Kutumika kwako ndio kumdatisha uliye naye/ Unaye mtarajia

Kutumika kwako ndio kumdatisha uliye naye/ Unaye mtarajia

mmmuhumba

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2017
Posts
493
Reaction score
478
Kwenye mahusiano yenye afya, vitendo ndio uuza uzuri wa mpenzi na thamani aliyonayo mpenzi. Vitendo husisimua moyo, akili na viungo vya mwili. Akili uwaza, mwili upokea hisia na ulimi unena.

Mwenza bora ugusa hizi sehemu haswa mtu akawa radhi kwa lolote katika mapenzi na maisha Kutumika katika mapenzi namaanisha kitendo cha kujitoa kufanya lolote jema lenye kumfurahisha na kugusa maisha ya mpenzi wako aone kweli umekusudia kuwa wake.

Je kivipi?

Pokea mapenzi kwa kujali uwepo wake umetongozwa/umetongoza na tayari upo katika mahusiano, kusema ndio na nakupenda haitoshi, onyesha kujali kwako kwa kumjulia hali, kumtamani, kummisi, kumpongeza kwa zuri, ishini pamoja kwa kuthaminiana.
Kuna wenza hawataki kuonyesha uwepo wao kimapenzi wakidai wanaogopa, mtu akijua anapendwa anasumbua, sio kweli, mtu anayejua anapendwa huwa jasiri na ujitoka kimapenzi, yuko tayari kutumika nawe.

Fanya vitendo vya mapenzi kijinsia kama ni mwanaume hudumia acha kutegea au kujitoa ufahamu, kiwe kidogo ama kingi fanya pale unapoweza. Kama ni mwanamke jitume unapopokea kuwa wa shukrani na onyesha wewe ni mwanamke wa mtu sio dada kwake. Haja za mapenzi lazima mtimiziane. Kuna mtu anakula vya mtu afu anakaza kama nati ya jembe a trekta, ndio mana wengi huwafika mabaya kwa kukamiwa na wanaume zao au wanawake zao ili tu kukomolewa.

Wapenzi hawasubiri ufanya linalowezekana.
Kuna siri ipo vichwani mwa wapenzi, anayesema anasubiri ni wachache wenye uvumilivu wa haja zao (maana ni watu wazima ) yaani mahitaji yao. Mwanaume akisema anakusubiria tambua atapochoka anatafuta mwingine mwanamke aliyetayari kutumika. Nafasi yako taratibu inapotea kwake badala ya kuwa kipenda roho unakuwa kipoza koo. Kwa wanawake wakisema wanasubiri wakati anatamani kupika na kupakua, basi naye ufanya maisha yake na kujitegemea.

Taratibu thamani ushuka, ndio mana wanasema "wajanja uenda dukani kununua viatu vipya ama mtumba lakini huwa wamevaa viatu sio kwamba uenda peku"
Hivyo atavua vya zamani na kuvaa vipya na akijisikia kumfata anayemsubiri atavivaa vya zamani atakwenda tu kumchora.

Kuwa romantiki/mtu mwenye bashasha/mbwembwe gusa hisi za mapenzi.
Penzi umelitaka mwenyewe unapaswa kumtambua nini anataka mwenzio, wanaume na wanawake wengi wanafeli hapa. Tafuta maneno mazuri, sms nzuri, vizawadi tofauti vya kawaida, shusha sauti ya ukali, tumia mwili wako, ulimi wako na vidole vyako kuzungumza hisia zako. Tambua panapompa raha upaguse ama kinachompa raha uumpe. Wengi uamini nyeti ndio raha ilipo ya mwenza hapana sio kila mtu hisia zake na raha yake ni hapo. Kuna sehemu zingine uliza kwangu utafundashwa.

Jiongeze uelewa
Mwanaume tambua sio wakati wote wanawake uweza kuomba shida zao ila uweza tu kudokeza kimaneno au kivitendo, mfano:
KE: naumwa sko poa.
ME: Pole umepata tiba?.
KE: Bado nataka kwenda ila labda kesho…
Tambua anahitaji fedha ya matibabu hana, sio mpaka aseme. Yako mengi ya kujiongeza iwe chakula, mavazi, vocha na mbaya aisee mwanaume unavua nguo ya ndanii ya mwenza wako na unaiona ina tobo au imepauka hata kununua mpya huwazi, mara ya kumi unamvua tu na anaona hiyo hiyo wee bwana tumika, jiongeze.

Tumika hata kwa wanawake nyeti zako sio dhamana kila mwenye jinsia yako anayo hebu tafuta kingine cha ziada kuonyesha wewe si kama wengine ni mwanamje bora.

Beba ndoto za mwenza wako
mshike mkono kimaendeleo iwe kazi, biashara ama chochote chenye maslahi. Kila mtu utaka unafuu, msaidie na thamani yako itapanda.

Hebu jitathmini je unatumka kuimarisha penzi lako kwa mkeo/mumeo/ mpenzi.
Kwa mwanamke na mwanaume usipotumika kimapenzi na kimaisha huwawezi kumdatisha wala mpenzi wao, zaidi ya kufanywa kama dawa tu kwamba ni ya muda mfupi uiacha, mana kazi yake imeisha.

Kubali kutumia akili zako, mwili wako na uwepo wako kuonyesha uliyemchagua ujafanya bahati mbaya bali umeridhia na unahitaji akupende daima, kumdatisha ni kumpa sababu ya maana uliyenaye kwanini akukose wewe, Mpe kilemba cha heshima mwenza wako, heshima yako aitembelee ajivunie hana anachopoteza kwako zaidi ya kuyajenga maisha na mapenzi bora.
 
Mapenzi hayana fomula mkuu. Kule kwa wakurya (Mara) mwanamke anakatwa Hadi mkono lkn bado ndoa inadumu.

Huku kwenu mwanamke unamnunulia gari, lkn siku akikosa hela ya mafuta ndoa inavunjika. Ujinga mtupu.
 
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana... Alafu hayanaga muongozo...
 
Hakunaga fumyula kwenye mapenzi,unaweza ukamfanyia haya yote na mwisho wa siku akachepuka na punga mmoja wa mtaani kwenu.
 
We labda huishi nchii kwanza huyo utakemfanyia vyote atakushanga badala ya kukupenda atahisi umetumwa nn na akiwa na mshoga zake anakusema yule jamaa anajifanya kadata kweli mi naswali zangu nasubiri wale wanawake wa peponi sisi uzazi wa adam hpn
 
Kwenye mahusiano yenye afya, vitendo ndio uuza uzuri wa mpenzi na thamani aliyonayo mpenzi. Vitendo husisimua moyo, akili na viungo vya mwili. Akili uwaza, mwili upokea hisia na ulimi unena.

Mwenza bora ugusa hizi sehemu haswa mtu akawa radhi kwa lolote katika mapenzi na maisha Kutumika katika mapenzi namaanisha kitendo cha kujitoa kufanya lolote jema lenye kumfurahisha na kugusa maisha ya mpenzi wako aone kweli umekusudia kuwa wake.

Je kivipi?

Pokea mapenzi kwa kujali uwepo wake umetongozwa/umetongoza na tayari upo katika mahusiano, kusema ndio na nakupenda haitoshi, onyesha kujali kwako kwa kumjulia hali, kumtamani, kummisi, kumpongeza kwa zuri, ishini pamoja kwa kuthaminiana.
Kuna wenza hawataki kuonyesha uwepo wao kimapenzi wakidai wanaogopa, mtu akijua anapendwa anasumbua, sio kweli, mtu anayejua anapendwa huwa jasiri na ujitoka kimapenzi, yuko tayari kutumika nawe.

Fanya vitendo vya mapenzi kijinsia kama ni mwanaume hudumia acha kutegea au kujitoa ufahamu, kiwe kidogo ama kingi fanya pale unapoweza. Kama ni mwanamke jitume unapopokea kuwa wa shukrani na onyesha wewe ni mwanamke wa mtu sio dada kwake. Haja za mapenzi lazima mtimiziane. Kuna mtu anakula vya mtu afu anakaza kama nati ya jembe a trekta, ndio mana wengi huwafika mabaya kwa kukamiwa na wanaume zao au wanawake zao ili tu kukomolewa.

Wapenzi hawasubiri ufanya linalowezekana.
Kuna siri ipo vichwani mwa wapenzi, anayesema anasubiri ni wachache wenye uvumilivu wa haja zao (maana ni watu wazima ) yaani mahitaji yao. Mwanaume akisema anakusubiria tambua atapochoka anatafuta mwingine mwanamke aliyetayari kutumika. Nafasi yako taratibu inapotea kwake badala ya kuwa kipenda roho unakuwa kipoza koo. Kwa wanawake wakisema wanasubiri wakati anatamani kupika na kupakua, basi naye ufanya maisha yake na kujitegemea.

Taratibu thamani ushuka, ndio mana wanasema "wajanja uenda dukani kununua viatu vipya ama mtumba lakini huwa wamevaa viatu sio kwamba uenda peku"
Hivyo atavua vya zamani na kuvaa vipya na akijisikia kumfata anayemsubiri atavivaa vya zamani atakwenda tu kumchora.

Kuwa romantiki/mtu mwenye bashasha/mbwembwe gusa hisi za mapenzi.
Penzi umelitaka mwenyewe unapaswa kumtambua nini anataka mwenzio, wanaume na wanawake wengi wanafeli hapa. Tafuta maneno mazuri, sms nzuri, vizawadi tofauti vya kawaida, shusha sauti ya ukali, tumia mwili wako, ulimi wako na vidole vyako kuzungumza hisia zako. Tambua panapompa raha upaguse ama kinachompa raha uumpe. Wengi uamini nyeti ndio raha ilipo ya mwenza hapana sio kila mtu hisia zake na raha yake ni hapo. Kuna sehemu zingine uliza kwangu utafundashwa.

Jiongeze uelewa
Mwanaume tambua sio wakati wote wanawake uweza kuomba shida zao ila uweza tu kudokeza kimaneno au kivitendo, mfano:
KE: naumwa sko poa.
ME: Pole umepata tiba?.
KE: Bado nataka kwenda ila labda kesho…
Tambua anahitaji fedha ya matibabu hana, sio mpaka aseme. Yako mengi ya kujiongeza iwe chakula, mavazi, vocha na mbaya aisee mwanaume unavua nguo ya ndanii ya mwenza wako na unaiona ina tobo au imepauka hata kununua mpya huwazi, mara ya kumi unamvua tu na anaona hiyo hiyo wee bwana tumika, jiongeze.

Tumika hata kwa wanawake nyeti zako sio dhamana kila mwenye jinsia yako anayo hebu tafuta kingine cha ziada kuonyesha wewe si kama wengine ni mwanamje bora.

Beba ndoto za mwenza wako
mshike mkono kimaendeleo iwe kazi, biashara ama chochote chenye maslahi. Kila mtu utaka unafuu, msaidie na thamani yako itapanda.

Hebu jitathmini je unatumka kuimarisha penzi lako kwa mkeo/mumeo/ mpenzi.
Kwa mwanamke na mwanaume usipotumika kimapenzi na kimaisha huwawezi kumdatisha wala mpenzi wao, zaidi ya kufanywa kama dawa tu kwamba ni ya muda mfupi uiacha, mana kazi yake imeisha.

Kubali kutumia akili zako, mwili wako na uwepo wako kuonyesha uliyemchagua ujafanya bahati mbaya bali umeridhia na unahitaji akupende daima, kumdatisha ni kumpa sababu ya maana uliyenaye kwanini akukose wewe, Mpe kilemba cha heshima mwenza wako, heshima yako aitembelee ajivunie hana anachopoteza kwako zaidi ya kuyajenga maisha na mapenzi bora.
uzi mzuri sana....nimejitahidi kuusoma wote. asante ndg.
 
Yote yanawezekana,
Ila sio kizazi hiki Cha michepuko hii tuliyonayo
Kuna wanaume wanachepuka na wanawake ni wadanganji ila wanamipaka alafu hata mwenza wake akiletewa taarifa hawez kukubal kuaminika kwa namna anavyotumikiwa.
Kubwa ni kutimiza wajibu kwa uliyenaye alafu endelea kuchepuka kwa stara.[emoji41]
 
Back
Top Bottom