani kuna haja ya raia wa kawaida kuiheshimu ?

Nakala : Tundu Lissu
Yaani kwa kitendo hiki cha Spika Ndugai ni dhahiri ameamua kuisigina Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977

Kilichotakiwa ni huyo Spika kuburuzwa mahakamani kwenda kujibu mashitaka yake.......

Hata hivyo ninachohofu ingawa hilo ni kosa straight forward, lakini kwa kadri nchi hii inavoendeshwa hivi sasa, usije shangaa mhimili huo wa mahakama ukaamua "kujivua" wajibu wake kwa kisingizio kuwa wanaogopa kuingilia utendaji wa mhimili huo wa Bunge!
 
Back
Top Bottom