Kutoruhusiwa kutumia Laptop kwenye Internate Cafe

mfianchi

Platinum Member
Joined
Jul 1, 2009
Posts
11,904
Reaction score
8,371
Hapa TZ. Internate cafe nyingi haziruhusu kutumia. Laptops kwenye cafes zao na kama wanarusu basi bei ya muda wa kutumia huwa mara mbili zaidi kulinganisha kama ungetumia PC za cafe sijui tatizo liko wapi,naamini kutokana na mabadiliko ya nyakati ni muhimu watoa huduma au wamiliki wabadilike sioni kwanini kutumia Laptops mtu alipie mara mbili zaidi.
 
Nafikiri hii imekaa kibiashara sana, kwani wanataka utumie Computer zao ili ulipie kuliko kuiba na kutolipia, Jiulize kama wewe ndo mwenye cafe unawateja wawili wanakuja watu kumi wana laptops zao wanataka kutumia bure utafikiliaje? Je utawakubalia watumie na wakati wewe toka asubuhi una wateja wawili tu?
 
 


Hayo Maswahiba yalishanikuta lakini ninachofikiria mimi wanaogopa kuwa utaupdate laptop yako na hivyo utadownload MB nyingi ambapo itakuwa hasara kwao kwani wao wanalipia kwa MB kutoka kwa ISP.

Cha muhimu hapa cafe zetu zijipange kukidhi mahitaji ya anaye kuja na laptop yake. It's true anampunguzia mzigo mwenye cafe na inakuwa more advantage.

Na kama hizo cafe wanalipa kwa MB kutoka kwa ISP wajaribu kuangalia upya mipangilio yao.
 
...Pale Kijitonyama kuna Cafe inafanya hivyo. Unaenda na Laptop yako wanakuchomekea kwenye outlet yao ya internet ila sina hakika kama wanakuchaji kwa muda ama per MB lakini naona wanapata wateja si haba.
 
...Pale Kijitonyama kuna Cafe inafanya hivyo. Unaenda na Laptop yako wanakuchomekea kwenye outlet yao ya internet ila sina hakika kama wanakuchaji kwa muda ama per MB lakini naona wanapata wateja si haba.
Hapo kijitonyama nafikiri ni Stambuli Internate cafe ipo jengo la Millenium karibu na mgahawa wa Steers,tatizo siku hizi hapo imekuwa kijiwe cha masuperstar wa bongo flavour wakija ni hadithi tu za nanihii ananibania,sijui produzya fulani kaiba wimbo fulani etc,pia siku hizi Stambuli Cafe si kama zamani net hukatika mara kwa mara na iko slow saana.Ila bigup kwa staff wa hapo cafe kwani wanajali wateja na huduma zao ni za weredi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…