Kutumia mabavu ili upendwe au utawale ni ugonjwa wa akili

Kutumia mabavu ili upendwe au utawale ni ugonjwa wa akili

green rajab

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
12,387
Reaction score
39,119
Tabia za kidikteta zimeanza kuwaingia viongozi wanaovaa ngozi za kondoo kumbe mioyo yao imejaa uroho wa madaraka na upunguani wa akili.

Watanzania hawakuzoea kusikia au kupitia huu upumbavu unaoendelea haya mambo aliyafanya Iddi Amin Dada miaka ya 70 kipindi anatawala Uganda kimabavu sasa Dunia ya leo Mtu mmoja au kikundi Cha watu kwa maslahi yao na Uroho wa Madaraka kweli wanafikia hatua ya kumshusha Mtanzania mwenzako kwenye basi unaenda kumuua na kumtupa kama kuku.

Hivi Hawa wanaofanya Haya mauaji ni Watanzania wenzetu kweli. Pia ikumbukwe hii roho ya ukatili ya kukamata mtu yoyote na kuua mda wowote mnayowaambukiza Watanzania ikishawaingia mtaweza kuidhibiti kweli.

Soma Pia: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana
 
1725813627761.png
 
roho ya ukatili ikishawaingia watz watashindwa kuwazuia na watakua wamechelewa soon tu
 
Back
Top Bottom